Monday, September 7, 2015

Ray: hata wakisema Lowassa sijui fisadi, tunamtaka huyo huyo fisadi..hatumtaki Magufuli kwasababu CCM tumeshaichoka


Msanii wa filamu, Vicent Kigosi (Ray), akizungumza na waandishi wa habari juu ya harakati zao wanazozifanya za kumnadi mgombea Urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendele (CHADEMA) chini ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), Mhe. Edward Lowassa, na mgombea mwenza, Juma Duni Haji.

Msanii wa Filamu, Shamsa Ford.





Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Ally Timbulo (Timbulo)


Na Juma Mohamed

 Baadhi ya wasanii wa filamu na muziki hapa nchini wamesema wamechoshwa na utawala wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao wanaamini unachangia kurudisha nyuma maendeleo ya sanaa, na kuamua kuunga mkono upinzani.
Akizungumza mkoani Mtwara leo, muigizaji maarufu wa filamu, Vicent Kigosi (Ray), amesema nchi ya Tanzania ina kila aina ya utajiri lakini hauwanufaishi wananchi wake huku akiwashangaa wasanii wanaounga mkono CCM wakati wanajua hakina faida kwao.

 "Tumekuwa tukipewa ahadi nyingi ambazo hazina msingi, na tunashangaa kuna baadhi ya wasanii wanajua shida za wasanii na shida za watanzania wote ambao ni masikini wa kutupwa ambapo nchi hii ina kila aina ya utajiri..kwahiyo nimekuja Mtwara kuwaambia kwanza Mtwara mumepigwa kwenye gesi, kwahiyo watu wa Mtwara badilikeni na mchagueni Lowassa, huu ndio wakati wa madiliko sasa nchi yetu hii.." alisema Ray.

Na kuongeza "Chama Cha Mapinduzi kimekaa madarakani miaka zaidi ya 50 na hawajafanya mabadiliko..sasaivi tunataka mabadiliko, na hata wakisema Lowassa sijui fisadi, tunamtaka huyo huyo fisadi..hatumtaki Magufuli kwasababu CCM tumeshaichoka kukaa katika nchi hii na tunahitaji mabadiliko.." aliongeza.
 
Naye, msanii na muandaaji wa muziki wa kizazi kipya, Rahim Ramadhan (Bob Jounior), amesema lengo la kutembelea mkoani humo ni kuwahamasisha wananchi kuunga mkono vyama vinavyouna Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) na kutembelea makundi maalumu ikiwa ni pamoja na watoto yatima.

Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Fred Marick (Mkoloni)

 
Wasanii hao zaidi ya 30 waliwasili mkoani humo jana na kutumbuiza katika viwanja vya Mashujaa, ikiwa ni harakati za kumnadi mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) chini ya UKAWA, Mhe. Edward Lowassa na mgombea ubunge wa Mtwara mjini kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Maftaha Nachuma.

No comments: