_logo.png)
Na Juma
Mohamed.
WATUMIAJI wa
umeme mkoani hapa wameshauriwa kuzima vifaa vyao mara baada ya kukatika kwa
umeme ili kuhepuka kusababisha madhara ya kuunguliwa na vifaa hivyo na hata kupelekea
athari zaidi katika nyumba zao.
Akizungumza jana ofisini kwake, Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)
mkoa wa Mtwara, Mhandisi Azizi Salum, alisema wananchi wanatakiwa kuwa makini
na vifaa vyao na kuachana na dhana iliyopo kwa baadhi yao wakiamini kuwa
kuungua kwa vifaa kunatokana na umeme kurudi kwa kasi baada ya kukatika.
“Pale ambapo
umeme unakatika, basi kama kulikua kuna kifaa ambacho kilikua kinafanya kazi ni
vizuri kikazimwa, umeme utakaporudi basi vile vifaa vinaweza vikawashwa..matatizo
yanatokea kama pale kifaa kitakua kimeachwa ‘on’ labda kama ulikua unapiga pasi
ukajisahau ukaiacha ‘on’ umeme ukirudi pale kwavyovyote vile pasi ina ‘heat’ kwahiyo
kama kuna kitu chochote karibu ambacho kinauwezo wa kuungua kinaweza kuleta
madhara..” alisema.
Aidha,
alisema hali ya upatikanaji wa umeme katika mkoa wa Mtwara kwa sasa imetengamaa
baada ya kupatikana kwa vifaa vya mashine moja kati ya mbili ambazo zilipatwa
na hitilafu na kusababisha mgao wa umeme katika baadhi ya maeneo kwa siku
chache zilizopita.
Alisema, kutokana
na kituo cha kuzalisha huduma hiyo kilichopo mkoani hapa kuhudumia pia katika
mkoa wa Lindi, maeneo ambayo yaliathirika na mgao huo yalikuwa ni pamoja na
Mtwara mjini, Tandahimba, Newala, Lindi mjini, Nachingwea na Masasi.
Meneja huyo
alitoa wito kwa watumiaji wa umeme kuongeza juhudi katika ulipaji wa bili zao,
kwani kwa kufanya hivyo inasaidia kuongeza kipato katika shirika hilo na
kuwawezesha kuboresha huduma zao hasa za mitambo ambayo ikipatwa na hitirafu
inapelekea ukosefu wa umeme kwa wananchi.
No comments:
Post a Comment