Tetesi za Jumanne magazeti Ulaya

JUVENTUS KUMNG'OA DZEKO MAN CITY

KLABU ya Juventus itahamishia mawindo yake kwa mshambuliaji Manchester City, Edin Dzeko mwenye umri wa miaka 26, wakati wakijiandaa kujitoa kwenye mbio za kuwania saini ya mshasmbuliaji wa Arsenal, Robin van Persie mwenye umri wa miaka 28.
MANCHESTER City inajipanga vema kutumia mwanya wa Juve kujitoa kwenye mbio za kumuwania Van Persie, wakati Kibibi Kizee hicho cha Turin inaelezwa kinaweza kuhamishia mawindo yake kwa mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez mwenye umri wa miaka 25 sambamba na Dzeko.
KLABU ya Tottenham inamtaka mshambuliaji mwenye umri wa miaka 25-wa Marseille, Loic Remy na inaweza kubadilishana mchezaji wake Luka Modric mwenye umri wa miaka 26, kwa mchezaji wa Real Madrid, Lassana Diarra mwenye umri wa miaka 27.
QPR inatarajiwa kufanya usajili wa nguvu kwa kumchukua kipa mkongwe wa Aston Villa, Shay Given mwenye umri wa miaka 36, ambaye alicheza chini ya kocha wa Rangers, Mark Hughes katika klabu ya Manchester City. Mchezaji mwenye umri wa miaka 31 wa West Ham, Robert Green naye anaweza kuingia rada hizo.
Shay Given
Kipa mkongwe Given.
KLABU iliyorejea Ligi Kuu ya England, West Ham, wameingiwa na hofu ya kumpoteza nyota wao Robert Green kutokana na kudai mshahara mkubwa.
KOCHA wa QPR, Hughes pia anaweza kuhamishia ndoana zake kwa mshambuliaji wa Wigan, Victor Moses mwenye umri wa miaka 21.
MMILIKI wa Chelsea, Roman Abramovich ametoa ruhusa klabu kusajili mchezaji yeyote bila kujali gharama, akiwemo nyota wa Lille, Eden Hazard, mwenye umri wa miaka 21, mshambuliaji wa Porto, Hulk mwenye umri wa miaka 25, na mshambuliaji wa Atletico Madrid, Radamel Falcao mwenye umri wa miaka 26.
KLABU ya Barcelona inajiandaa kutoa ofa ya pauni Milioni 10 kumnasa beki Muargentina wa Manchester City, Pablo Zabaleta, mwenye umri wa miaka 27.
KLABU ya Chelsea imeipa Arsenal hadi wiki ijayo kutoa jibu kama inataka kumsajili moja kwa moja kiungo wanayemtupia kwa mkopo hivi sasa, Myahudi Yossi Benayoun mwenye umri wa miaka 32.
MWENYEKITI wa Tottenham, Daniel Levy amesafiri hadi Uholanzi jana kufanya mpango wa kumsajili beki Mbelgiji wa Ajax, Jan Vertonghen mwenye umri wa miaka 25, ambaye pia anatakiwa na klabu za Arsenal na AC Milan.
KLABU ya Blackpool ya Daraja la Kwanza England, inataka kumchukua moja kwa moja mshambuliaji mwenye umri wa miaka 29 wa Swansea, Stephen Dobbie wanayemtumia kwa mkopo hivi sasa.

MARTINEZ KATIKA KIKAO KINGINE NA WAMILIKI WA LIVERPOOL MAREKANI

Roberto Martinez
Martinez has been in charge of Wigan for three years
KOCHA Roberto Martinez anajiandaa kukutana na wamiliki wa klabu ya Liverpool Marekani kesho, baada ya kufanya nao mazungumzo ya awali England mwishoni mwa wiki.
KOCHA wa zamani wa England, Fabio Capello anaimezea mate nafasi hya kazi iliyo wazi Uwanja wa Anfield, lakini hana mawasiliano na Liverpool.
KLABU ya Chelsea imejifanya kama haijasikia lolote kutoka kwa mshambuliaji wake Fernando Torres aliyelalamikia maisha yake asiyoyafurahia Stamford Bridge, lakini imemuambia Mspanyola huyo mwenye umri wa miaka 28, kwamba haendi popote.
MMILIKI wa Chelsea,Roman Abramovich binafsi amemuhakikishia maisha bora Torres katika mustakabali wake Chelsea.
Randy Lerner atasafiri hadi England kesho, wakati Aston Villa ikikaribia kumalizana na kocha mpya. Kocha wa Molde, Ole Gunnar Solskjaer ndiye anapewa nafasi hiyo lakini Kocha wa Norway, Paul Lambert na kocha wa Brighton, Gus Poyet pia nao wanapewa nafasi.
KIUNGO Joe Cole anafikiri anaweza kuwa na mafanikio Liverpool, lakini tu iwapo atacheza dimba la kubwa.

BALOTELLI AKOROFISHANA NA NYWELE ZAKE SASA

BAADA ya kuambia aepuke matatizo na kocha wa Italia, Cesare Prandelli, mshambuliaji chipukizi Mario Balotelli amekuwa akijaribu mitindo mbalimbali ya mikato ya nywele, ukiwemo wa Carlos Valderrama