Friday, January 16, 2015

KUZIONA NDANDA NA SIMBA NI BUKU 3

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhwqJDeiyXYJojatgG8zifSIBDDb9yqnd9Ukvc30AgJ09LAtx1qOcObhcBxMQseb8fKazL7hwgfnA7ctmC7PW2JVLN6G1aiYW3Vx8PCTwWXQoN78ftSyXa6QR5bDcCqSCmXM9bmvNYXTOk/s1600/IMG-20140913-WA0029.jpg
Ndanda Fc


http://3.bp.blogspot.com/-X-bQzOHM7W0/VAu0Do-5baI/AAAAAAAAoNA/OjDlFBnIY4I/s640/11111.JPG
Simba Sc

 Na Juma Mohamed

Maandalizi ya mechi ya Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara kati ya Ndanda Fc dhidi ya Simba inayotarajiwa kufanyika hapo kesho katika uwanja wa Nangwanda Sijaona hapa mkoani Mtwara, yanakwenda vizuri, huku mechi kamishna na waamuzi wakitarijiwa kuwasili leo tayari kwa mchezo huo ambao unatarajiwa kuwa wa upinzani wa hali ya juu, kutokana na timu zote kuwa katika nafasi za chini katika msimamo wa Ligi hiyo.
Wenyeji Ndanda Fc wao wanashika nafasi ya 11 katika msimamo wakiwa na alama 10, huku wapinzani wao wekundu wa Msimbazi wakiwa katika nafasi ya 12 na alama zao 9.
Akizungumza na waandishi wa habari, mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoani Mtwara, Othmani Kambi, amesema timu zote mbili tayari zipo hapa mkoani Mtwara na hakuna taarifa zozote za matatizo kuhusiana na mchezo huo.
Kuhusu tiketi ni kwamba zinatarajiwa kuanza kuuzwa mapema hapo kesho, ambapo mashabiki wataingia uwanjani kwa shilingi elfu 5 na shilingi elfu 3.
Aidha Kambi amezungumzia utaratibu wa kuingia magari uwanjani, kuwa hakutakuwa na gari lolote litakalo ruhusiwa kuegeshwa ndani ya uwanja, na wametenga sehemu za kuegesha magari nje ya uwanja ambapo magari yatakayoruhusiwa kuingia ni ya askari polisi, mgeni rasmi na gari la zima moto

Ikumbukwe kwamba timu hizi zilikutana katika mchezo wa kirafiki hapa mkoani Mtwara mwaka jana katika tamasha la Ndanda day, na mchezo kumalizika kwa suluhu.
Simba wao kabla ya mchezo huu walikuwa wakishiriki michuano ya kombe la Mapinduzi kule Zanzibar, ambapo wameibuka mabingwa baada ya kuwafunga Mtibwa Sugar kwa mikwaju ya Penalt 4-3, huku Ndanda wakitoka sare ya goli 1-1 na Polisi Moro, katika mchezo wa Ligi kuu uliofanyika hapa Mkoani Mtwara wiki moja iliyopita.

No comments: