Paul Raphael Kiongera |
Na Juma Mohamed
Straika wa
Simba raia wa nchini Kenya Paul Raphael Kiongera, ataukosa mchezo wa Ligi Kuu
dhidi watani wao wa jadi Yanga utakaofanyika Oktoba 12 katika Uwanja wa Taifa
Dar Es salaam, baada ya kuumia katika mchezo wao wa kwanza dhidi ya Coastal
Union uliomalizika kwa sare ya kufungana magoli 2-2.
Kiongera alipata
jeraha hilo la goti baada ya kugongana na golikipa wa Coastal Union Shabani
Kado, na kulazimika kutoka nje dakika ya 88 baada ya kucheza kwa dakika 21
pekee, baada ya kuingia katika dakika ya 67.
Ripoti zinasema
straika huyo atakuwa nje ya Uwanja kwa wiki 6 hadi 8 kabla ya kuanza mazoezi,
kwa maana hiyo ataukosa mchezo wao dhidi ya Yanga utakaopigwa Oktoba 12.
Amejiunga na
orodha ya wachezaji majeruhi wa Simba ambao ni Issa Rashidi na Haroun Chanongo,
lakini kuna habari njema pia kwa wanamsimbazi kutokana na kurejea kwa kiungo
wao mahiri Jonas Mkude.
Simba wamepiga
kambi visiwani Zanzibar, kujiandaa na mchezo wao unaofuata wa Ligi Kuu dhidi ya
Polisi Moro, utakaopigwa Septemba 27 mwaka huu.
SOURCE: GOAL.COM
No comments:
Post a Comment