Sunday, June 24, 2012

BREAKING NEWS! SIMBA YAMSAJILI BEKI MASOMBO LINO TOKA DC MOTEMA PEMBE

Hatimae wekundu wa msimbazi Simba leo hii wamefanikiwa kumsajili beki MASOMBO LINO kutoka klabu ya Dc Motema Pembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Masombo Lino amabaye anacheza nafasi ya beki wa kati amekamilisha uhamisho mara tu baada ya kutua nchini leo asubuhi, awali Simba ilitaka kumsajili beki wa zamani wa Étoile Sportive du Sahel ya nchini Tunisia Gladys Bokese amabaye kwasasa anaichezea Dc Motema Pembe lakini imesitisha mpango huo na kuamua kumpa kibarua MASOMBO.

OKWI AGEUKA LULU SOKO LA USAJILI: SASA TIMU MOJA YA SERIE A NA MAMELODI SUNDOWNS ZAGOMBEA SAINI YAKE

Nyota ya mshambuliaji wa kimataifa wa Simba raia wa Uganda Emmanuel Okwi, inazidi kuwaka, siku chache baada ya klabu bingwa ya Orlando Pirates kutuma barua ya kumtaka mshambuliaji huyo wa Simba aende kufanya majaribio kwenye klabu hiyo, leo hii timu pinzani ya Orlando kwenye ligi ya Afrika kusini, Mamelodi Sundowns wameuambia uongozi wa Simba kwamba wapo tayari kumnunua mshambuliaji huyo.

Taarifa zilizothibitishwa kutoka ndani ya uongozi wa Simba zinasema kwamba Mamelodi wametuma maombi ya kutaka kumsaini Okwi ambaye amekuwa na msimu mzuri sana ndani na nje ya ligi kuu ya Vodacom msimu ulioisha.

Pia chanzo changu hicho cha habari kutoka ndani ya Simba kilisema kwamba kuna timu moja inayoshiriki ligi kuu ya Italia Serie A, wameonyesha nia ya kumtaka Okwi lakini wamesema kwamba wanasubiri mpaka michuano ya Euro itakapoisha ndipo watakapoamua juu ya suala la usajili wa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uganda

No comments: