Wednesday, May 16, 2012


RASMI LIVERPOOL YAMTUPIA VIRAGO DALGLISH


EXIT ... Kenny Dalglish has left Liverpool
EXIT ... Kenny Dalglish has left Liverpool
Published: 56 minutes ago

KENNY DALGLISH amefukuzwa na Liverpool baada ya miezi 16 ya kufanya kazi.

Mkataba wa Mcotland huyo umevunjwa wakati yeye akiwa Marekani.
Licha ya kuiongoza klabu hiyo, kutwaa Komeb la Ligi maarufu kama Carling Cup na kucheza fainali ya Kombe la FA, ambako ilifungwa kwa utata na Chelsea, lakini kufanya vibaya kwenye Ligi Kuu kumemponza.
Ikiwa imemaliza katika nafasi ya naneLigi Kuu- hiyo ni kinyume cha matarajio ya klabu hiyo, kupata nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa.
Liverpool imemaliza msimu ikiwa na pointi 52 —ambazo ni chache zaidi kihistoria katika ushiriki wao kwenye Ligti, wakizidiwa kete na wapinzani wao wa Merseyside, Everton.
Wakali hao wa Anfield pia walishinda mechi chache mno kihistoria msimu huu, 14, tangu msimu wa 1953-54 na wamfunga mabao machache zaidi (47) tangu msimu wa 1991-92.
Wamiliki wa timu pia hawakufurahishwa na jinsi alivyokuwa akimchukulia Luis Suarez .
Dalglish alitua Liverpool akirithi mikoba ya kocha wa sasa wa England, Roy Hodgson Januari mwaka jana.

YANGA WAMPONZA KIIZA, ATEMWA THE CRANES, OKWI NDANI



KUFULIA kwa Yanga sasa kunaanza kumgharimu hata mshambuliaji wake, Mwanasoka Bora wa Uganda, Hamisi Kiiza.
Kocha wa The Cranes, Bobby Williamson leo ametaja kikosi cha awali cha wachezaji 30 kwa ajili ya maandalizi ya mechi dhidi ya Angola na Senegal kuwania Fainali za Kombe la Dunai mwaka 2014, huku akimoiga chini mchezaji huyo matata.
The Cranes itakwenda Luanda, Angola Juni 3, mwaka huu kucheza na wenyeji kabla ya kumenyana na Senegal mjini Kampala, Juni 9. Liberia ni timu nyingine kwemnye kundi lao.
Kikosi kamili cha Cranes ni; Makipas: Denis Onyango (Sundowns, SA), Posnet Omwony (Leopards, SA), Abel Dhaira (IBV, Iceland), Hamza Muwonge (Bunnamwaya),
Mabeki: Simeon Masaba (URA), Denis Guma (Victoria University), Isaac Isinde (St George, Ethiopia), Henry Kalungi (Richmond Kickers, USA), Godfrey Walusimbi (Bunnamwaya), Hassan Wasswa (Kayseri, Turkey), Joseph Ochaya (KCC), Andy Mwesigwa (Ordabasy, Kazakhstan), Habib Kavuma (APR, Rwanda), Edward Ssali (Bunnamwaya), Joseph Owino (Azam, TZ)
Viungo: Mike Sserumaga (St George, Ethiopia), Tonny Mawejje (IBV, Iceland), Musa Mudde (Sofapaka, Kenya), Patrick Ochan (TP Mazembe, DRC), Martin Mutumba (AIK, Sweden), Dan Wagaluka(APR, Rwanda), Moses Oloya (Sai Go, Vietnam), Sula Matovu (St George, Ethiopia), Mike Mutyaba (El Merreikh, Sudan)
Washambuliaji: Brian Umony (Becamex Binh Doung, Vietnam), Emma Okwi (Simba, TZ), Caesar Okhuti (Bunnamwaya), Robert Ssentongo (URA), Geoffrey Massa (Yenicami, N. Cyprus), Fabian Kizito (Leonidas, Netherlands)

No comments: