![]() |
| Wanakikundi cha ngoma ya asili wakitumbuiza |
![]() |
| Danford Peter, akipokea zawadi ya simu kutoka TTCL |
![]() |
| Danford Peter, akipokea zawadi ya simu kutoka TTCL |
![]() |
| Mnara wa mawasiliano wa TTCL uliozinduliwa |
![]() |
| Danford Peter, mwenye koti jeupe akizindua mnara wa mawasiliano wa TTCL |
![]() |
| Danford Peter, akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa TTCL |
![]() |
| Mnara wa TTCL uliozinduliwa juzi, Lupaso, wilayani Masasi. |
Na Juma
Mohamed, Masasi.
Wananchi wametakiwa
kuwa na matumizi mazuri ya simu na mitandao kwa ujumla na kuepuka kuitumia
kinyume na taratibu ambapo baadhi ya watu hutumia kwa kutoa lugha za matusi,
picha zisizo na maadili ya Kitanzania na ujumbe unaoashiria uchochezi.
Wito huo ulitolewa
juzi na Katibu Tawala wa wilaya ya Masasi, Danford Peter, wakati wa hafla ya
uzinduzi wa mnara wa mawasiliano wa kampuni ya simu Tanzania (TTCL), katika
kata ya Lupaso wilayani Masasi.
Alisema
baadhi yawatu wamekuwa wakikiuka taratibu za matumizi ya mitandao kwa kurusha
picha zisizoendana na maadili ya nchi yetu na kwamba uwepo wa sheria ya
mitandao itasaidia kuwabana watu wa aina hiyo.
Aidha, Peter
aliwataka wakulima kutumia simu na mitandao mingine kwa kutafuta masoko ya
mazao wanayoyapata kutokana na kilimo ndani na nje ya maeneo yao wanayoishi kwa
ajili ya kukuza kipato.
Alisema
mitandao ni njia mojawapo ya kutangaza kiasi cha mazao yaliyopatikana hasa
mazao ya ufuta, alizeti, choroko na korosho ambalo ndio zao kuu la biashara kwa
mkoa wa Mtwara, na kwa kufanya hivyo wanunuzi watapa kufahamu wastani wa
uzalishaji wa mazao katika maeneo husika.
“Tunafahamu
kwamba korosho ndio zao pekee linalowapatia wananchi wetu kipato..sasa mitandao
hii ni njia mojawapo ya kutangaza kwamba tunakorosho kiasi gani sisi tuliopo
hapa Lupaso, tuna ufuta kiasi gani tuliozalisha, tuna alizeti kiasi gani
tuchozalisha ambacho tunahitaji soko..sasa njia pekee ya kuwasiliana na
kutangaza hivyo vitu ni kupitia mitandao.” Alisema.
Kwa upande
wake, Meneja wa TTCL mkoa wa Lindi ambae alimwakilisha mkurugenzi wa kanda ya
Zanzibar na kusini, Nicodemus E. Mngulu, alisema kupitia mfuko wa kusimamia
utoaji wa huduma ya mawasiliano kwa wote nchini (UCSAF), kampuni hiyo ilipewa
jukumu la kufikisha huduma za mawasiliano katika kata 20 katika awamu ya kwanza
ya utekelezaji wa mradi wa mawasiliano vijijini.
“Katika kata
hizo za mwanzo, Lupaso na Lipumbulu ni mojawapo ya kata zilizonufaika na mradi
huo. Hii ni sehemu ya juhudi za serikali kuhakikisha upatikanaji wa mawasiliano
kwa urahisi zaidi na pia kuchangia ukuaji wa maendeleo katika maeneo ya
vijijini.” Alisema Mngulu.
Mnara huo
uliozinduliwa unakuwa ni mnara wa tano wa kampuni hiyo kwa mkoa wa Mtwara, na
kwamba unatoa huduma katika vijiji vitatu vya Lupaso, Mchoti na Lipumbulu
vyenye wakazi zaidi ya 2,000, kwa mujibu wa sense ya watu na makazi ya mwaka
2012.
……………………..mwisho………………………………………………………..








No comments:
Post a Comment