LAMBERT AMWAGA WINO VILLA PARK
|
Paul Lambert |
Na Juma Mohamed
Meneja wa Aston Villa Paul Lambert ametia saini mkataba mpya wa miaka
minne ambao utamuweka Villa Park hadi Juni 2018, klabu hiyo ya Ligi ya
Premia ilitangaza Jumatano.
Lambert, 45, alichukua hatamu Villa mwaka 2012 na ameongoza klabu
hiyo ya Midlands kuwa katika nafasi ya pili katika ligi kuu ya Uingereza baada
ya mechi nne msimu huu mpya.
“Nimejitolea kuhakikisha tunaendelea kuunda klabu hii hadi ifikie
pale tunapotaka,” Lambert alisema kwa mujibu wa nukuu katika akaunti
rasmi ya Twitter ya Villa.
"Hii ni klabu kubwa, kalbu nzuri sana ya soka, Tunaweza kuangalia
siku za usoni tukiwa na matumaini na hamu ya kufana msimu huu, na misimu
itakayofuata.”
Lambert, aliyekuwa kiungo wa kati wa kimataifa wa Scotland wakati wa
uchezaji wake, alishinda Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya akiwa na Borussia
Dortmund mwaka 1997 na akaanza ukufunzi baada ya kustaafu 2005.
Baada ya kukaa Livingston, Wycombe Wanderers, Colchester United na
Norwich City, alijiunga na Villa Juni 2012 baada ya Alex McLeish
kufutwa.
Villa walimaliza katika nafasi ya 15 misimu ya kwanza miwili ya Lambert kuwa
kwenye usukani, na kuponyoka kushushwa ngazi kwa alama tano nyakati zote
mbili.
Lakini wameanza vyema msimu huu, na walishinda 1-0 wakiwa Liverpool Jumamosi kwenye mechi yao ya majuzi zaidi.
SOURCE: SUPER SPORT
No comments:
Post a Comment