Kikosi cha Simba |
WEKUNDU wa
Msimbazi, Simba SC leo wana kazi moja tu ya kumalizia kazi waliyoifanya kwa
kiasi kikubwa Dar es Salaam, wiki mbili zilizopita.
Simba leo itakuwa
uwanjani Sudan kumenyana na Al Ahly Shendi ya huko katika mechi ya pili ya raundi
ya tatu ya michuano ya Kombe la Shirikisho.
Simba iliondoka
jijini Jumanne kuelekea Sudan kwa ajili ya mechi hiyo ambapo hata hivyo
hawakupata mapokezi mazuri kutoka kwa wenyeji wao hali ilioufanya uongozi wa
klabu
hiyo kuazimia
kupeleka malalamiko (CAF).
Simba leo inahitaji
ushindi au kama kufungwa isiwe zaidi ya mabao 3-0 ili isonge mbele hatua
inayofuata ya michuano hiyo baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 katika
mechi ya kwanza iliyochezwa wiki mbili zilizopita kwenye Uwanja wa Taifa Dar es
Salaam.
Habari kutoka Sudan
zinasema pamoja na vituko walivyofanyiwa na wenyeji, lakini kikosi cha Simba
kiko imara kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa katika mji wa
Shendi.
Kwa mujibu wa Ofisa
Habari wa Simba Ezekiel Kamwaga Simba imefanyiwa vitendo ambavyo si vya
kiuanamichezo ikiwa ni pamoja na kusafirishwa umbali mrefu, kupewa chakula usiku
sana pamoja na kulazwa kwenye hosteli badala ya hoteli nzuri kama walivyofanyiwa
wao
walipofika nchini.
Kamwaga alisema
wachezaji wako kwenye hali nzuri na kocha Milovan Circovick ameahidi kuibuka na
ushindi.
“Kila kitu chetu
kwa upande wa benchi la ufundi kiko sawa, pamoja na vurugu zao lakini tunaamini
dakika 90 uwanjani ndio zitaongea,” alisema Kamwaga.
“Wachezaji wako
kwenye ari kubwa pamoja na mizengwe ya hapa na pale, kwani hawakukatishwa tamaa
badala yake walifanya mazoezi wenyewe pamoja na kocha kuwapa
mapumziko…
wachezaji wanasema lengo lao ni kuvuka raundi inayofuata na watavuka hata
wakiwafanyiwa vituko,”alisema Kamwaga.
VIKOSI
VYA LEO:
SIMBA
SC:
Kikosi
cha Simba leo kinatarajiwa kuwa; Juma Kaseja. Shomari Kapombe, Amir Maftah,
Victor Costa, Kelvin Yondan, Mwinyi Kazimoto, Uhuru Suleiman, Patrick Mafisango,
Felix Sunzu, Haruna Moshi na Emmanuel Okwi, wakati kwenye benchi watakuwapo Ally
Mustafa
‘Barthez’,
Obadia Mungusa, Juma Jabu, Derrick Walullya na Salum
Machaku.
Al
AHYL SHANDY:
Abdulrahma
Ali, Elnour Altigani, Isaac Seun Malik, Saddam Abu Talib, Fareed Mohamed/Orwah
Ibrahim dk 83, Zakaria Nasu, Razak Yakubu, Faris Abdallah, Hamopuda
Bashir/Mogabid Farouq dk63, Nadir Eltaveb na Bashiro
Ubamba.
Mungu ibariki Simba. Ibariki Tanzania. Amiiin.
SAMATTA, MAZEMBE WATINGA NANE BORA AFRIKA
Sinkala |
TOUT Puissant
Mazembe imefuzu kuingia Nane Bora ya Ligi ya Mabingwa Afrika, kwa mara ya sita
mfululizo baada ya kutoa sare ya 1-1 na wenyeji El Merreikh kwenye Uwanja wa
Omdurman, Khartoum jana, Mazembe, yenye mshambuliaji mwingine Mtanzania, Thomas
Emmanuel Ulimwengu, lakini ‘anasugua mwanzo mwsiho’, ilitangulia kupata bao
kupitia kwa Nathan Sinkala.
Mazembe imefuzu kwa
ushindi wa jumla wa 3-1, baada ya awali kushinda 2-0 nyumbani, Mbwana Ally
Samatta wa Tanzania akifunga bao moja.
Merreikh
ilisawazisha kupitia kwa mchezaji wake Mganda, Mike MUTYABA dakika ya 61.
Kama kawaida,
mshambuliajio chipukizi wa Tanzania, Mbwana Ally samatta alikuwa mwiba mchungu
kwenye safu ya ulinzi ya Merreikh na hata bao la jana lina mchango
wake.
Sasa ni wakati wa
Samatta kujiuza zaidi kupitia mechi sita atakazocheza kwenye hatua ya makundi ya
Ligi ya Mabingwa- na kutokana na ndoto za Mazembe kuchukua ubingwa, kuna
uwezekano kinda huyo wa Tanzania mwishoni mwa mwaka akaweka rekodi ya kuwa
Mtanzania wa kwanza kucheza Klabu Bingwa ya Dunia ya FIFA.
GONGA CHINI KILA PICHA UIONE KWA UKUBWA HALISI Al Merreikh Vs TP Mazembe
UNAYOPASWA KUJUA KABLA YA MAN CITY V QPR LEO
Aguero |
VIKOSI VYA LEO: |
MANCHESTER CITY HartZabaleta, Kompany, Lescott, Clichy Yaya Toure, Barry Nasri, SilvaAguero, Tevez |
QPR
KennyOnuoha, Ferdinand, Hill, Taiwo Mackie, Barton, Derry, Taarabt Zamora, Cisse |
IKIWA
haina mchezaji majeruhi au anayetumikia adhabu, kocha Roberto Mancini hana cha
kuhofia akiwa kikosi kamili katika mechi ya mwisho ya kuwania ubingwa wa Ligi
Kuu England, dhidi ya QPR Uwanja wa Ethiad leo.
Kwa
sababu hiyo, hatutarajii mabadiliko kwenye kikosi cha kwanza cha Manchester City
ikitarajiwa kushusha kikosi kile kile kilichozifunga Manchester United na
Newcastle katika mechi mbili zilizopita.
Kwa
QPR, wote Shaun Derry anayesumbuliwa na maumivu ya mguu na Akos Buzsaky nyama za
paja, wako shakani kucheza, ingawa kocha though Mark Hughes anaweza 'kuwatoa
muhanga' ili kuimarisha safu yake ya kiungo katika mchezo wa leo mgumu
wanaotakiwa kushinda wabaki Ligi Kuu.
Samba
Diakite anayesumbuliwa na virusi, dhahiri ataukosa mchezo huo, wakati Alejandro
Faurlin ataendelea kuwamo kikosini licha ya maumivu ya mguu yanayomkabili.
Djibril Cisse, aliyefunga bao muhimu pekee la ushindi dakika za mwishoni dhidi
ya Stoke City katika mchezo uliopita ugenini, anaweza kuwamo kwenye kikosi cha
kwanza.
JE, WAJUA? |
-
<!--[if !supportLists]-->1. <!--[endif]-->Manchester City wana nafasi kubwa ya kuchukua ubingwa, kwani hata Manchester United wakiifunga Sunderland, wao wakawafunga QPR kipigo kiduchu, wanajivunia wastani wa mabao tisa zaidi walioyonayo hadi sasa dhidi ya wapinzani wao hao.<!--[if !supportLists]-->2. <!--[endif]-->Kikosi cha Roberto Mancini, kimeshinda mechi zao 17 za nyumbani hadi sasa, na matokeo mbaya Etihad hadi sasa ni sare ya 3-3 na Sunderland, Machi 31.<!--[if !supportLists]-->3. <!--[endif]-->Mshambuliaji wa City, Sergio Aguero amefunga mabao mengi zaidi Ligi Kuu msimu huu (22) ambayo ni mabao manne zaidi katika idadi ya jumla ya mabao ya QPR waliyofunga msimu huu.<!--[if !supportLists]-->4. <!--[endif]-->Wenyeji wameshinda mechi zao zote tano zilizopita, wakitisa nyavu za wapinzani mara 15 ndani ya mechi hizo na zao kutikiswa mara moja tu.<!--[if !supportLists]-->5. <!--[endif]-->QPR wamefungwa mechi 10 zilizopita kabla ya kushinda 1-0 dhidi ya Stoke City katika mechi iliyopita.<!--[if !supportLists]-->6. <!--[endif]-->Pointi tatu zitaihakikishia QPR. Sare pia itawasaidia kunusurika kwa wastani mzuri wa mabao - lakini kikosi cha Mark Hughes kikifungwa na Bolton ikaifunga Stoke, wageni watarejea Championship.<!--[if !supportLists]-->7. <!--[endif]-->Tangu ajiunge na klabu hiyo akitokea Lazio, Januari, Djibril Cisse (pichani juu kulia) amekuwa akifunga mabao sambamba na kupigwa kadi nyekundu, hadi sasa akiwa amefunga mabao matano na kupewa kadi mbili nyekundu.<!--[if !supportLists]-->8. <!--[endif]-->Kocha wa QPR, Hughes aliiongoza City kwa miezi 18 kati ya mwaka 2008 na 2009 kabla ya kupigwa chini na nafasi yake kupewa Mancini.<!--[if !supportLists]-->9. <!--[endif]-->Man City wana kawaida ya kuuanza mchezo mtaratibu, huku asilimia nane tu ya mabao yao ndiyo yamepatikana katika dakika 20 za mwanzo kwenye Ligi Kuu, wakati QPR asilimia 25 ya mabao yao ni ya mapema..<!--[if !supportLists]-->10. <!--[endif]-->Yaya Toure alifunga bao la ushindi katika ushindi wa 3-2 wa City mara ya mwisho timu hizo zilipokutana kwenye Uwanja wa Loftus Road,Novemba 5, mwaka jana
No comments:
Post a Comment