Na Juma Mohamed, Mtwara.
CHAMA
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema rasilimali ya gesi
ilioko mkoani hapa inakwenda kuudidimiza zaidi mkoa huo katika lindi la
umasikini kutokana na serikali kutokuwa na taarifa sahihi juu ya mapato
na matumizi yatakayotokana na rasilimali hiyo.
Akizungumza
wiki iliopita mkoani hapa katika mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja
wa Nkanaredi, naibu katibu mkuu wa chama hicho Visiwani Zanzibar, Salum
Mwalimu, alisema sababu nyingine ni kutokana na serikali ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM) kuingia mikataba ya muda mrefu na wawekezaji.
“Hatuna
kauli sio tu Wanamtwara, Watanzania hatuna kauli..na tutapiga kelele,
tutabisha, tutatukana, tutaandamana, tutagoma mwisho wa siku mzungu
anakuja na mkataba..mkishindwa kuzuiliwa na ‘field
force’ wataleta askari wao wawazuie kwasababu wana mkataba.” Alisema.
Alisema
serikali ya CCM ikotayari kurudi madarakani kwa gharama yoyote
kwasababu ya kutaka kuendelea kunufaika na mikata walioingia na
wawekezaji, ambapo alionya wananchi wanaodhani kuwa kuwarudisha
madarakani viongozi wa CCM kutawasaidia juu ya kunufaika na rasilimali
hiyo.
“Hakuna gesi hapa ya kuendelea kupatikana miaka mitano
ijayo..lakini kitu tunachoweza kufanya Watanzania ni kudhibiti mikataba
hii kabla ya gesi haijaanza kutoka kwa wingi, na njia pekee ya kudhibiti
ni kuikataa CCM mwezi Oktoba, tupeni UKAWA (Umoja wa Katiba ya
Wananchi) tukaizime mikataba ya kiovu..” aliongeza Mwalimu.
Awali
akizungumza katika ukumbi wa chuo kikuu huria wakati wa kuwatunuku
vyeti wanafunzi 34 wa chuo kikuu kishiriki cha SAUT tawi la Mtwara,
ambao ni wanachama wa Taasisi ya Wanafunzi wanachama wa Chadema wa Vyuo
Vikuu (CHASO), Mwalimu alisema, chama hicho
sasa kinatumia mtindo wa kocha wa Chealsea Josee Mourinho wa
kuwashambulia wapinzani wao CCM.
“Walizoea kutuonea onea hawa
kwasababu tulikuwa tunatumia ‘formation ya 4,4,2 kwamba viongozi wa
chama ndio 4 yakwanza, 4 ya katikati ndio ya wabunge alafu mbele kule
yuko sijui dkt Silaa na mwenyekiti Mbowe, tumebadilisha sasaivi..sasaivi
tunatumia ‘Mourinho style’, tumetoa washambuliaji tumejaza viungo,
wakiangalia namba sita wanamuona Prof. Lipumba, pale katikati wanamuona
Mbatia, ukigeuka huku unamuona Mnyika, ukisogea mbele unamuona
Mwalimu..yani tunawapiga ‘Mourinho style’ ndiomana wameacha kufurukuta
wako kimya..” alisema.
Kwa upande wake, katibu wa balaza la
vijana la chama hicho (BAVICHA) Edward Simbei, alisema CCM
wanachokifanya kwa sasa hata hawajielewi na kusema kuwa ni sawa na
kuruka sarakasi wakati wamevaa taulo.
“ Hakiamungu tutawipiga
katafunua hawajawahi kuona..tumejipanga mwaka huu kuigawanya nchi
hii katika vipande vinne, kutakuwa na kikosi cha anga, kikosi cha
miguu, kutakuwa na kikosi cha kamati ya ushindi..” alisema Simbei.
………………….mwisho…………………………………..
No comments:
Post a Comment