Tuesday, March 27, 2012

ABIDAL KISU CHA INI LEO


Abidal na Dani Alves
BEKI wa Barcelona, Eric Abidal leo ndio anatarajiwa kufanyiaji upasua wa ini Hospital Clinic mjini Barcelona on. Taarifa zinasema amejitokeza rafiki yake wa tangu utotoni kumchangia damu kuelekea kwenye upasuaji huo.
Kulikuwa kuna wasiwasi kwamba Abidal asingecheza tena soka ya ushindani baada ya upasuaji kama huo mwaka jana, lakini Mfaransa huyo alipona na kurudi kazini akicheza soka safi katika ushindi wa 3-1 wa Barca dhidi ya Manchester United katika fainali ya Ligi ya Mabingwa kwenye Uwanja wa Wembley. Abidal pia hivi karibuni alisaini mkataba mpya na Barca.

No comments: