
Na Juma
Mohamed, Mtwara.
MBUNGE wa
Sengerema Mhe. Willium Ngeleja amewataka makada wenzie wa Chama Cha Mapinduzi
(CCM) na Watanzania kwa ujumla, wampime kwa mambo 15 likiwemo la ujenzi wa
bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam.
Akizungumza wilayani Masasi alikokwenda kuomba wadhamini na kufanikiwa kuwapata 65,
Ngeleja alisema mradi huo ambao unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka huu
na kusaidia taifa kuokoa kiasi cha zaidi ya dola za kimarekani trilioni 1.6,
ulibuniwa kipindi ambacho yeye alikuwa waziri wa nishati na madini.
Alisema
jambo lingine ambalo Watanzania wanapaswa kumpima nalo ni kudhibiti umeme wa
mgao, ambapo kipindi ambacho alikabidhiwa wizara hiyo mwaka 2008 kulikuwa na
matukio ya mgao wa umeme kwasababu ya miundombinu mibovu katika shirika la
Umeme Tanzania (TANESCO).
“Mimi
niliukuta mgao katikati kabisa, lakini baadae Novemba 2011 mimi ndio
niliofanikiwa kudhibiti mgao wa umeme Tanzania..kwahiyo watanzania wenzangu
kupitia CCM nawaomba wanipime kwa kutumia hicho kigezo.” Alisema.
Aliongeza
kuwa, miradi mingi ya umeme vijijini inayotekelezwa sasaivi ilibuniwa katika
kipindi ambacho alikuwa akiiongoza wizara ya nishati na madini ambapo
ilipitishwa katika bajeti za mwaka 2008 mpaka ya 2012 na yeye ndio aliwasilisha
bungeni bajeti hizo.
“Kumbukumbu
zinaonyesha kwamba mimi nikiwa waziri wa nishati na madini, wizara hiyo na
taasisi zake, kwamujibu wa mkaguzi na mdhibti mkuu wa hesabu za serikali (CAG),
zilikuwa zinafanya vizuri na hatimae tulikuwa tunapata hati safi..maana yake
tuliisimamia vizuri wizara na taasisi zake..” aliongeza.
Aliendelea
kusisitiza vipaumbele vyake muhimu ambavyo ataanza navyo iwapo atafanikiwa
kuingia ikulu kuwa ni kuimarisha uchumi, ambapo aliweka msisitizo katika sekta
ya kilimo, utawala bora alitaja kuwa ni kipaumbele cha pili hasa katika
jitihada za kupiga vita rushwa, ufisadi na mmomonyoko wa maadili.
Vingine ni
kuimarisha huduma za kijamii zikiwemo za maji, elimu na afya ambavyo vitatokana
na kuimarika kwa uchumi huku uimarishaji wa miundombinu kikiwa ni kipaumbele
chake cha nne.
…………………..mwisho…………………………………….
No comments:
Post a Comment