RONALDO GUNDU LAANZA MAPEMAAA, AKOSA PENALTI URENO IKIPIGWA 3-1 NYUMBANI
Football | Uefa Euro 2012TM
URENO ilipoteza nafasi kibao,
ikiwemo Cristiano Ronaldo (pichani juu kushoto) kukosa penalti, katika mchezo
ambao walitandikwa mabao 3-1 nyumbani na Uturuki jana, kujiandaa na Fainali za
Kombe la Mataifa ya Ulaya, Euro 2012.
Kipigo hicho kinamaanisha kwamba,
Ureno itaingia kwenye Euro 2012 baada ya kucheza mechi tatu bila kushinda hata
moja. Pia walitoka sare ya 0-0 na Macedonia wiki iliyopita na wakatoka sare na
wenyeji washirika wa Euro, Poland mwezi Februari. Ureno wapo Kundi B pamoja na
timu kali tupu, Ujerumani, Uholanzi na Denmark.
|
|
MESSI NA ARGENTINA WAUA 4-0 KOMBE LA DUNIA
Football | World Cup 2014
UAMUZI wa Argentina kutumia washambuliaji wake wote
wanne 'babu kubwa' umezaa matunda, baada ya jana kufanikiwa kupata ushindi wa
4-0 dhidi ya Ecuador hivyo kuongoza mbio za kuwania tiketi ya kucheza Fainali za
Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil kwa nchi za Amerika Kusini.
Sergio Aguero, Gonzalo Higuain, Lionel Messi na
Angel Di Maria wote walifunga mabao katiuka mchezo ambao, Argentina walipata
mabao matatu ndani ya dakika 11 za kipindi cha kwanza.
Messi, alionyesha soka safi mno pengine kuliko
anayoonyesha Barcelona na alikuwa nyota ya mchezo huo uliopigwa kwenye Uwanja wa
Monumental, mjini Buenos Aires.
"Tunatakiwa kuwa timu ngumu, imara katika ulinzi na
hiyo itamfanya Lionel afanye mavitu yake kwa uhuru," alisema Alejandro
Sabella.
Argentina inaongoza kundi la Amerika Kusini kwa
pointi zake 10, baada ya kucheza mechi tano, ikiizidi pointi moja tu Chile,
ambayo iliifunga Bolivia 2-0 mjini La Paz, na mbili zaidi dhidi ya Uruguay na
Venezuela waliotoka sare ya 1-1 mjini Montevideo.
Pamoja na hayo, Argentina inawezwa kupitwa mwishoni
mwa wiki ijayo, wakati wakicheza mechi ya kirafiki na wapinzani wao wakubwa na
wenyeji wa fainali zijazo za Kombe la Dunia, Brazil nchini
Marekani.
| |
WATANZANIA WASHIRIKI MBIO ZA VITA DHIDI YA SARATANI YA MAZIWA MAREKANI
Wananchi hao wakiwemo
waTanzania walikusanyika katika viwanja vya Down Town Washington DC siku ya
Jumamosi June,2,2012 katika kuitikia wito wa kuunga mkono wanawake ambao
wanakabiliwa na ugonjwa wa saratani ya maziwa, utafiti na elimu dhidi ya ugonjwa
huo
Tukio hili liliaza kwa
matembezi ya vikundi vya mataifa mbali mbali wanaoishi hapa nchini
marekani
Watembeaji wengi
waliohudhuria katika matimbizi hayo kutoka majimbo mbali mbali nchini
Marekani
Maradhi ya saratani ya
maziwa yanakisiwa kuwadhuru watu 25 milioni kote ulimwenguni ambapo kama hatua
haitochukuliwa inakisiwa watu milioni 10 kufa katika kipindi cha miaka 25
ijayo.
Kina dada wwakiwa katika
matembezi ya kupiga vita ogonjwa wa saratani ya maziwa siku ya Jumamosi
June,2,2012 ndani ya washington D.C nchini Marekani.
Rais wa Jumuia ya
waTanzania DMV Mh. Iddi Sandaly, wakwanza kushoto, Waheeda Margaret Gathesha,
Chief wa swahilivilla Abou Shatry, Aunt Rehema, pamoja na Salma Jay Jay pia
alikuwepo katika matembezi ya kupigana na ujongwa wa saratani ya maziwa hapa
Washington DC.
Wazawa wa kitanzania
wanaoishi nchini marekani wakiwa katika matembezi ya kupiga vita ogonjwa wa
saratani ya maziwa mapema leo jumamosi June,4,2011 ndani ya washington D.C
nchini marekani.
Jamii iliyostaarabika
ni yenye kuheshimu Mawazo & Mitazamo ya wengine. Mchango wako katika kazi
yoyote ulenge kujenga jamii yenye Kujitambua, Kujithamini na
Kujiwajibisha.
Warembo wa kiTanzania
wakiwa mstari wa mbele katika mpango mzima wa kutimiza mwindo wa mile
tatu
Team Tanzania waki wakiwa
kipata picha ya pamoja katika kuitikia wito wa kuunga mkono wanawake ambao
wanakabiliwa na ugonjwa wa saratani ya maziwa, utafiti na elimu dhidi ya ugonjwa
huo.
Mamia ya watu kutoka
sehemu mbali mbali waliungana kwa pamoja katika zowezi hilo la kuunga mkono
wanawake ambao wanakabiliwa na ugonjwa wa Saratani ya maziwa.
Wana nchi wakiwa katika
mwendo wa Susan G.Komen. kumaliza vita dhidi ya maradhi ya Saratani ya Maziwa
Susan G.Komen. 2012!
Kina kaka nao pia
hawajajiweka nyuma kuunga mkono Susan G.Komen. kumaliza vita dhidi ya maradhi ya
Saratani ya Maziwa Susan G.Komen. 2012! ndani ya Washington DC.
Ahsanteni sana Auntie
Rehema na Dada Zuhura, kwa kutupa muamko wa kuwajibila na kushiriki katia zowezi
haya hili la kupiga vita ugonjoa huu wa satarani ya maziwa. M/mungu akujalie
Afya njeema Insha-Allah Ameen.!
Latino Team pia
hawakujiweka nyuma kupiga vita ungonywa huo hatari unaowapa tabu kina Mama
Ghana Team pia
walishiriki katika zowezi zima la Susan G.Komen. kumaliza vita dhidi ya maradhi
ya Saratani ya Maziwa Susan G.Komen. 2012
Mamia ya wananchi wakiwa
katika matembezi ya Susan G.Komen. 2012! Down Town Washington DC
Dada Sofia na akiwa
katika matembezi pamoja na Team Tanzania na nyengine mchanganyiko
Team Tanzania baada ya
kumaliza matembezi ya Susan G.Komen. dhidi ya kupiga vita maradhi ya Saratani
ya maziwa. (Picha maelezo na swahilivilla.blogspot.com)
FERGUSON SASA AGEUKA MKONO WA BIRIKA
Tetesi za J'pili magazeti Ulaya
FERGUSON APEWA BEI CHAFU KUWANASA MODRIC, TIOTE, BAINES
KOCHA Sir Alex Ferguson
ameambiwa kwamba Manchester United itatakiwa kulipa jumla ya pauni Milioni 72
ili kuwapata wachezaji watatu inayowataka - lakini hayuko tayari kutoa fungu
hilo kwa ajili ya nyota hao, Luka Modric, mwenye wa miaka 26 wa Tottenham,
Leighton Baines mwenye umri wa miaka 27 wa Everton na Cheick Tiote mwenye umri
wa miaka 25 wa Newscastle.
KLABU
ya Manchester United imemlenga nyota wa Valencia, Jordi Alba, mwenye umri wa
miaka 23, kwa kutoa fedha na mchezaji ili kumnasa nyota huyo na mchezaji
watakayemtoa atakuwa Mbrazil, Anderson.
KUTOKA
kwa mchezaji maarufu wa Liverpool, mshambuliaji Dirk Kuyt, mwenye umri wa miaka
31, inaweza kuwa sehemu ya mpango wa kubadilishana wachezaji na Fiorentina, na
beki wa pembeni mwenye thamani ya pauni Milioni 12, Juan Manuel Vargas, mwenye
umri wa miaka 28.
KLABU
ya Manchester City itaanza kumwaga fedha za usajili kwa ajili ya msimu ujao kwa
kutoa pauni Milioni 25 kumnasa beki wa Athletic Bilbao, mwenye umri wa miaka
23, Javier Martinez.
TAARIFA
za vyombo vya habari nchini Hispania, zimesema Tottenham imepiga hatua ya
mawasiliano rasmi ya kumsajili mshambuliaji wa Athletic Bilbao, mwenye umri wa
miaka 27, Fernando Llorente.
KLABU
ya QPR inajipanga kumpa ofa kipa wa Tottenham, Heurelho Gomes, mwenye umri wa
miaka 31, ili akafufue makali yake Loftus Road.
KLABU
ya Arsenal ina nia ya kumsajili mshambuliaji kinda wa miaka 18 wa Crewe mwenye
thamani ya pauni Milioni 10, Nick Powell.
KLABU
ya Southampton imetenga dau la pauni Milioni 2 kumnasa kiungo wa Millwall, Liam
Trotter mwenye umri wa miaka 23, ambaye amekuwa akihusishwa na mpango wa
kutimkia Fulham na Sunderland.
REDKNAPP MAMBO MAGUMU
MWENYEKITI
wa Tottenham, Daniel Levy amekataa kumuongezea mkataba kocha Harry Redknapp,
ambaye alitaka apewe miaka mitatu zaidi katika mkataba wake uliobakiza mwaka
mmoja na ongezeko la maslahi yake. Hii inamaanisha wawili hao watafanya kazi kwa
mgogoro mkubwa msimu ujao.
KOCHA
mpya wa Liverpool, Brendan Rodgers mpango wake wa muda mrefu ni kutwaa taji na
klabu hiyo, akisema; "Yanaweza kuwa manne".
BEKI
wa Manchester United, Nemanja Vidic amepewa ruhusa ya kuanza mazoezi kamili
mwanzoni mwa mwezi ujao.
No comments:
Post a Comment