Tuesday, May 15, 2012

RYAN GIGGS ATANGAZWA KUWA MCHEZAJI BORA WA MUDA WOTE WA PREMIER LEAGUE - HUKU BABU FERGIE AKIWA KOCHA BORA


Ryan Giggs ametangazwa kuwa mchezaji bora wa muda wote katika historia ya Premier league - huku Sir Alex Ferguson akichukua tuzo kocha bora wa Barclays Premier league history.

Fergie na Giggs wamechukua tuzo hizo wakati ligi hiyo ikisherehekea miaka 20 ya mfumo wa premier league.

Giggs ndio mchezaji aliyecheza mechi nyingi na kushinda makombe mengi ya premier league chini ya uongozi wa Sir Alex Ferguson.

Mchezaji wa zamani wa United na kocha msaidizi wa England Gary Neville alisema: "Ryan Giggs ndio mchezaji kiingereza atakayebakia kuwa aliyefanikiwa zaidi kwa muda wote na sioni mchezaji mwingine wa kuja kuzivunja rekodi zake na kumpita.

"Amevunja na kuzipita kila rekodi katika suala la kuchukua makombe ndani ndani ya mipaka ya nchi hii. Mchezaji ambaye anafurahisha kumuona akicheza kila wiki."

Wakati huo huo kikosi cha Arsenal kilichomaliza ligi bila kufungwa kimetajwa kama kikosi bora - Arsenal walimaliza ligi bila kufungwa mwaka 2003/04.

Alan Shearer alitajwa kama mfungali bora wa muda wote akiwa na magoli 260 - huku David James akitajwa kama golikipa mwenye clean sheets nyingi(173)

Neville, Giggs, na Shearer pia walitajwa kwenye kikosi bora kabisa cha premier league history.

MAKUNDI YA LIGI YA MABINGWA AFRIKA YAPANGWA.

Orange CAF Champions League draw:
Group A
Sunshine (Nigeria)
Esperance (Tunisia)
AS Chlef (Algeria)
ESS (Tunisia)
Group B
Ahly (Egypt)
TP Mazembe (RD Congo)
Berekum Chealsea (Ghana)
Zamalek (Egypt)
Orange CAF Confederation Cup 2nd 1/8 finals
MAS (Morocco) v Léopards de Dolisie (Congo)
El Hilal (Sudan) v CO Bamako (Mali)
AFAD (CIV) v WAC (Morocco)
El Merrikh (Sudan) v Black Leopards (South Africa)
Djoliba (Mali) v Club Africain (Tunisia)
Dynamos (Zimbabwe) v Interclube (Angola)
Stade Malien (Mali) v COD Meknès (Morocco)
Coton Sport (Cameroon) v El Ahly Shandy (Sudan)

TAKWIMU: CRISTIANO RONALDO VS IONEL MESSI - NANI ZAIDI MWEZI WA 5 - NA MSIMU MZIMA.

TAKWIMU ZA MWEZI WA TANO

280 MINUTES PLAYED 279
7 GOALS 3
4 PENALTIES 1
0 ASSISTS 1
15 / 7 (46.7%) TOTAL SHOTS / ON GOAL 25 / 11 (44%)
127 / 104 (81.9%) PASSES / COMPLETED 90 / 61 (67.8%)
7.8 GOAL.COM
AVERAGE RATING
7.0
46 2011-12 LA LIGA GOALS 50
65 (56) 2011-12 COMPETITIVE GOALS (APPEARANCES) 57 (52)
http://i1.goal.com/files/images/stats/goal/team-logos/1/451_48x48.jpg

TAKWIMU ZOTE ZA MSIMU WA 2011-12 LA LIGA

3406 MINUTES PLAYED 3483
50 (37) GOALS (GAMES) 46 (38)
10 PENALTIES 12
15 ASSISTS 12
201 / 98 (48.7%) TOTAL SHOTS / ON GOAL 260 / 103 (39.6%)
2439 / 1995 (81.8%) PASSES / COMPLETED 1529 / 1175 (76.8%)
7.46 GOAL.COM
AVERAGE RATING
7.24
72 (59) 2011-12 COMPETITIVE GOALS (GAMES) 60 (55)
http://i1.goal.com/files/images/stats/goal/team-logos/1/451_48x48.jpg

ANTONIO VALENCIA ATAWALA TUZO ZOTE ZA KLABU YA MANCHESTER UNITED


Usiku wa jana ulikuwa ni bora zaidi kwa kijana kutoka Ecuador bwana Luis Antonio Valencia anayeichezea klabu ya Manchester United baada ya kufanikiwa kuchukua tuzo tatu zinatolewa na klabu hiyo kila mwisho wa msimu. Valencia alishinda tuzo ya goli bora la msimu kwa klabu hiyo alilofunga dhidi ya Blackburn, pia akashinda tuzo ya mchezaji bora anayeteuliwa na wachezaji pamapoja na tuzo ya mchezaji wa mashabiki.
NANI KAWAFUNIKA WENZIE HAPA???/
Bouncebackability: Wayne Rooney delivered a speech to his down-trodden team-matesBouncebackability: Wayne Rooney delivered a speech to his down-trodden team-mates


Phil JonesFederico Macheda
David de Gea

KWA MARA YA KWANZA NDANI YA MIAKA 84 - RONALDO NA MESSI WAFANIKIWA KUWA WACHEZAJI WALIOFUNGA MAGOLI ZAIDI YA 120 KWENYE MSIMU MMOJA.



EUROPE'S GREATEST
GOAL-SCORING SEASONS
PLAYER
GOALS
SEASON
L. Messi (Barcelona)
72
2011-12
G. Muller (Bayern)
67
1972-73
F. Deak (Szentlorinci)
66
1945-46
G. Zsengeller (Ujpest)
65
1938-39
D. Dean (Everton)
63
1927-28
J. McGrory (Celtic)
62
1927-28
C. Ronaldo (Madrid)
60
2011-12
R. Resmja (Tirana)
59
1950-51
J. McGrory (Celtic)
59
1926-27
F. Roberts (Glentoran)
59
1930-31
F. Deak (Ferencvarosi)
59
1948-49

TAARIFA KUTOKA TFF

ASPIRE KUANZA KUSAKA VIPAJI MEI 21
Mchakato wa kusaka vipaji kwa chipukizi wenye umri chini ya miaka 14 kupitia mpango wa kukuza vipaji wa Aspire Football Dream ambao uko chini ya Idara ya Ufundi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) utafanyika kuanzia Mei 21 mwaka huu.
Vituo vitakavyohusika ambavyo kila kimoja kinatakiwa kuwa na watoto wasiopungua 176 na tarahe ya kufanyika mchakato huo kwenye mabano chini mng’amua vipaji (scout) kutoka Hispania ni Morogoro (Mei 21 mwaka huu saa 3 asubuhi) na Bagamoyo mkoani Pwani (Mei 21 mwaka huu saa 8 mchana).
Vingine ni Kawe, Dar es Salaam (Mei 22 mwaka huu saa 3 asubuhi), Makongo, Dar es Salaam (Mei 22 mwaka huu saa 8 mchana) na Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam (Mei 26 mwaka huu saa 9 mchana).

Mpango wa Aspire Football Dream unafadhiliwa na Mtoto wa Mfalme wa Qatar katika nchi 16 duniani kwa Tanzania una jumla ya vituo 14. Vituo vingine ni Kigamboni, Tandika, Ukonga, Kitunda, Mbagala, Magomeni na Tabata.

Watoto watakaochaguliwa katika mchakato huo watakwenda katika mchakato mwingine kwa nchi za ukanda wa Afrika Mashariki utakaofanyika jijini Nairobi, Kenya.

Watakaofuzu kutoka hapo ndiyo watakaokwenda kwenye vituo vya kuendeleza vipaji (centre of excellence) vya Aspire Football Dreams. Aspire ina vituo viwili vya kuendeleza vipaji ambavyo viko Doha, Qatar na Dakar, Senegal.

TWIGA STARS KUJIPIMA KWA BANYANA BANYANA
Timu ya Taifa ya wanawake (Twiga Stars) inatarajia kucheza mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Afrika Kusini (Banyana Banyana) itakayofanyika Mei 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Twiga Stars inayojiandaa kwa mechi ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wanawake (AWC) dhidi ya Ethiopia imeingia tena kambini jana (Mei 14 mwaka huu) kujiwinda kwa mechi hiyo itakayochezwa Mei 26 mwaka huu jijini Addis Ababa.

Banyana Banyana pia iko katika kinyang’anyiro cha kutafuta tiketi ya Fainali za Nane za AWC ambapo katika raundi hii ya pili imepangiwa Zambia na itaanzia mechi hiyo ugenini jijini Lusaka.

Mei 12 mwaka huu Twiga Stars ilicheza mechi ya kimataifa ya kujipima nguvu dhidi ya Zimbabwe (Mighty Warriors) iliyofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Kambi ya timu iko Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Ruvu mkoani Pwani.

Naye Kocha Mkuu wa Twiga Stars, Charles Boniface Mkwasa katika kuimarisha kikosi chake kabla ya mechi ya Jumapili dhidi ya Banyana Banyana amemwita tena kikosi mshambuliaji mkongwe Esther Chabruma.

Wakati huo huo, Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Rwanda kuchezesha mechi hiyo ya AWC kati ya Tanzania (Twiga Stars) na Ethiopia.

Waamuzi hao ni Angelique Tuyishime atakayepuliza filimbi wakati waamuzi wasaidizi ni Sandrine Murangwa, Speciose Nyinawabari na Salma Mukansanga. Kamishna wa mchezo huo wa kwanza ni Catherine Adipo kutoka Uganda.

Mechi ya marudiano itachezwa Dar es Salaam wiki mbili baadaye ambapo mshindi atapata tiketi ya kucheza Fainali za Nane za AWC zitakazofanyika Novemba mwaka huu nchini Equatorial Guinea.

WATUNISIA KUICHEZESHA STARS ABIDJAN
Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limeteua waamuzi kutoka Tunisia na Misri kuchezesha mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia hatua ya makundi kati ya Taifa Stars na Ivory Coast itakayochezwa Juni 2 mwaka huu jijini Abidjan.

Mwamuzi atakuwa Slim Jedidi wakati mwamuzi msaidizi namba moja ni Bechir Hassani, wote kutoka Tunisia. Mwamuzi msaidizi namba mbili ni Sherif Hassan kutoka Misri. Mwamuzi wa akiba ni Youssef Essrayri pia kutoka Tunisia.

Mtathmini wa waamuzi (referee assessor) ni Rachid Medjiba kutoka Algeria wakati Kamishna wa pambano hilo atakuwa Saleh Issa Mahamat kutoka Chad.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

No comments: