Tuesday, September 8, 2015

Mwanafunzi kinara wa kufaulu aambulia '0' mtihani wa mwisho..

Mariam Malak

Maelfu ya wazazi na wanafunzi wamejitokeza kumuunga mkono mwanafunzi mmoja shupavu Mariam Malak raia wa nchini Misri, aliyepata sufuri katika mtihani wake wote wa mwisho.
Jambo la kushangaza ni kwamba, mwanafunzi huyo amekuwa mfano wa kuigwa nchini humo kutokana na alama za juu alizopata katika mitihani ya awali, alikuwa na matarajio ya kuzoa alama ya juu zaidi yaani A itakayomwezesha kujiunga na chuo cha mafunzo ya daktari lakini.
Katika mtihani wake wa mwisho, Malak alipewa alama za chini zaidi, ikimaanisha kuwa hakuandika hata herufi moja aliyojibu kikamilifu.

Mariam Malak

Kutokana na hali hiyo, mwanafunzi huyo anashuku kuwa kulitokea kosa kubwa kwani yeye alivyofanya mtihani huo hadhani kama angeufeli.
''Kwa kweli sikuamini macho yangu eti nimefeli mtihani wa mwisho'' alinukuliwa Malak na Shirika la Utangazaji la Nchini Uingereza (BBC).
Aidha, baada ya kutafuta jina lake bila ya mafanikio katika orodha ya watahiniwa waliopasi mtihani wao wa mwisho, alipoteza fahamu papo hapo.
Malak alikuwa hajaufeli mtihani mmoja bali alikuwa amezoa sufuri katika masomo yote saba.
Yaani alikuwa ameambulia sufuri juu ya mia 0% katika masomo yote saba.
''Hii sio kweli''
Familia yake inadai kuwa huwenda malaka ameangushwa mtihani wake wa mwisho maksudi tu kwa sababu ya hila, na kwamba huenda ikawa ni njama ya kufifisha ndoto yake ya kuwa daktari.
 Awali ilidhaniwa kuwa alichukiwa kwa sababu yeye ni wa kutoka kwenye tabaka la Wamisri wachache ambao ni wakristo wa kicoptic lakini dhana hio ilikataliwa.
Wizara ya Elimu imelazimika kumpa mtihani wa kubaini iwapo hati iliyowakilishwa kwa jina lake ni yake haswa ama ni ghushi, hata hivyo ikatoa uamuzi kuwa ilikuwa yake haswa.
Hata hivyo maelfu ya watu waliotazama nakala za hati aliyoandika kwenye runinga walisema hazifanani kabisa na zile zilizopewa jina lake.
Kufuatia tofauti hiyo, ukurasa ulianzishwa kwa nia ya kuishinikiza wizara ya elimu kuingilia kati kutanzua kitendawaili hicho.
Ukurasa huo unawafuasi takriban 30,000 kufikia sasa.
Tayari watu kadha wamejitokeza kugharamia malipo yake yote ya chuo kikuu.
Ndugu yake Mina anasema kuwa wanashuku majibu yake yalipewa mtu mwengine.


SOURCE: BBC

No comments: