Thursday, January 7, 2016

Madereva wa mabasi Mtwara wagoma kwa saa tatu.


Baadhi ya abiria wanaosafiri kutoka Mtwara kwenda jijini Dar es Salaam wakiwa katika kituo kikuu cha mabasi mkoani Mtwara hawaelewi hatima yao kutokana na mgomo wa madereva uliodumu kwa takribani saa tatu kutokana na madereva watatu kushikiliwa na jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani kwa kosa la kwenda mwendo kasi.


Baadhi ya abiria wanaosafiri kutoka Mtwara kwenda jijini Dar es Salaam wakiwa katika kituo kikuu cha mabasi mkoani Mtwara hawaelewi hatima yao kutokana na mgomo wa madereva uliodumu kwa takribani saa tatu kutokana na madereva watatu kushikiliwa na jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani kwa kosa la kwenda mwendo kasi

 Na Juma Mohamed.

ABIRIA wanaosafiri kwa mabasi ya kutoka Mtwara kwenda jijini Dar es Salaam wamelazimika kusubiri kwa muda wa saa tatu kutokana na madereva wa mabasi hayo kugoma kuondoka kushinikiza kuachiwa huru wenzao watatu wanaoshikiliwa na jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani kutokana na kwenda mwendo kasi.
Wakizungumza katika kituo kikuu cha mabasi mkoani hapa, baadhi ya abiria walisema hali hiyo imekwamisha mipango yao kwasababu wapo wanaosafiri kwa matatizo na wapo wanaosafiri kwa ajili ya kuwahi mambo mengine ya msingi kwa ajili ya shughuli za ujenzi wa taifa.
Muhidin Chinengo, ambaye ni msafiri anyeelekea mkoani Shinyanga, alisema juzi alikata tiketi katika basi la Machinga kwa ajili ya kusafiri jana mpaka Dar es Salaam ambako angeunganisha kwa usafiri wa Treni na kufika Shinyanga katika chuo cha Maopareta lakini amekutana na kikwazo hicho ambacho hakujua hatima yake.

Baadhi ya abiria wanaosafiri kutoka Mtwara kwenda jijini Dar es Salaam wakiwa katika kituo kikuu cha mabasi mkoani Mtwara hawaelewi hatima yao kutokana na mgomo wa madereva uliodumu kwa takribani saa tatu kutokana na madereva watatu kushikiliwa na jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani kwa kosa la kwenda mwendo kasi.

“Nikiwauliza walionikatia tiketi wanasema wana mgomo kutokana na madereva wao ambao wamekatwa kwasababu ya mwendo kasi..kila tukiwahoji ili tujue uwezekano wa kusafiri wao wenyewe hawatupi taarifa au hawatoi ushirikiano wowote, kwahiyo mimi nilikuwa nawaomba kama Machinga Transporter makao makuu ni Mtwara bosi mwenyewe yuko hapa na meneja wake yuko hapa na wanajua hadha hizi tunazopata sisi wananchi basi atusaidie..” alisema.
Naye Iddi Selemani, msafiri wa basi la Maning Nice, alisema anashangazwa na kitendo cha askari kuonekana kituoni hapo lakini bado hakuna muafaka wowote wa jambo hilo huku wao wakiendelea kusota na kutojua ni muda gani wataanza kusafiri.
Kwa upande wake, Dereva wa basi la Buti la Zungu, Abdul Mcharu, alisema hoja yao ya msingi ni kutaka kujua hatima ya madereva hao wa mabasi matatu ambao aliwataja majina kuwa ni Imma (Ibra Line), Athumani (No Raiz) na Rashid Machemba (Machinga) ambao walikamatwa kwa kosa la kwenda mwendo kasi.

Dereva wa basi la Buti la Zungu, Abdul Mcharu akizungumzia juu ya mgomo ambao ulidumu kwa takribani saa tatu kutokana na madereva watatu kushikiliwa na jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani kwa kosa la kwenda mwendo kasi.

“Kitu ambacho kinatutoa katika mawazo yetu ya kawaida sisi madereva na kutupeleka katika mawazo makubwa sana ni kwamba swala la Tochi kwanzia jana (Juzi) saa 9 mpaka sasaivi saa 2 kweli mtu yuko mahabusu alafu katika hali ya sintofahamu tulikwenda sisi pale ili kutaka suluhu inamaana maderva wa Mtwara ndio sisi..inamaana RTO wa Mtwara amepanga moja mbili tatu kwenye hili, litakalo mkuta ambalo tutagundua kwamba tushamweleza ni lakwake..” alisema Dereva huyo.
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Mtwara (RTO) Meloe Buzema, alisema madereva waliokamatwa suala lao linashughulikiwa na wanatarajiwa kufikishwa mahakamani ili wasomewe mashitaka yao.

Mkuu wa kitengo cha Usalama Barabarani mkoa wa Mtwara (RTO) Meloe Buzema, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mgomo wa madereva ulidumu kwa takribani saa tatu kutokana na madereva watatu kushikiliwa na jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani kwa kosa la kwenda mwendo kasi.

Alisema, jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani kwa sasa lipo katika oparesheni ya kudhibiti makosa ya mwendo kasi kwasababu ajali nyingi zinazotokea ni kutokana na mwendo kasi huku wahusika wanatozwa faini alafu bado wanaendelea kufanya makosa kwaiyo namna ya kuweza kukabiliana nao ni kuwafikisha mahakani.
“Ajali zote zinazotekea ni mwendo kasi, sasa hatuwezi kuacha tukawa tunateketeza maisha ya watu kwa kuwafumbia macho watu ambao tunaweza tukachua hatua stahiki..kwasababu kama faini tunaona wanapigwa faini na askari 30,000 barabarani lakini bado wanaendelea kufanya yaleyale ndio maana tumeona tufikie hatua ya kuwapeleka mahakamani..” alisema.
Hata hivyo mtandao huu ulishuhudia mabasi yakianza safari kituoni majira ya saa tatu asubuhi isipokuwa ni basi moja la Ibra Line ambalo halikupata dereva mwingine wakuliendesha.



No comments: