Tuesday, April 24, 2012

Tuesday, April 24, 2012



SIKU SABA BAADA YA CHELSEA KUPIGA SHUTI MOJA NA KUPATA GOLI HUKU BARCA WAKIPIGA MASHUTI 24 BILA GOLI - TIMU HIZI MBILI ZINARUDAIANA LEO NOU CAMP - NANI KUTINGA FAINALI

Siku saba baada ya takwimu za shuti moja bao moja kwa Chelsea na mashuti 24 bila mabao kwa Barcelona kwenye uwanja wa Stamford Bridge, timu hizi zinarudiana kwenye uwanja wa Nou Camp.

Barcelona wamekuwa kwenye wakati mgumu baada ya kufungwa mechi mbili mfululizo huku nyota wake Lionel Messi akisindwa kung'aa kwenye kwenye mechi zote mbili.
Chelsea walipoifunga Barca mapema wiki iliyopita wengi waliona kuwa timu hii toka London imepanda baiskeli ya miti na Barcelona ingeshinda kiwepesi mchezo wa marudiano.

Hata hivyo kipigo cha kwenye El Classico kimewaweka Barca kwenye hali tofauti ya kisaikolojia ambayo inaweza kuwa sababu ya aidha kushinda au kufungwa kwenye mchezo wa marudiano.
Ukirudi nyuma na kutazama sababu ambazo zinaweza kuwa zimeipelekea Barca kufungwa michezo yote miwili na kuzichanganya kwa pamoja hapa ndio unapoweza kugundua hali ngumu waliyo nayo Barca hii leo.

Kwenye mechi ya jumatano iliyopita mfumo waliotumia Chelsea na bahati kwa pamoja viliwasaidia vijana wa Di Matteo. Mfumo aliotumia siku hiyo ulikuwa rahisi, kuta mbili za wachezaji wanne kila moja nyuma ya mpira na kujaribu kupunguza nafasi ya Barca kufaidi kumiliki mpira kuanzia katikati mwa uwanja kuelekea liliko lango la Chelsea.

Pamoja na hilo , Di Matteo aliwaelekeza viungo Raul Meireles na John Obi Mikel kuhakikisha wanakufa na Lionel Messi ,Xavi na Andres Iniesta huku Ramires akifanya kazi ya kuua mashambulizi ya upande wa kulia aliko Mbrazil mwenzie Dani Alves.

Mbinu hizi zilifaulu kwa kusaidiwa na ari waliyokuwa nayo Chelsea kisaikolojia pamoja na bahati iliyokuwa upande wao kwani ukiachilia mbali jinsi Chelsea walivyoshinda huwezi kusahau mara ambazo Barca waligongesha mwamba na mara ambazo Petr Cech alifanya kazi ya ziada kuokoa au mabeki kina Ashley Cole wakiondosha hatari langoni mwao.

Kwenye mchezo dhidi ya Real , Barca waligharimiwa sana na kuwakosa watu mbadala wanaoweza kufanya kazi ya ufungaji zaidi ya Lionel Messi.

Huwezi kuacha kufikiri kuwa nafasi mbili alizopata Christian Tello na kushindwa kuzitumia zingekuwa zimetumiwa vyema na mtu kama Pedro au David Villa . Pengo la David Villa limeonekana sana kwenye El Classico na kuna kila uwezekano kuwa endapo Chelsea watafuzu basi pengo hilo litaonekana kwenye mchezo huo pia.

Pamoja na hayo Real walikuwa na aina ya uzoefu na uwez wa kutumia nafasi chache za kufunga walizozipata jambo ambalo si timu nyingi zinazocheza na Barca zinafanya. Ukiwaangalia Barcelona wenyewe kama Barcelona kuna baadhi ya viashiria mbalimbali ambavyo vilionyesha kuwa hawako mchezoni siku ya jumamosi.

Lionel Messi hana kawaida ya kuwa mlalamishi lakini alilalama kwa waamuzi kuliko mchezaji yoyote siku ile na hata Xavi na wengineo walikuwa wanaonekana kupagawa jambo ambalo linakufanya uhisi kuwa ile hali ya woga ambayo timu pinzani inakuwa nazo ikicheza dhidi ya Barca inakuwa nayo imehamia kwa Barcelona wenyewe.

Safu ya ulinzi nayo imekuwa tatizo kubwa . Carles Puyol anastahili kubeba lawama kwenye mabao yote matatu ambayo Barca imeruhusu kwenye michezo miwili iliyopita na endapo atacheza tena huenda Di Matteo akawaelekeza wachezaji wake kupeleka presha kwenye upande wake.

Hata hivyo Barcelona wanabaki kuwa timu yenye uwezo hata pale ambapo wanapitia kwenye kipindi kigumu kama livyokuwa kwenye msimu huu na quality yao pekee ambayo dhahiri shahiri ni bora kuliko ya Chelsea inaweza kutosha kugeuza matokeo.
Kikubwa kitakachoamua mchezo ni hali ya kisaikolojia ya wahezaji a Barcelona.

Wanapaswa kuacha yaliyotokea kubaki huko nyuma yaliko na ku-deal na mchezo wa leo kama wa leo . Endapo wataruhusu kuingiwa na hali ya woga kwa maana wanaweza kufungika kirahisi.

Kwa hali ya kawaida Barcelona ni washindi na hiki ni kitu ambacho wahezaji wanaingia nacho uwanjani kwa kuwa wana "winning mentality" . Ila hiyo hiyo mentality inaweza kuondoka na swali ambalo kila mmoja anajiuliza ni kama hiyo winning mentality ipo baada ya michezo miwili migumu ambayo Blaugurana wamefungwa?

Chelsea wana nafasi finyu ya kupata ushindi kwenye mchezo wa leo na nafasi pekee kubwa waliyo nayo ya kusonga mbele ni kutafuta bao la ugenini huku wakilinda kwa nidhamu kama waliyolinda nyo kwenye mchezo wa Stamford Bridge.

Tetesi toka kwenye magazeti ya Hispania kwa masaa 24 yaliyopita zimekuwa zikisema kuwa Lionel Messi hayuko kwenye physique nzuri , pengine michezo imekuwa mingi mfululizo pengine kama ilivyo kwa kila binadamu wachezaji wa Barcelona wamechoka baada ya kuwa na msimu ambao mambo yamekuwa magumu kwao?
Haya ni maswali ambayo majibu yake yatapatikana ndani ya masaa machache yajayo.

Monday, April 23, 2012


CHELSEA KULAMBA £10 MILLIONI WAKIWATOA BARCA NA KUCHUKUA UBINGWA WA ULAYA.

Wachezaji wa Chelsea wamehaidiwa na bosi wao Roman Abramovich kupata bonasi ya £10 million ikiwa watafanikiwa kuifunga Barca, kisha kwenda fainali na kuchukua ubingwa wa kwanza wa ligi ya mabingwa wa ulaya katika historia ya timu hiyo.

According to gazeti la The Sun la Uingereza ikiwa Chelsea watafanikiwa kuchukua kombe hilo watapewa kiasi hicho cha fedha huku manager wao wa muda Roberto Di Matteo nae hatoondoka mikono mitupu.

Kila mchezaji wa kikosi cha wachezaji 25 atapokea kiasi cha £350,000 ikiwa watafanikiwa kubeba kombe la ulaya pale Allianz Arena mwezi ujao.
Roberto Di Matteo ambayo bado hajapokea ongezeko la mshahara ukiachana na 1.2millionaliyokuwa akilipwa kwa mwaka kama kocha namba 2 nyuma ya Villas Boas.

Bonasi yake itajadiliwa katika kikao cha baina yake na mmiliki wa The Blues.

Hata hivyo taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo zinasema kiungo huyo wa zamani wa klabu atavuta mkwanja unaofikiwa paundi 500,000 kama shukrani kwa kugeuza msimu wa Chelsea - japokuwa bado hajapewa uhakika wa kupewa kazi ya moja kwa moja kama kocha mkuu.

Di Matteo amefungwa mechi moja tu tangu amrithi Villas Boas huku akiwa aemcheza mechi 14.


WAINGEREZA NA MBWEMBWE ZAO KABLA YA EURO 2012. THREE LIONS



HII NDIO KEKI JUAN MATA ALIMNUNULIA DAVID LUIZ WAKATI YA BIRTHDAY YAKE JUZI



VIDEO: VAN DER SAR BADO WAMO



UKWELI NA UTHIBITISHO KWAMBA BARCELONA BILA MESSI HAKUNA KITU.

Katika mechi mbili za hivi karibuni za Barcelona, mchawi wa soka wa sasa ulimwenguni Lionel Messi hakufanikiwa kufnga goli - na Barcelona wakafungwa mfululizo na Chelsea na Real Madrid. Lakini hawezi kufanya mabo yote peke yake.

Kiukweli tuache ubishi pembeni Muaregentina huyu ndio roho ya Barcelona, na mfano mzuri ni huu katika katika mechi nne ambazo Barcelona wamefungwa msimu huu Messi hakufunga kabisa ndani ya mechi na pia katika mechi 21 ambazo Lionel hakufunga matokeo hajawahi kuwa mazuri kwa Catalans.

Angalia ukweli huu.



WHEN MESSI HAS FAILED TO SCORE IN 2011-12

RIVAL COMPETITION DATE RESULT
Real Sociedad La Liga Sep 10
2-2
AC Milan Champions League Sep 13
2-2
Valencia La Liga Sep 21
2-2
Sporting La Liga Oct 2
1-0
Viktoria Plzen Champions League Oct 19
2-0
Sevilla La Liga Oct 22
0-0
Granada La Liga Oct 25
1-0
Getafe La Liga Nov 26
0-1
Real Madrid La Liga Dec 10 3-1
Al Sadd Club World Cup Dec 15 4-0
Espanyol La Liga Jan 8 1-1
Osasuna Copa del Rey Jan 12 2-1
Real Madrid Copa del Rey Jan 18 2-1
Real Madrid Copa del Rey Jan 25 2-2
Villarreal La Liga Jan 28 0-0
Valencia Copa del Rey Feb 1 1-1
Valencia Copa del Rey Feb 8 2-0
Osasuna La Liga Feb 11 2-3
AC Milan Champions League April 3 0-0
Chelsea Champions League April 18 0-1
Real Madrid La Liga April 21 1-2


KIMENUKA YANGA: KIONGOZI WA KAMATI YA USAJILI SEIF AHMED AJIUZULU

Kufuatia mfululizo wa matokeo mabaya yaliyopelekea timu ya Yanga kupoteza ubingwa wake, hatimaye leo kiongozi na mwenyekiti wa kamati ya usajili wa Yanga - Seif Ahmed ametangaza kujiuzulu.

Seif ambaye amehusika na usajili wa wachezaji wengi wa Yanga msimu huu amesema ameona bora ajiuzulu ili kupisha kiongozi mwingine ambaye ataoangeza ufanisi na kuisadia Yanga iweze kurudisha makali yake na kuuchukua tena ubingwa wake wa ligi kuu msimu uajo.

Kwa taarifa zaidi endelea kutembelea mtandao huu.

ITS ALMOST DONE..... SIMBA YAKARIBIA BINGWA WA VODACOM PREMIER LEAGUE 2012


WEKUNDU wa Msimbazi, Simba SC jioni hii wamejihakikishia ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya kuifunga Moro United ya Morogoro maba 3-0 na mechi ya wapinzani wao katika mbio za ubingwa, Azam FC dhidi ya Mtibwa Sugar ikivunjika timu hizo zikiwa zimefungana 1-1, Uwanja wa Azam, Chamazi.
Mabao ya Simba SC yalifungwa na Patrick Mutesa Mafisango, Haruna Moshi Shaaban 'Boban' na Felix Mumba Sunzu Jr.
Simba sasa imetimiza pointi 59, ambazo kutokana na matokeo ya leo ya sare ya 1-1 kati ya azam na Mtibwa, haziwezi kufikiwa na timu yoyote. Lakini kujiweka salama, Simba itahitaji japo polnti moja katika mechi zake tatu zilizobaki.
Mchezo kati ya Azam na Mtibwa ulivunjika wakati beki Salum Swedi amekwishaifungia bao Mtibwa na Mrisho Khalfan Ngassa ameifungia Azam FC. Mtibwa waligomea mechi hiyo wakipinga Azam kupewa penalti. Sasa Kamati ya Ligi Kuu itakutana kesho na kutoa uamuzi, lakini kuna uwezekano mkubwa Mtibwa ikatozwa faini na wapinzani wao kupewa ushindi.



Nafasi
Timu MP W D L GF GA +/- Pts
1  Simba SC 25 18 5 2 42 12 30 59
2  Azam 23 15 5 3 34 11 23 50
3  Young Africans 24 15 4 5 38 21 17 49
4  Mtibwa Sugar 23 10 5 8 31 25 6 35
5  Coastal Union 24 10 2 12 24 29 -5 32
6  Kagera Sugar 24 7 10 7 25 25 0 31
7  JKT Ruvu 24 7 10 7 25 30 -5 31
8  Ruvu Shooting 24 7 9 8 20 19 1 30
9  JKT Oljoro 23 7 8 8 16 20 -4 29
10  Toto African 24 5 11 8 23 27 -4 26
11  African Lyon 24 5 8 11 20 29 -9 23
12  Villa Squad 24 6 5 13 26 43 -17 23
13  Moro United 25 3 10 12 27 44 -17 19
14  Polisi Dodoma 25 3 8 14 18 34 -16 17

MAGOLI 34 NA JINSI ALIVYOBADILISHA MSIMU WA ARSENAL: TATHIMINI YA MCHEZAJI BORA WA ENGLAND VAN PERSIE KUTOKA AUGUST 2011 - APRIL 2012

AUGUST
GAMES PLAYED(SUBSTITUTE)
GAMES WON/DRAWN/LOST
GOALS SCORED
AVERAGE GOAL.COM PLAYER RATING
4(0)
1/1/2
2
6.25
Van Persie, na Arsenal in general, walianza msimu taratibu. Baada ya sare tasa katika mechi ya ufunguzi., baadae mdachi huyo akafunga goli muhimu la kusawazisha dhidi ya Udinese katika mechi ya play off ya champions league kabla ya kufunga goli la pili katika mechi ya aibu kwa upande wao waliyofungwa 8-2 naManchester United.
SEPTEMBER



SEPTEMBER
GAMES PLAYED(SUBSTITUTE)
GAMES WON/DRAWN/LOST
GOALS SCORED
AVERAGE GOAL.COM PLAYER RATING
4(0)
1/1/2
2
6.25
Arsenal waliendelea kucheza ovyo mwezi wote wa septmber, ushindi mwembamba dhidi ya Swansea na droo ngumu dhidi ya Dortmund zikifuatiwa na kufungwa na Blackburn huku Van Persie akifanikiwa kufunga goli 1 katika mechi dhidi ya wajerumani. Mambo yalianza kwenda vizuri baada ya kufunga goli mbili zilizoisadia Arsenal kushinda 3-0 dhidi Bolton.

OCTOBER
GAMES PLAYED(SUBSTITUTE)
GAMES WON/DRAWN/LOST
GOALS SCORED
AVERAGE GOAL.COM PLAYER RATING
5(0)
4/0/1
7
7.50
Mwezi October Van Persie alifakuwa na urafiki mzuri na magoli ya wapinzani. Baada ya kufungwa na Tottenham, nahodha wa Arsenal alifunga mabao mawili ya ushindi ya Sunderland , akafunga mawili tena katik mechi dhidi ya Stoke kabla ya kufunga hat trick katika london derby dhidi ya Chelsea.
NOVEMBER
GAMES PLAYED(SUBSTITUTE)
GAMES WON/DRAWN/LOST
GOALS SCORED
AVERAGE GOAL.COM PLAYER RATING
4(1)
3/2/0
5
7.50
Hali ya hewa ikawa ya baridi ulipofika mwezi November lakini mdachi huyu akazidi kuwa wa moto. Baada ya kufunga goli katika ushindi wa 3-0 dhidi ya West brom @Emirates, Van Persie akafunga katika mechi ya tano mfululizo akitupia bao mbili za ushindi dhidi ya Norwich City na Dortmund huku Gunners wakianza kuirudisha form yao iliyokuwa imepotea.
DECEMBER
GAMES PLAYED(SUBSTITUTE)
GAMES WON/DRAWN/LOST
GOALS SCORED
AVERAGE GOAL.COM PLAYER RATING
6(0)
4/1/1
4
7.08
Magoliyakizidi kumwagika kwa Van Persie katika kipindi cha sikukuu, akifunga dhidi ya Wigan, kabla ya kutia kambani dhidi ya Everton na Aston Villa. Akakosa bao katika mechi dhidi ya Wolves, na sasa akawa anahitaji hat trick dhid ya QPR ili kuifikia rekodi ya Alan Shearer ya kufunga mabao mengi katikA KALENDA YA mwaka wa premier league, lakini akafunga goli moja.

JANUARY
GAMES PLAYED(SUBSTITUTE)
GAMES WON/DRAWN/LOST
GOALS SCORED
AVERAGE GOAL.COM PLAYER RATING
4(0)
1/0/3
4
6.75
Gunners walianza mwaka 2012 na vipigo vitatu mfululizo, Van Persie akifunga dhidi ya Swansea na Man United. Baada ya kumuangalia Henry akifunga katika mechi yake ya kwanza dhidi ya Leeds, Mdachi huyu alikwenda kufunga penati mbili katika mechi ya raundi ya nne dhidi ya Aston Villa.

FEBRUARY
GAMES PLAYED(SUBSTITUTE)
GAMES WON/DRAWN/LOST
GOALS SCORED
AVERAGE GOAL.COM PLAYER RATING
6(0)
3/1/2
4
6.75
Mwezi mbaya, walianza na sare ya 0-0 dhidi ya Bolton, kabla ya mambo kubadilika na kushinda 7-1 dhidi ya Blackburn huku Van Persie akifunga hat tick kabla hawajaenda San Siro na kufungwa magoli manne kwa nunge. Baadae wakaja wakatolewa katika FA Cup baada ya kufungwa 2-0 na Sunderland. Mechi iliyofuatiwa walianza kufungwa 2-0 na Spurs pale Emirates kabla ya Pesie kurudisha na kwenda hafl time wakiwa wamelingana. Kipindi cha pili Walcott akaibuka shujaa baada ya kufunga mengine na kuifanya timu yake iibuke na ushindi wa 5-2.


MARCH
GAMES PLAYED(SUBSTITUTE)
GAMES WON/DRAWN/LOST
GOALS SCORED
AVERAGE GOAL.COM PLAYER RATING
6(0)
5/0/1
4
6.75
Ushindi dhid ya Spur uliamsha cheche za ushindi za Arsenal. Van Persie akafunga goli muhimu dhdi ya Liverpool. Gunners wakakaribia kuushangaza ulimwengu baada ya kuifunga AC Milan 3-0 katika mchezo wa pili wa UCL huku Van Persie akifunga goli penati. Nahodha huyo pia alifunga goli la ushindi dhidi ya Newcastle ingawa mwezi huo uliisha kwa kipigo dhidi ya QPR.




APRIL

GAMES PLAYED(SUBSTITUTE)
GAMES WON/DRAWN/LOST
GOALS SCORED
AVERAGE GOAL.COM PLAYER RATING
4(0)
2/1/1
1
6.7
Form ya the Dutchman hivi karibuni imekuwa ya kawaida sana, akifunga goli moja mpaka sasa ndani ya mwezi huu wa nne katika dhidi ya Wolves.




JUMLA YA TATHIMINI YOTE YA MIEZI 10
SEASON'S TOTAL THUS FAR
GAMES PLAYED(SUBSTITUTE)
GAMES WON/DRAWN/LOST
GOALS SCORED
AVERAGE GOAL.COM PLAYER RATING
43(2)
26/7/12
34
6.94

RONALDINHO GAUCHO ! HUYU MTU ANA BALAA



Zinedine Zidane - Footballs Greatest document


No comments: