Mchezaji wa Simba, Awadh Juma akitoka kukimbizana na mashabiki wa Ndanda. |
Wachezaji wa Simba na kocha wao Dylan Kelly walipoanza kuzozana na mashabiki wa Ndanda ndani ya uwanja wa Nangwanda Sijaon |
Kocha wa Simba Dylan Kelly, akijaribu kuwaondoa wachezaji wake waliokuwa wakigombana na mashabiki wa Ndanda mara baada ya kumaliza mazoezi ya asubuhi. |
Hali ilivyokuwa nje ya uwanja wa Nangwanda Sijaona, katika vurugu za wachezaji wa Simba na mashabiki wa Ndanda |
Mwenyekiti wa mashabiki wa Ndanda, Mohamed Jimbu (Mwenye fulana la Blue) akiwa ndani ya gari la Polisi wakielekea kituoni. |
Askari wakiondoka na mashabiki wawili wa Ndanda waliohusika katika vurugu |
Na Juma
Mohamed, Mtwara.
WACHEZAJI wa
timu ya Simba wamelazimika kupigana na mashabiki wa timu ya Ndanda ya mkoani
hapa nje ya uwanja wa Nangwanda Sijaona na kurushiana mawe, kutokana na kukerwa
na vitendo vilivyofanywa na mashabiki hao vya kuwazuia kutumia lango kuu la
kuingilia na kutokea uwanjani, na baadala yake kuwataka watumie lango
wanalotaka wao.
Vurugu hizo
zilianzia ndani ya uwanja huo mara baada ya Simba kumaliza mazoezi yao ya
asubuhi ambapo walitaka kutoka uwanjani kwa kutumia lango kuu ambalo awali
wakati wanaingia mashabiki wa Ndanda walizuia lisifunguliwe kwa madai kuwa ni
mbovu na Simba kulazimika kutumia lango lingine dogo ambalo kwa kawaida
halitumiwi na timu wakati wa kuingia au kutoka uwanjani.
Golikipa wa Simba, Manyika Peter na kiungo, Abdi Banda, wakirejea kutoka katika harakati za kupambana na mashabiki wa Ndanda |
Wachezaji wa Simba wakiwakimbiza mashabiki wa Ndanda. |
Mashabiki wa
Ndanda walionekana kuwarushia maneno ya kuudhi na lugha za matusi wachezaji wa
Simba muda wote wakiwa mazoezini na hata baada ya kumaliza, jambo ambalo
liliwafanya wahamaki na kuamua kwenda kuwashambulia baadhi yao, huku mwalimu wa
Simba Dylan Kelly akihangaika kuwadhibiti wachezaji wake ambao leo wanaingia
uwanjani kukipiga na Ndanda Sc.
Wachezaji
hao walionekana kukimbizana na mashabiki nje ya uwanja huku baadhi ya mashabiki
wakirusha mawe ambayo hata hivyo hayakuweza kumpata au kumuathiri mtu yeyote
mpaka Simba walipoondoka eneo la tukio.
Akizungumzia
tukio hilo, mjumbe wa kamati ya utendaji ya Simba, Iddi Kajuna, alisema ni
kitendo ambacho sio cha kiungwana na hakikubaliki mahali popote katika michezo
na kwamba ameliomba Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuliangalia kwa
mapana suala hilo na ikibidi hatua za kinidhamu ziweze kuchukuliwa dhidi yao.
Mchezaji wa Simba, Mussa H. Mgosi, akiondolewa katika vurugu na Iddi Kajuna. |
“Cha hajabu
sasa wakati wachezaji wamemaliza mazoezi na wanajaribu kutoka sasa kupitia
mlango mwingine ambao wao walikuwa hataki wapiti mlango ule na walitaka wapiti mlango
ambao wameuandaa wao, ndipo walipoanza kuvamia wachezaji kwa kuwatusi, kuwapiga
lakini tukajaribu kuwasihi wachezaji wakapata hasira sana ambayo kwakweli
haikuweza kuvumilika lakini tulijitahidi sana kuwabana wachezaji tukiwa watu zaidi
ya 20 kuwarudisha ndani ya basi huku wao wakiendelea kurusha mawe, matofali..sasa
tukaona huu sio ustaarabu tukawaondoa na tukajaribu kwenda sasa kwenye chombo
cha dola na baadhi yao wawili tayari tumewatia mikononi..” alisema Kajuna.
Mjumbe wa Kamati ya utendaji ya Simba, Iddi Kajuna, akizungumzia kuzuka kwa vurugu baina ya wachezaji wao na mashabiki wa Ndanda. |
Alisema,
wapo baadhi ya mashabiki wa Ndanda ambao walionyesha ustaarabu kwa kujaribu
kuwaonya wenzao ambao walifikia hatua ya kumtolea lugha za matusi hata mzee
Hassan Dalali ambaye ameambatana na timu hiyo.
Kwa upande
wake, mwenyekiti wa mashabiki wa Ndanda, Mohamed Jimbu, akizungumza kwa ufupi
kabla ya kukamatwa na askari, alisema Simba walishikwa na woga usio na msingi
kutokana na vitisho ambavyo vilionyeshwa na mashabiki hao ambavyo havikuwa na
nia yoyote mbaya.
Meneja wa Timu ya Ndanda, Martin Mwesiga, akizungumzia vurugu za mashabiki wa Ndanda na wachezaji wa Simba. |
“Huo ni
uwoga wao Simba, kwasababu wamekuja asubuhi wamekuta mashabiki wapo hapa na wao
wenyewe wanataka kufanya mazoezi kwahiyo walivyoingia walikuta vitu vya
ajabuajabu ambavyo mashabiki wenyewe hivyo vitu vilikuwa ni vya kuwatisha tu Simba,
hao Simba wakawa wamekuja juu wanataka kuanzisha vurugu tokea asubuhi..kwahiyo
walivyokuwa wameingia, mashabiki wakawa wanawazomea wachezaji wao viongozi
wakapanda jukwaa kubwa kwenda kugombana na mashabiki..” alisema Jimbu kabla ya
kukimbia baada ya kuona askari.
Wachezaji wa Simba wakiwa mazoezini, kujiandaa na mchezo wao dhidi ya Ndanda Sc wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara. |
Kocha wa Simba, Dylan Kelly, akiwa katika mazoezi ya asubuhi na wachezaji wake, katika uwanja wa Nangwanda Sijaona |
Naye, katibu
wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mtwara (MTWAREFA) Charles George, alisema Mtwarefa
inalaani kitendo hicho kilichofanywa na mashabiki hao ambapo alikiri kuwa
walitumia muda mwingi kuwakashifu wachezaji na viongozi wao, na kwamba
watajaribu kukutana na viongozi wa Ndanda ili kuwaagiza wake na viongozi wa
mashabiki hao kuwasihi juu ya vitendo hivyo ambavyo vinaweza pia kuigharimu
timu yao.
Kaimu kamanda
wa polisi mkoa wa Mtwara, Mrakibu mwandamizi wa Polisi, George Salala, alikiri
kupokea taarifa za malalamiko kutoka kwa viongozi wa Simba wakilalamikia
vitendo hivyo vya kufanyiwa vurugu, na kusema kuwa wameshaanza kulifuatilia
tukio hilo ambalo sio la kiungwana.
Katibu wa Chama cha Soka Mkoa wa Mtwara (MTWAREFA), Charles George, akizungumzia tukio la vurugu za mashabiki wa Ndanda na wachezaji wa Simba. |
Aliwaomba
viongozi wa Ndanda kukaa na mashabiki wao kwa ajili ya kuwatuliza ili mchezo
huo unaofanyika leo uweze kuchezwa kwa amani na utulivu.
“Mpaka
sasaivi nimekwishawaagiza maofisa wangu na wakaguzi wanaanza kulifuatilia hili na
tutakapo baini wale waliohusika, kwa hakika tutachukuwa hatua kali..na kesho (Leo)
ulinzi utakuwa wakutosha tutatumia nguvu zote za kiusalama tulizonazo
kuhakikisha kwamba pale uwanjani hapatokei uvunjifu wa amani..” alisema.
No comments:
Post a Comment