Na Juma Mohamed.
WANANCHI wa
kata ya Shangani, manispaa ya Mtwara Mikindani, waliandaa hafla ya kumpongeza Diwani wao mteule kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Ahmad Mbarale, baada ya kushinda katika uchaguzi mkuu uliopita.
Wananchi hao wamemtaka diwani huyo kushughulikia na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili
ikiwa ni pamoja na changamoto zinazowakabili akina mama katika hospitali ya
rufaa ya Ligula wakati wa kujifungua.
Katika hafla hiyo, baadhi ya kina mama wameelezea kutoridhishwa
kwao na huduma za uzazi zinazotelewa katika hospitali hiyo.
Fatuma
Namanoro, alisema wamemchgua diwani huyo ili awe kimbilio la wanawake kutokana
na kukabiliwa na changamoto nyingi hasa upande wa afya, ambapo alisema kumekuwa
na lugha zisizo nzuri kwa wahudumu wakati wanapokwenda kujifungua hospitalini
hapo.
Alisema,
awali kupitia sera za Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho ndicho kilikuwa
kinaongoza kata hiyo, waliambiwa kuwa huduma za uzazi kwa kina mama zitakuwa
zinapatikana bure lakini imekuwa tofauti.
“Sasaivi
wanawake tunazaa kule hospitali tunaambiwa tulete kilakitu ni juu yetu, sasaivi
wale ambao wanatuhudumia inakuwa ni maneno matupu, wanatupwa nje, manesi
wanakuwa ni wakali wakati sivyo inavyotakiwa, nesi anatakiwa awe mpole kutokana
na kazi yake..wanawake tunateseka, kwahiyo ndio maana sasaivi tumeona tufanye
haya mabadiliko katika uchaguzi ili tuwapate watu wengine, na mungu ametujaalia
tumepata UKAWA na tumepata ‘jembe’..” alisema.
Alisema,
anaimani kuwa diwani huyo atakuwa na msaada mkubwa kwa wananchi hasa wanawake,
na atakuwa ni mtu wa kusikiliza na kutatua kero sio tu kwa wanawake wa Chadema,
bali ni kwa wanawake wote.
“Diwani
tuliyemchagua Ahmad Mbarale, tunahitaji atusaidie kama ‘wamama’hasa katika
kituo cha afya cha hospitali ya Ligula, tunapokuwa tunajifungua huduma ni za
shida, tunahitaji atutetee kama wanawake..na kwenye vikundi mbalimbali kwa
ahadi alizoziaidi tunahitaji azitekeleze kama alivyoahidi katika manispaa
akazitekeleze hasa wanawake asituangushe kwa sera zote alizozitoa..” alisema Monica
James, mkazi wa mtaa wa Ligula.
Akitolea ufafanuzi
wa namna ya kutatua kero za afya kwa kina mama wakati wa kujifungua, diwani
huyo alisema wataboresha Zahanati zilizopo katika kata hiyo ambazo ni Zahanati
ya Shangani na Zahanati ya Polisi, ambapo alisema mkakati uliopo ni kuziongezea
uwezo na kuhakikisha kunakuwa na vifaa tiba ambavyo vitawawezesha kina mama
kujifungulia pasipo kuwa na matatizo.
“Kumekuwa na
malalamiko makubwa sana ya huduma za kina mama katika hospitali ya Ligula
ambayo ni hospitali ya rufaa, ile ni hospitali ya mkoa na ya wilaya pia, japo
haipo kwenye kata yangu lakini inagusa kata zote, kitu cha kwanza tukiingia
katika baraza la halmashauri tutajaribu kutembelea pale ili kuweza kugundua wenyewe
kwa macho yetu ili iwe rahisi kutatua kero hizo..´alisema.
Alisema,
moja ya jitihada atakazozifanya ni kutafuta wafadhili ambao anaamini kupitia
wao kero hizo zitapungua kwa kiasi kikubwa kama sio kwisha kabisa, pamoja na kuishinikiza
serikali iweze kuandaa bajeti ya kutosha kwa ajili ya kutatua kero hizo ambazo
zinalalamikiwa katika maeneo mengi ya huduma za afya.
Kwa upande
wake, mbunge mteule wa viti maalumu kupitia Chadema, Tunza Issa Malapo, alisema
atashirikiana ipasavyo na mbunge wa jimbo hilo kupitia Chama cha Wananchi
(CUF), Maftaha Nachuma, kuhakikisha wanatetea masilahi ya wananchi wa Mtwara
hasa akina mama juu ya kero wanazozipata wakati wa kujifungua.
“Kina mama
walikua wanalala chini pale Ligula hospitali wakati wanasubiri watu wajifungue,
sisimizi wakwetu, mvua yakwetu, jua lakwetu ‘Ngwangwalati’ wakwetu..tunasema
imetosha, na nilikuwa nasema katika mikutano yangu, hawa madiwani na sisi
wabunge kama hatutekelezi haya 2020 ‘mtupi chini’..” alisema.
No comments:
Post a Comment