Miongoni mwa vyakula vilivyokumbwa na kadhia kutokana na mvua iliyoambatana na upepo mkali. |
![]() |
Paa la nyumba lililohezuliwa kutokana katika moja ya nyumba |
Na Juma Mohamed, Mtwara.
KAYA zipatazo 150 wilayani Tandahimba
mkoani hapa hazina makazi kufuatia upepo mkali ulioambatana na mvua iliyonyesha
kwa muda mfupi unaokadiriwa kutozidi dakika 3 katika Kijiji cha Chaume na
Sokoine, kuezua nyumba na nyingine kubomolewa vibaya huku baadhi ya wakazi
wakikosa chakula.
Kadhia hiyo iliyowakumba wakazi hao
ilitokea January mosi mwaka huu majira ya saa saba mchana, na kuzusha taharuki
kubwa ambayo wakazi wa vijiji hivyo
waliona sehemu kubwa ya kujiokoa ni kukimbilia misikitini ambako swala ya
ijumaa ilikuwa ikiendelea.
Wakizungumza baada ya tukio hilo badhi
ya waathirika walisema mvua hiyo licha ya kuezua paa na kubomoa nyumba pia
iliangusha miti ya mikorosho, na kuharibu vyakula vilivyoifadhiwa ndani na
kwamba waziomba kampuni, watu binafsi, mashirika mbalimbali kuwasaidia katika
kipindi hiki kigumu ambacho wanakabiliana nacho.
![]() |
Paa limehezuliwa |
“Hili janga lilitukuta jana majira ya
saa saba (January 1), tena nilikuwa na umati wa watu humu ndani tena ni kujihifadhi
kwa masuala ya ngoma, tukajikuta tumevamiwa na upepo mkali kabisa ambao
ulitushinda kila idara..ikawa kazi ya mungu ikapita na sasa hatuna chakula, na
tunashukuru serikali kupitia mhe. Diwani alichukua jukumu la kuwasiliana na
uongozi wa wilaya na ulifika lakini tunachoomba ni serikali, makampuni ya dini,
binafsi basi yaweze kutusaidia..” alisema Hassan Mzee.
Naye Salma Khatibu, aliiomba msaada
kwa majirani zake na viongozi wa serikali kuweza kumsaidia kutokana na kubokewa
na nyumba na kupoteza vyakula na vyombo ambapo hali hiyo inamuweka katika
mazingira magumu ya kimaisha yeye pamoja na familia yake.
Kwa upande wake, Mbunge wa jimbo la
Tandahimba, Katani Ahmad (CUF) alisema mara baada ya kupata taarifa za tukio
hilo aliwasiliana na mkuu wa wlilaya hiyo, Emmanuel Luhaula ambae kwa ahraka
aliwasiliana na kamati yake ya ulinzi na usalama ambayo iliwahi kufika eneo la
tukio kwa ajili ya kujua undani wake.
Alisema, baada ya mkuu huyo wa wilaya
kuwasiliana na kamati ya maafa ya wilaya, lilitolewa agizo la kutolewa chakula
kwa waathirika ambacho ni unga kg 25 na maharage kg 5 kwa kila kaya huku juhudi
zaidi zikifanyika za kuwasiliana na mkuu wa mkoa wa Mtwara Halima Dendego
ambaye baadae aliwasili kijijini huko.
![]() |
“Ninaamini na ninamatarajio makubwa
sana na ofisi ya waziri mkuu ambayo mfuko wa maafa uko chini yake itatupa
ushirikiano mkubwa sana na mimi kama Mbunge nitaendelea kusukuma jambo hili
kuhakikisha kwamba tahafifu kwa waathirika hawa inapatikana kwa kuweza
kuezekewa nyumba zao ili warudi katika hali ya kawaida..” alisema na kuongeza:
“Lakini wito wangu kwa wananchi wa
Chaume, wawe watulivu, wawe na subra, wapole kwa wakati huu ambao tunapitia
kwani hili ni janga ambalo mungu ndio amelipanga na wala sio binadamu, mungu
akileta jambo lake kwa sisi waisilamu lazima tushukuru kwanza maana pengine
kuna jambo amelinusuru kwasababu fikiria nyumba 150 lakini waliopata athari ni
watu saba ambao kati yao watu sita wamerudi kwao na mgonjwa mmoja tu ndio yuko
hospitali ya Newala akipata matibabu..” aliongeza Katani.
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya
Tandahimba, Namkulya Suleiman Namkulya, alisema pamoja na jitihada zilizoanza
kufanyika lakini halmashauri hiyo itahakikisha inashirikiana na wadau
mbalimbali wa maendeleo ili kuweza kufanikisha marekebisho katika shule
zilizoatihirika na ofisi za serikali.
“Tunakusudia kuona mambo ya msingi
kama vile shule pamoja na ofisi za serikali, hela ikitafutwa kwa haraka ili kuona
namna ya kuweza kuhakikisha wanafunzi mpaka kufikia Januari 11 wanarudi shuleni
na hizi ofisi za serikali angalau baada ya wiki moja au bili ziendelee kufanya
shughuli zake kama kawaida.” Alisema.
Aliongeza kuwa katika kuonyesha
ushirikiano katika jambo hilo, Benki ya NMB tawi la Tandahimba wameahidi kutoa
msaada wa bati 120 huku halmashauri ikiendelea kutafuta wadau wengine ili
kupata msaada zaidi pamoja na kuunganisha nguvu ya halmashauri hiyo kupitia
pato lake la ndani.
No comments:
Post a Comment