SIMBA, YANGA TAJIRI KULIKO BAKHRESA, BASI TU...
KATIKA
sheria 17 za soka, sheria ya kwanza ni Uwanja. Shirikisho la Soka la Kimataifa
(FIFA) linatoa uzito mno katika suala la Uwanja.
Kwa
nini Uwanja? Katika akili ya kawaida, kama tunataka kucheza soka, jambo la
kwanza na la msingi kutilia mkazo ni Uwanja.
Ndiyo,
ni hivyo. Lakini je, viongozi wa klabu zetu kongwe nchini Simba na Yanganao wana
frikra kama hizo? Sidhani. Wakati tumekaribia mno kwenye kilele cha sherehe za
miaka yetu 50 ya Uhuru, Simba na Yanga zinafurajia kuwapo kwa zaidi ya 75 na
ushehe tangu kuanzishwa kwake.
Wakati
huo huo, nchini kuna klabu nyingine za soka zinakimbiza siku ili angalau
zitimize muongo mmoja tu tangu kuanzishwa kwake.
Ila
leo akija mgeni na kutambulishwa kwa klabu zote nchini, zikiwemo ambazo zina
miaka zaidi ya 75 tangu kuanzishwa kwake na zile change, itakuwa vigumu
kumshawishi akubaliane na hali halisi.
Mpokee
mgeni na uanze kumtembeza- anzia Mtaa wa Msimbazi, muonyeshe makao makuu ya
klabu ya Simba, ajionee lile jingo chakavu na lile pembeni yake ambalo
halijaisha.
Mtoe
hapo mpelekea makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani- muonyeshe makao makuu ya
klabu ya Yanga- ajionee eneo kubwa linaloweza kuwa la kifahari siku moja tu,
akipatikana mtu wa kuliendeleza.
Baada
ya hapo, mpeleke Mbagala, eneo la Chamazi ambako kuna makao makuu ya Azam FC na
muonyeshe Uwanja mpya mdogo na wa kisasa mithili ya viwanja vingi ambavyo vipo
nchi za Scandinavia barani Ulaya.
Mkutanishe
na Patrick Kahamele, amtembeze kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo ya soka
klabu, ikiwemo soka ya vijana.
Mkutanishe
na wenye timu wampe mipango yao ya baadaye- tena iliyo katika maandishi na
mikakati ya utekelezaji wake.
Baada
ya hapo mpe wasifu wa hizo klabu kwamba Simba na Yanga zipo tangu nchi hii
haijapata Uhuru na Azam haina hata miaka mitano tangu
ianzishwe.
Lazima
atashangaa. Lazima atastaajabu. Hii nini maana yake? Viongozi wa Simba na Yanga
bado hawajajitambua. Bado hawajatambua soka inahitaji vipaumbele gani na kama
hivyo ndivyo.
Inaonekana
dhahiri viongozi wa Simba na Yanga hawana dira wala mipango na watu wa aina
hiyo, kutoka mikononi mwao ni vigumu mno klabu hizo kupiga hatua, hata ndogo
ndogo tu za kimaendeleo.
Ukubwa
wa majina ya Simba na Yanga na umaarufu wake, pekee ni mtaji mkubwa wa kuendesha
klabu hizo, ambao inasikitisha hadi haujatumiwa na viongozi wa klabu hiyo
kuzinufaisha klabu hizo.
Bado
inasikitisha kuona hadi kesho, kitegauchumi kikubwa cha Simba na Yanga ni
‘bakuli’- yaani kutembea kwa matajiri na wafanyabiashara kuomba
misaasa.
Kwa
sasa Yanga wana mgogoro na chanzo ni hali mbaya ya kifedha ndani ya klabu, kama
ilivyoanishwa na Wajumbe wawili waliong’atuka, Seif Ahmad ‘Magari’ na Abdallah
Bin Kleb na wakati Fulani ilibidi Mwenyekiti wa Yanga, Wakili Lloyd Baharagu
Nchunga aende kumbembeleza Yussuf Manji arejeshe ufadhili wake kwenye klabu
hiyo.
Dhahiri,
Nchunga aliamua kufanya hivyo baada ya kuona mambo ni magumu na klabu haiwezi
kujiendesha bila msaada.
Lakini
Nchunga labda tu awe hajui historia ya klabu yake- ni klabu ambayo hadi mwaka
1975, ikiwa haina ufadhili wowote, tayari ilikuwa ina majengo yake mawili, dogo
Mtaa wa Mafia na hilo kubwa la Jangwani, ambalo linaambatana na Uwanja wa
Kaunda.
Ilikuwa
ina mabasi yake ambayo mengine yalikuwa yanatumika kwa shughuli za klabu na
mengine yanatumika kibiashara.
Kadhalika
kwa Simba, hadi 1975 ilikuwa ina jengo lake wakati huo likiwa la kifahari na
linalong’ara na kuupendezesha Mtaa wa Msimbazi- miaka hiyo Mwenyekiti wa Simba
Alhaj Ismail Aden Rage aliwahi kufika Dar es Salaam na kujaribu kutaka kuichezea
klabu hiyo, lakini kiwango chake kidogo hakikumpa nafasi, aliishia kujaribiwa
kwenye mechi kadhaa.
Simba
ilikuwa ina mabasi pia- na haikuwa na mfadhili yoyote, zaidi ya ujanja na fikra
za viongozi wa klabu hiyo.
Unaweza
kuona kabisa hali ilivyo leo Simba na Yanga ukilinganisha na miaka hiyo, maana
yake haziendelei zaidi ya kudumaa. Wengi wanaamini elimu kubwa ndio msingi wa
maendeleo- sahihi kabisa. Leo viongozi wa Simba na Yanga ni wenye elimu za
viwango vya juu na wana taaluma. Rage Mhasibu na Nchunga
Mwanasheria.
Lakini
viongozi wa Yanga wa miaka hiyo, hawakuwa na elimu kubwa, ila mambo
waliyoyafanya yanawafanya thamani yao iwe juu kuliko hawa waliokaa shule muda
mrefu.
Dunia
ya leo ni nyepesi mno kwa mtu ambaye kweli anataka maendeleo. Taasisi kubwa kama
zilivyo Simba na Yanga hivi sasa zinakopesheka na mabenki ni mengi mno nchini
ambayo yanaweza yakazipa mikopo klabu hizo zifanye miradi yao ya
maendeleo.
Yanga
wana Uwanja wa Kaunda ambao wanaweza kuuboresha, ukawa Uwanja wa kisasa wenye
uwezo wa kukusanya hata watu 20, 000 katika mechi moja na kuujingizia fedha
nyingi.
Hivi
kweli Yanga wamekwishazungumza hata na mdhamini wao tu Kilimanjaro Beer juu ya
kuwasilisha programu ya kuuendeleza Uwanja wa Kaunda?
Naamini,
TBL watakuwa tayari kutumia kuta za Uwanja wa Kaunda kujitangaza kibiashara-
iwapo Yanga watawasilisha mapendekezo ya mradi
yaliyosimama.
Watu
20,000 kila wiki mara mbili wanamiminika Uwanja wa Kaunda kutazama mechi- au
watu wasiopungua 5,000 kila siku kwenye mazoezi ya kikosi cha kwanza- ni kiasi
gani TBL itakuwa inanufaika?
Lakini
Yanga nayo itakuwa inapata kiasi cha fedha?
Azam
‘walilaani’ kweli Uwanja wa Taifa ulipofunguliwa, kwani yale makato ya Uwanja
waliyokuwa wanayapata kila mechi ambayo SImba au Yanga ilicheza Chamazi yaliota
mbawa. Sasa tunataka nini ili kujua umuhimu wa kuwa na Uwanja?
Lakini
si TBL tu, yapo makampuni mengine ambayo yanajua soka ina wapenzi wengi na
yanaweza kunufaika kwa kuwekeza huko, je Yanga
wamekwishayafikia?
Mradi
wa ujenzi barabara ya Jangwani inalifanya eneo hilo liwe mjini kabisa na kuuweka
sokoni zaidi Uwanja wa Yanga- je Nchunga na viongozi wenzake wanafikiria
nini?
Azam
wamejenga Uwanja wao Mbagala na tumeshuhudia msimu huu mashabiki wa Simba na
Yanga wakienda kuzishangilia timu zao kwenye Uwanja huo, inakuwaje Simba
wanashindwa kujenga Uwanja nje ya mji japokuwa walishindwa kuwa na eneo
mjini?
Soka
ni biashara kubwa ambayo mtaji wake mkuu ni Uwanja- ndio maana klabu zote Ulaya
hata ndogo zina viwanja vyake. Ulaya itaendelea kuwa kioo chetu
daima.
Wanachokifanya
Rage na Nchinga kwa sasa ni kitu ambacho hata Rashid Ngozoma Matunda (sasa
marehemu) na Hassan Daalal walikifanya klabu yao.
Uongozi
wa staili ya kusajili wachezaji, kuweka timu kambini, kuisafirisha mikoani
kucheza mechi na kukusanya mapato ya milangoni, hata yule mwanachama wa Simba
mlemavu anayeitwa Kipukuswa au Soud Tall wa Yanga wanaweza
kuufanya.
Nani
atashindwa? Lakini Rage na Nchunga wanapaswa kujitambua sasa na kuhakikisha
wanafanya kitu ambacho kitawafanya wakumbukwe na kuwa sehemu ya historia ya
klabu hizo.
Wasome
historia ya Simba na Yanga na baada ya hapo waache blah blah na usanii, ni mambo
ambayo yamekwishapitwa na wakati.
Waonyeshe
wanajiamini na kutumia ukubwa wa majina ya klabu hizo na umaarufu wake kuzipatia
mafanikio klabu hizo.
Ona
sasa Azam inayowaacha ‘uchi’- timu ya juzi tu, lakini ina mipango. Na hapa
kisingizio kisiwe Bakhresa ana fedha hapana, ana mipango na malengo, kwani wapo
wenye fedha waliojaribu kuwekeza kabla yake, mfano Mohamed Dewji, Alex Kajumulo
na Merey Balhaboub na wakafeli.
Bado
naamini Simba na Yanga kila moja ni tajiri kuliko Bakhresa, ila sasa hazina watu
wenye kuweza kuchimba dhahabu, kusafisha na kuiingiza sokoni. Na kwa mtaji huu,
zitaendelea kuwa za kubahatidha tu- mfano Simba mwaka huu wanafanya vizuri
Afrika, baada ya hapo hadi miaka 10 tena baadaye.
Ndiyo-
nani asiyejua mafanikio ya Simba ni ya kubahatisha? Walikuwa wana mipango gani
mwanzoni mwa msimu hata tuseme wanavuna walichopanda? Weka unazi kando- jadili
hili kwa kina, ukirejea ule usajili wa kubahatisha bahatisha- ambao chupuchupu
umtupe nje ya kikosi Emmanuel Okwi msimu huu, ambaye sasa ndiye anaibeba
timu?
Au
tumesahau jamani, huyu mchezaji si alikwenda Afrika Kusini na klabu ilikuwa
tayari kumuuza kwa kumuona hana manufaa, ila alipokwama kwa sababu alikuwa
hajamaliza mkataba, akaambiwa arejee kikosini.
Umefika
wakati sasa tuweke unazi kando ili kuzisaidia SImba na Yanga- zinatia
kichefuchefu, tunazipenda basi tu!
RATIBA YA MECHI ZA KUFUNGA MSIMU ENGLAND LEO NA MUDA KIBONGOBONGO, MSIMAMO NA WAFUNGAJI WOTE WA MABAO
Silva na Tevez wa Man City, inayotarajiwa kutwaa ubingwa leo |
Barclays Premier League | RATIBA
Mechi zote Live Super Sport TV
Sunday 13 May 2012 |
Chelsea | v | Blackburn | Stamford Bridge | Saa11:00jioni | |
Everton | v | Newcastle | Goodison Park | Saa11:00jioni | Preview |
Man City | v | QPR | Etihad Stadium | Saa11:00jioni | Preview |
Norwich | v | Aston Villa | Carrow Road | Saa11:00jioni | |
Stoke | v | Bolton | Britannia Stadium | Saa11:00jioni | |
Sunderland | v | Man Utd | Stadium of Light | Saa11:00jioni | Preview |
Swansea | v | Liverpool | Liberty Stadium | Saa11:00jioni | |
Tottenham | v | Fulham | White Hart Lane | Saa11:00jioni | Preview |
West Brom | v | Arsenal | The Hawthorns | Saa11:00jioni | Preview |
Wigan | v | Wolverhampton | The DW Stadium | Saa11:00jioni |
Barclays Premier League | MSIMAMO
Pos | Team | P | W | D | L | GF | GA | GD | Pts |
1 | Man City | 37 | 27 | 5 | 5 | 90 | 27 | 63 | 86 |
2 | Man Utd | 37 | 27 | 5 | 5 | 88 | 33 | 55 | 86 |
3 | Arsenal | 37 | 20 | 7 | 10 | 71 | 47 | 24 | 67 |
4 | Tottenham | 37 | 19 | 9 | 9 | 64 | 41 | 23 | 66 |
5 | Newcastle | 37 | 19 | 8 | 10 | 55 | 48 | 7 | 65 |
6 | Chelsea | 37 | 17 | 10 | 10 | 63 | 45 | 18 | 61 |
7 | Everton | 37 | 14 | 11 | 12 | 47 | 39 | 8 | 53 |
8 | Liverpool | 37 | 14 | 10 | 13 | 47 | 39 | 8 | 52 |
9 | Fulham | 37 | 14 | 10 | 13 | 48 | 49 | -1 | 52 |
10 | West Brom | 37 | 13 | 8 | 16 | 43 | 49 | -6 | 47 |
11 | Sunderland | 37 | 11 | 12 | 14 | 45 | 45 | 0 | 45 |
12 | Swansea | 37 | 11 | 11 | 15 | 43 | 51 | -8 | 44 |
13 | Norwich | 37 | 11 | 11 | 15 | 50 | 66 | -16 | 44 |
14 | Stoke | 37 | 11 | 11 | 15 | 34 | 51 | -17 | 44 |
15 | Wigan | 37 | 10 | 10 | 17 | 39 | 60 | -21 | 40 |
16 | Aston Villa | 37 | 7 | 17 | 13 | 37 | 51 | -14 | 38 |
17 | QPR | 37 | 10 | 7 | 20 | 41 | 63 | -22 | 37 |
18 | Bolton | 37 | 10 | 5 | 22 | 44 | 75 | -31 | 35 |
19 | Blackburn | 37 | 8 | 7 | 22 | 47 | 76 | -29 | 31 |
20 | Wolverhampton | 37 | 5 | 10 | 22 | 38 | 79 | -41 | 25 |
Barclays Premier League | WAFUNGAJI WA MABAO
Van Persie anayeongoza kwa mabao |
Player | Team | Goals |
Robin van Persie | Arsenal | 30 |
Wayne Rooney | Man Utd | 26 |
Sergio Aguero | Man City | 22 |
Clint Dempsey | Fulham | 17 |
Ayegbeni Yakubu | Blackburn | 16 |
Demba Ba | Newcastle | 16 |
Emmanuel Adebayor | Tottenham | 16 |
Grant Holt | Norwich | 14 |
Edin Dzeko | Man City | 13 |
Mario Balotelli | Man City | 13 |
Papiss Cisse | Newcastle | 13 |
Daniel Sturridge | Chelsea | 11 |
Danny Graham | Swansea | 11 |
Frank Lampard | Chelsea | 11 |
Luis Suarez | Liverpool | 11 |
Rafael Van der Vaart | Tottenham | 11 |
Steven Fletcher | Wolverhampton | 11 |
Gareth Bale | Tottenham | 10 |
Javier Hernandez | Man Utd | 10 |
Jermain Defoe | Tottenham | 10 |
Peter Crouch | Stoke | 10 |
Peter Odemwingie | West Brom | 10 |
Danny Welbeck | Man Utd | 9 |
Darren Bent | Aston Villa | 9 |
Steve Morison | Norwich | 9 |
Total | 996 |
No comments:
Post a Comment