Na Juma Mohamed, Mtwara.
VYAMA vya ushirika vya mikoa ya Lindi na Mtwara vimetakiwa kuwahamasisha wanachama wao juu ya umuhimu wa kununua hisa katika jengo la Ushirika, lililopo mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam, ili waweze kunufaika na rasilimali hiyo.
Akizungumza katika
semina ya uhamasishaji wa ununuzi wa hisa za jengo hilo, ilioandaliwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania (TFC) na kufanyika katika ukumbi wa VETA mjini Mtwara, Mrajisi Msaidizi wa vyama vya Ushirika mkoa wa Mtwara, John
Henjewele alisema, lengo kuu la semina hiyo ni kuwajengea uwezo viongozi wa
vyama vya ushirika vya mikoa ya Lindi na Mtwara kwenda kusambaza elimu watakayoipata,
kwenye vyama vyote ili waweze kununua hisa kwa wingi katika dhana halisi ya
uwekezaji wa pamoja.
Naye, katibu
mtendaji wa TFC, Willigis Mbogoro, alisema mfumo wa sasa wa uwekezaji katika
ushirika haumnufaishi mwanachama wala vyama vyenyewe isipokuwa unanufaisha
taasisi na watu wa nje kwasababu vyama vya ushirika ndivyo vyenye uwezo wa
kukopa na hata kununua pembejeo za kilimo, na dio sababu sirikisho hilo
likaamua kuja na mfumo wa dhana ya uwekezaji wa pamoja ili mwanachama aweze
kunufaika.
“Januari 14
mwaka huu, wanaushirika walikutana kule Dodoma wakaanzisha taasisi ya uwekezaji
wa pamoja ya ushirika, na kwakuanzia tumeanza na lile jengo la ushirika
(Ushirika Towers Co-operative Joint Enterprise), ni taasisi ambayo tayari
imekwishaanzishwa kutokana na huo mkutano.” Alisema Mbogoro.
Katibu wa
chama cha ushirika cha Muungano, mkoani hapa, Abdulrahman Abdul, alisema kama
kweli shirikisho hilo likitekeleza mambo yote waliyoahidi ikiwa ni pamoja na kunzisha
benki ya pamoja, kununua hisa kutoka katika jengo la ushirika na kufufua
kiwanda cha kuchapisha vitabu, itasaidia kuboresha na kuongeza kipato kwa
wanaushirika ambao hali zao ni duni kwa sasa kwa kukosa nguvu ya pamoja.
……………………….mwisho……………………………………………….




No comments:
Post a Comment