Tuesday, March 27, 2012

TIGER WOODS ARUDISHA MAKALI


Tiger Woods
NYOTA wa gofu, Tiger Woods ameibua matumaini ya kutwaa taji la tano la Masters baada ya kutwaa taji lake la kwanza la PGA Tour tangu Septemba mwaka 2009, Bay Hill.
Mchezaji huyo nambari moja zamani duniani alitwaa taji lake la kwanza mwaka huu, baada ya kumfunga mitupo mitano Graeme McDowell kwenye viwanja vya Arnold Palmer Invitational.
"Nina usongo na Masters," alisema mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 36, ambaye ametwaa mataji 14 makubwa.
Woods alikuwa ana miaka miwili ya kucheza bila kushinda taji lolote, kufuatia matatizo yake binafsi ya kifamilia kabla ya kutwaa taji la Chevron World Challenge, Desemba.

No comments: