PAUL SCHOLES KUREJEA TIMU YA TAIFA
Tetesi za J'tatu magazeti ya Ulaya
VICHWA VYA HABARI VYA
UBINGWA WA MAN CITY ENGLAND:
"Miracle
Manc!" - the Sun
City yamaliza ukame wa ubingwa wa Ligi Kuu wa miaka 44 |
"We
won it in Fergie time" - the Sun
"Foot
of God" - Daily Mirror
"Wincredible
- most amazing title clincher ever" - Daily Star
"Paradise
City" - Guardian
"Over
the blue moon" - Daily Express
"Mancini's
crazy gang make every last second count" - The Times
"Miracle
men - City end 44-year title hoodoo with most dramatic finale in history" -
Daily Telegraph
UNITED, SPURS ZAGOMBEA BEKI LA UFARANSA
Manchester
United na Newcastle zinaandaa uhamisho wa dau la pauni Milioni 6.5 kwa beki wa
kulia wa Ufaransa, Mathieu Debuchy baada ya Lille kusema mchezaji huyo mwenye
umri wa miaka 26 ataruhusiwa kuondoka.
Gwiji
wa Hispania, Raul ameondoka klabu ya Schalke ya Ujerumani, ambako aliibuka
kipenzi cha mashabiki akitupia mipira 27 nyavuni katika mechi 63 za Bundesliga,
akisaini klabu ya Al Sadd ya Qatar.
Derby
imekataa ofa ya pauni Milioni 1.2 kutoka Burnley kwa ajili ya beki wao, Jason
Shackell, mwenye umri wa miaka 28.
Mchezaji
anayewaniwa na Liverpool, Rasmus Elm amewaonya Wekundu hao kwamba fikra ziko
mbali na kuihama klabu yake, AZ Alkmaar ya Uholanzi m simu huu. Mchezaji huyo wa
kimataifa wa Sweden mwenye umri wa miaka 24amesema "anajisikia vizuri
AZ".
Middlesbrough
inavutiwa na mchezaji wa Portsmouth, Luke Varney, mwenye umri wa miaka 29, na
mshambuliaji huyo anaweza kupigwa bei kwa dau la pauni 375,000.
Liverpool
pia inataka kutoa ofa nyingine kwa mshambuliaji aliyefulia wa Manchester United,
Dimitar Berbatov, ambaye amecheza mechi tano tu msimu huu wa Ligi Kuu ya
England.
Mwenyekiti
wa Tottenham, Daniel Levy amesema kwamba hakuna kati ya wachezaji wao tegemeo,
atakayeondoka White Hart Lane msimu huu.
Everton
inataka kumsajili kipa wa Olympiakos, raia wa Hungary, Balazs Megyeri ili akampe
ushindani Tim Howard Uwanja wa Goodison Park. Kipa huyo mwenye umri wa miaka 22,
ambaye anaingia mwaka wa mwisho wa mkataba wake, anaweza kuwagharimu pauni
800,000.
Cardiff
na Ipswich inafanya majadiliano na kipa Joe Lewis, mwenye umri wa miaka 24,
ambaye anajiandaa kuondoka Peterborough kama mchezaji huru.
MANCINI ALIANZIA KANISANI
Kocha
wa Manchester City, Roberto Mancini alikwenda kusali kanisani na wachezaji
wawili kabla ya City kutwaa ubingwa jana, kiaina yake.
Kiungo
wa Manchester United, Paul Scholes, mwenye umri wa miaka 37, amefungua milango
ya mazungumzo na kocha wa timu ya taifa, Roy Hodgson juu ya kurejea kwenye soka
ya kimataifa.
Sir
Alex Ferguson ametoa ujumbe wa wasiwasi kwa mashabiki wa Manchester United,
kwamba Nahodha Nemanja Vidic atakosa ziara ya kujiandaa na msimu
mpya.
Hull
City 'imemtongoza' kocha wa zamani wa Leeds na Sheffield United, Kevin Blackwell
ili awe kocha wao mpya. The Tigers wamemfukuza Nick Barmby wiki iliyopita
No comments:
Post a Comment