Monday, May 14, 2012

ANGALIA NAMNA MAN UNITED WALIVYOJITAHARISHA KUBEBA UBINGWA: HELKOPTA ILIYOBEBA KOMBE YABADILI NJIA MARA 2 NDANI YA DAKIKA 5

False hope: Preparations were made to announce Manchester United as champions before their rivals struck

Huku dakika zikiwa zinasogea kuelekea full time pale Etihad Stadium, mashabiki wa Manchester United walianza kuamini.

Waliamini kwamba timu yao imefanya kitu kilichoonekana hakiwezekani kwa kuchukua ubingwa wa Barclays Premier League mbele ya majirani zao wenye kelele.

Na haikuwa tu mashabiki bali pia hata helikopta iliyobeba kombe halisi ilikuwa imeanza safari kuelekea Stadium of Light. Hata mabango yaliyokuwa yametengenezwa na United kusherehekea ubingwa yalianza kusogezwa uwanjani.

Lakini maili 140 katika jiji la Manchester, saa ikisoma saa 4.52pm, Edin Dzeko akasawazisha na kufanya ubao wa matokeo kusoma 2-2.

Kule Sunderland, mashabiki walikuwa wamebana pumzi zao mpaka kipenga kilipopulizwa, lakini dakika 3 tu baadae, Sergio Aguero akaingia na mpira ndani ya box na kufunga goli na kukamilisha the best comeback.

Wachezaji wa United, ambayo walibaki uwanjani wakisubiri hukumu yao, waliambiwa juu ya kilichotokea Etihad, na kwa haraka sura zao zikawa na majonzi.


False hope: Preparations were made to announce Manchester United as champions

Premature: The stands to hold the Premier League trophy were also constructed at the Stadium of Light


Mixed emotions: Manchester United fans celebrate (above) but then comes the news from the Etihad (below)
Mixed emotions: Manchester United fans celebrate (above) but then comes the news from the Etihad (below)

 Manchester United fans react to news from Manchester City
Defiant: One United fan reminds City that his club are way ahead in the Premier League trophy stakes

Mixed emotions: Manchester United fans celebrate (above) but then comes the news from the Etihad (below)
Mixed emotions: Manchester United fans celebrate (above) but then comes the news from the Etihad (below)

 Manchester United fans react to news from Manchester City
Defiant: One United fan reminds City that his club are way ahead in the Premier League trophy stakes

Na baadae washabiki wa United wakaibuka na bango linaloonyesha 19-3, kwa maana ya kuwadhiaki majirani zao ambao ndio kwanza wamebeba ubingwa wa 3 wakati wao wakiwa tayari na ubingwa wa 19.
Stunned: Manchester United players react to the news that they have lost the Premier League title
Stunned: Manchester United players react to the news that they have lost the Premier League title

Stunned: Manchester United players react to the news that they have lost the Premier League title
So close yet so far: A dejected Sir Alex Ferguson applauds the United crowd at the Stadium of Light


RUUD VAN NISTELROOY ATANGAZA KUTUNDIKA DARUGA!


JOHN BOCCO NA MBWANA SAMATTA WAITWA STARS!


Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen leo (Mei 14 mwaka huu) ametangaza kikosi cha wachezaji 25 kwa ajili ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia hatua ya makundi Kanda ya Afrika dhidi ya Ivory Coast.

Akitangaza kikosi hicho ambacho kitaingia kambini kesho kutwa (Mei 16 mwaka huu, Kim amesema uteuzi wake umezingatia uwezo wa mchezaji uwanjani, nafasi anayocheza na ubora wake.

Wachezaji walioitwa ni makipa; Juma Kaseja (Simba), Mwadini Ally (Azam) na Deogratius Munishi (Mtibwa Sugar). Mabeki ni Nassor Masoud Cholo (Simba), Aggrey Morris (Azam), Amir Maftah (Simba), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Simba), Waziri Salum (Azam), Shomari Kapombe (Simba) na Juma Nyoso (Simba).




Viungo ni Mwinyi Kazimoto (Simba), Salum Abubakar (Azam), Nurdin Bakari (Yanga), Jonas Mkude (Simba), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Edward Christopher (Simba- U20), Mrisho Ngasa (Azam) na Frank Domayo (JKT Ruvu- U20).

Washambuliaji ni Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Ramadhan Singano (Simba-U20), Simon Msuva (Moro United- U20), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Haruna Moshi (Simba) na John Bocco (Azam).

Stars inayodhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Kilimanjaro itacheza mechi ya kirafiki nyumbani Mei 26 mwaka huu dhidi ya Malawi kabla kuivaa Ivory Coast ugenini Juni 2 mwaka huu jijini Abidjan.

No comments: