Golikipa bora wa michuano ya Amani Cup, Elmanus Mbunju wa timu ya Chikongola, akipokea zawadi kutoka kwa kamanda wa polisi mkoa wa Mtwara, ACP-Henry Mwaibambe. |
Na Juma
Mohamed, Mtwara.
TIMU ya kata
ya Chikongola mkoani hapa imeibuka mabingwa wa michuano ya Amani Cup baada ya
kuichapa Kata ya Chikongola kwa magoli 2-1 katika mchezo wa fainali uliofanyika
juzi katika uwanja wa Polisi na kuhudhuliwa na vijana wengi waliohamasika na
michuano hiyo.
Baada ya
kuibuka mabingwa katika michuano hiyo ambayo iliandaliwa na Kamanda wa Polisi
wa Mkoa wa Mtwara ACP-Henry Mwaibambe, timu ya Chikongola ilikabidhiwa zawadi
ya fedha tasilimu shilingi laki tatu (300,000), mpira pamoja na Kombe, huku
mshindi wa pili timu ya kata ya Chuno ikipata fedha tasilimu shilingi laki
mbili (200,000) na mshindi wa tatu kata ya Shangani ikiambulia shilingi laki
moja (100,000).
Mashabiki wa timu ya Chikongola wakiwa wamembeba juu Nahodha wao, Ally Bushiri, baada ya kukabidhiwa kombe la ushindi wa michuano ya Amani Cup |
Zawadi nyingine
ambazo zilitolewa na kamanda wa polisi ni kwa mlinda mlango bora ambaye ni Elmanus
Mbunju wa Chikongola aliyepata kitita cha shilingi elfu hamsini (50,000),
mlinzi bora ni Ally Bushiri wa Chikongola, mfungaji bora Hussein Abdallah
kutoka kata ya Shangani na mwamuzi bora Muksini Chibwana ambao wote
walizawadiwa shilingi elfu hamsini (50,000).
Akizungumzia
lengo la kuandaa michuano hiyo, kamanda Mwaibambe alisema ilikuwa ni maalumu
kwa ajili ya kujenga na kuendeleza ukaribu baina ya wananchi na jeshi la polisi
na kuwashukuru baada ya kufanikisha zoezi la uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na
Madiwani uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu kumalizika kwa amani mkoani hapa.
Heka heka katika lango la timu ya Chikongola. |
“Nimefurahi
mashindano yalikuwa na msisimko mkubwa sana, malengo ya mashindano yametimia
kwamba malengo yetu ilikuwa ni kuwa karibu sana na jeshi la polisi tushirikiane
katika kukomesha uhovu mbalimbali katika jamii yetu..uchaguzi uliopita ulikuwa
nzuri, japo kulikuwa na changamoto nyingi sana wapo wachache walipata madhara
na waliumia, lakini kwa ujumla wake uchaguzi ulikwenda kwa amani na utulivu..si
kwa nguvu ya polisi bali ni ushirikiano wenu wananchi na jeshi la polisi,
hatuna zawadi ya kuwapa zaidi yah ii burudani..” alisema.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, ACP-Henry Mwaibambe, akikabidhi zawadi kwa Nahodha wa timu ya Chikongola, Ally Bushiri, baada ya kuibuka mabingwa wa michuano ya Amani Cup. |
Aidha,
aliwaahidi wananchi kuendelea kuwapatia burudani za aina hiyo kwa malengo
yaleyale, ambapo ifikapo mwezi Machi 2016, ataandaa mashindano mengine ambayo
yatakuwa bora zaidi ya haya ambayo yamemalizika.
Michuano
hiyo ambayo ilianza wiki mbili zilizopita na kuchezwa kwa mtindo wa mtowano,
ilihusisha jumla ya timu 20, ambapo timu 18 zilitoka katika kata zote 18 za
Manispaa ya Mtwara huku timu mbili zikitoka katika kata za Halmashauri ya
Mtwara vijijini.
No comments:
Post a Comment