Saturday, June 23, 2012

SIMBA YALITANDIKA TOTO LA YANGA


SIMBA 2 TOTO AFRICAN 0

SIMBA leo imeichapa Toto African ya Mwanza kwa mabao 2-0 katika pambano kali la kirafiki lililofanyika katika Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza.
Hiyo ilikuwa ni mechi ya kwanza ya kirafiki kwa Simba katika ziara yake ya mikoa ya kanda ya ziwa iliyoanza jana (Juni 22) na kumalizika keshokutwa.
Wekundu wa Msimbazi walianza pambano hilo kwa kasi na iliwachukua dakika 17 tu kuandika bao la kwanza lililowekwa kimiani na Uhuru Selemani aliyemalizia vizuri pasi ya Abdallah Juma.
Hadi kipindi cha kwanza kinamalizika, Simba ilikuwa inaongoza kwa bao hilo moja.
Katika kipindi cha pili, Simba ilifanya mabadiliko kwa kumtoa Abdallah Seseme na Hassan Khatib na nafasi zao kuchukuliwa na William Lucian (Gallas) na Jonas Mkude.
Mabadiliko hayo yalizaa matunda kwani katika dakika ya 48, Simba iliandika bao la pili lililofungwa na Salim Kinje, mchezaji mpya wa Simba aliyesajiliwa kutoka AFC Leopards ya Kenya.
Kinje alifunga bao hilo akiunganisha moja kwa moja kutoka nje ya 18 pasi ya kichwa kutoka kwa Uhuru.
Katika pambano la jana, wachezaji waliosajiliwa msimu huu walikuwa ni Waziri Hamad, Paulo Ngalema, Kiggi Makassy, Kinje na Abdallah Juma.
Wachezaji wawili wa kikosi cha vijana Simba maarufu kwa jina la U-20, Haruna Chanonga na Lucian pia walicheza mechi yao ya kwanza kwa kikosi cha wakubwa leo hii.
Juni 24 Simba itaingia kwenye uwanja wa Kambarage Shinyanga kupambana na mabingwa wa soka wa Uganda, Express FC.
SIMBA; Waziri, Hassan (Gallas), Ngalema (Omar Waziri), Obadia Mungusa, Haruna Shamte, Amri Kiemba (Edward Christopher), Chanonga, Seseme (Kiggi), Abdallah (Ramadhani Salum), Kinje na Uhuru.

 

MIYEYUSHO ALIVYOMTWANGA MMALAWI...


Bondia Francis Miyeyusho akimshambulia bondia kutoka Malawi John Masamba wakati wa mpambano wao uliofanyika Dar es salaam jana Miyayusho alishinda kwa K.O Raundi ya 5.picha na www,superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia John Masamba kutoka Malawi akioneshana ufundi wa kutupa masumbwi na Francis Miyeyusho wakati wa mpambano wao uliofanyika Dar es salaam jana. Picha na www.superdboxingcoach,blogspot.com

Bondia John Masamba kutoka Malawi akioneshana ufundi wa kutupa masumbwi na Francis Miyeyusho wakati wa mpambano wao uliofanyika Dar es salaam jana. Picha na www.superdboxingcoach,blogspot.com
Bondia Obote ameme akioneshana kazi na Cosimasi Cheka
Bondia Miyayusho akisikiliza wimbo wa taifa wakati wa kuimba nyimbo za matasifa mawili
Bondia Rashidi Ali akioneshana kazi na Amnos Mwamakula wakati wa mpambano wao jana
 

WEMA, DIAMOND 'BADO WAPENZI'

JANA katika ukumbi wa Makumbusho, katikati ya Jiji la Dar es Salaam, mkabala na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), kulikuwa kuna onyesho la Miss Dar Inter College.
BIN ZUBEIRY alikuwepo na kamera yake katika onyesho hilo, ambalo Jaji Mkuu alikuwa Miss Tanzania wa 2006, Wema Sepetu huku mpenzi wake wa zamani, Nassib Abdul ‘Diamond Platinum’ akitumbuiza.
Shoo ilichelewa kuanza kidogo hadi mida ya saa sita usiku- na baada ya warembo kucheza shoo ya ufunguzi, kupita na vazi la ubunifu na la jioni, kabla ya tano bora kutangazwa, ilikuwa zamu ya Platinum wa bongo kupanda katika stage.
Taa zilizimwa na kijana akaibuka na madansa wake jukwaani. Lakini wakati tu MC anasema anamuita Diamond, mapigo ya moyo ya Jaji Mkuu, yalionekana kubadilika na kwenda kasi.
Kwa muda wote, Majaji wenzake wawili walikuwa wanawasiliana naye, lakini ilionekana ghafla kama yeye amekata mawasiliano nao.
Kulikuwa kuna dalili za kutosha kusema; Wema alichanganyikiwa. Dida wa Times FC aliyekuwa jaji pia, alijitahidi kadiri ya uwezo wake kumfanya Wema awe katika hali ya kawaida, lakini alishindwa.
Wema alishindwa kujimudu. Kulikuwa kuna dalili zsa kutosha kusema Wema anampenda sana Diamond. Alikuwa anamfuatilia kwa kila hatua. Alikuwa anaingiwa na kuguswa na nyimbo za Wema Wangu, Mawazo na Nimpende Nani alizokuwa anaimba Diamond pale jukwaani.
Diamond naye sasa; ilionekana dhahiri kila anachokifanya jukwaani ni kwa ajili ya Wema. Na alikuwa anaomba sapoti ya mashabiki ili kujiridhisha kama yuko sahihi.
Kwa sisi waswahili huwezi kusita kusema Diamond alikuwa anampiga ‘vikoleo’ aka vijembe Wema. Lakini pamoja na yote, Diamond alionekana kuwasilisha hisia zake kwamba hakuwa tayari kuachana na Wema.
Ni kama kuna kitu kilimsukuma kujitoa katika mahusiano. Ni nini hicho? Kitendawili kigumu.
Ikumbukwe wawili hawa walifikia hadi kuvalishana pete ya uchumba lakini ndani ya miezi michache tu, penzi likavunjika.
Ila, ndani ya mioyo yao kuna siri nzito sana na kinachoonekana anakosekana jasiri tu kati yao wa kumuanza mwenzake kuhusu mada ya kurejesha uhusiano wao.
Wanaonekana wanapendana bado, na haitakuwa ajabu siku moja wakirudiana. BIN ZUBEIRY mwenye uzoefu wa kutosha juu ya masuala ya mahusiano, raha na maumivu ya mapenzi, anawoambea wawili hao, siku moja wawe mwili mmoja tena. Mungu wabariki na wafungue, waondolee uzito Wema na Diamond. Siku moja, waitane wife n husband. Inshaallah. True love never die.













No comments: