Wednesday, April 25, 2012
DAR ES SALAAM DERBY COUNTDOWN: YANGA WATUMA SALAMU MSIMBAZI - WAIFUMUA JKT OLJORO 4-1
YANGA, imekumbuka
shuka, wakati kumekucha baada ya jana kuichapa JKT Oljoro mabao 4-1, katika
mchezo Ligi Kuu Tanzania Bara, uliochezwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid,
mjini Arusha.
Kwa matokeo hayo,
Yanga imeweza kufikisha pointi 49 huku ikiendelea kushika nafasi ya tatu, baada
ya Azam kufikisha pointi 50 inayoshika nafasi ya pili, wakati Simba inaongoza
kwa pointi 59.
Yanga ambao walikuwa
mabingwa watetezi wa ligi hiyo, imelitema kombe hilo, baada kuboronga mechi
mbili huku ikinyang'anywa pointi tatu na Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Soka
Tanzania.
Kamati hiyo,
ilichukua uamuzi huo, baada ya Yanga kumchezesha, Nadir Haroub 'Cannavaro'
katika mechi yao dhidi ya Coastal Union, iliyochezwa Machi 31, kwenye Uwanja wa
Mkwakwani, Tanga.
Yanga ilimtumia
mchezaji huyu ambaye alikuwa anatumikia adhabu ya kadi nyekudu kutokana na
kumshambulia mwamuzi Israel Nkongo, aliyechezesha mechi yao dhidi ya Azam, Machi
10, mwaka huu, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Hata hivyo, matarajio
ya Yanga kupata nafasi ya kuiwakilisha nchi katika michuano ya Afrika mwakani
ni finyu, kwani imesaliwa na mechi moja dhidi ya Simba itakayochezwa Mei 5,
mwaka huu, Uwanja wa Taifa.
Katika mechi hiyo,
Yanga ikishinda itafikisha pointi 52, ambapo Azam itakuwa na uwezo wa kufikisha
pointi 56 iwapo itashinda michezo miwili dhidi ya Toto African na Kagera Sugar,
huku ikisubiri hatma ya matokeo ya mechi yao dhidi ya Mtibwa Sugar ambayo juzi
ulivunjika kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.
Mechi hiyo,
ilivunjika baada ya timu hizo kufunga bao 1-1, lakini mwamuzi wa mchezo huo
Rashid Msangi kutoka Dodoma, alivunja pambano hilo, kwa madai Mtibwa waligomea
penelti..
Katika mchezo
wa
kwanza
uliochezwa kwenye
Katika mchezo huo wa
jana, Yanga iliandika bao dakika ya 36 likifungwa na Hamisi Kiiza, kabla ya
Haruna Niyonzima kufunga la pili dakika 40.
Yanga ikicheza bila
Kocha mkuu wake, Kostadin Papic, Kiiza alifunga bao la tatu ikiwa ni dakika moja
kabla ya kwenda mapumziko ambapo Pius Kisambale akihitimisha 'sinia' la mabao
katika dakika 84.
Bao la kufutia
mafunzo la JKT Oljoro lilifungwa na kwa njia ya penelti.
KUTOKA KWA UPUMBAVU WA ZIDANE MPAKA UJINGA WA TERRY JANA: KADI NYEKUNDU ZA KIJINGA ZA MUDA WOTE KWA WACHEZAJI MAARUFU.
BECKHAM LASHES OUT (1998) |
CARRAGHER IN COIN CONTROVERSY
(2002) |
BOWYER & DYER EXCHANGE BLOWS (2005) |
A ROUND OF APPLAUSE FOR ROONEY
(2005) |
ROBBEN'S LACK OF CROWD CONTROL
(2006) |
ROONEY RUBBER-STAMPS ENGLAND EXIT (2006) |
ZIDANE LOSES HIS HEAD (2006) |
SCHOLES' HANDY WORK LANDS HIM IN TROUBLE
(2008) |
SLAP-AN IBRAHIMOVIC
(2012) |
TERRY'S KNEED-LESS RED CARD (2012) |
WAARABU WA SIMBA - AL ALHLY SHANDY KUDONDOKA BONGO KESHO - KUWAONA DHIDI YA SIMBA NI 5000 - 3000
SIMBA SPORTS
CLUB
P.O.BOX 15318 | TEL+255 222183330
|FAX +255 222183330 |MSIMBAZI/MCHIKICHI STREET | DAR ES SALAAM | TANZANIA |
EMAIL simbasportsclub@yahoo.com|
WEBSITE www.simba.co.tz|
AFFILIATED TO TFF, DRFA and IDFA
25/04/2012
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
NDUGU
waandishi.
Kama mnavyofahamu,
Jumapili ya Aprili 29 mwaka huu, timu ya soka ya Simba inakutana na klabu ya Al
Ahly Shandy kutoka Sudan katika mchezo wa hatua ya 16 bora ya michuano ya Kombe
la Shirikisho (CAF), kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Simba ni timu pekee
kutoka katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) iliyobaki katika
michuano yote ya kimataifa inayosimamiwa na CAF.
Kubwa zaidi, ndiyo
wawakilishi pekee wa Tanzania waliobaki katika michuano ya kimataifa na hivyo
wanabeba bendera ya taifa kokote kule waliko.
Maandalizi yote kwa
ajili ya pambano hilo yamekamilika.
Wapinzani wetu, Al
Ahly wanatarajiwa kuwasili kesho saa saba mchana kwa ndege ya Ethiopia
Airlines.
Waamuzi na Kamishina
wa mchezo wamepangwa kuwasili Ijumaa (keshokutwa) wakitokea nchini Swaziland na
Rwanda.
VIINGILIO
Kutokana na ukweli
kwamba mechi hiyo itakuwa ya kimataifa, Simba imepanga viingilio ambavyo kila
mwananchi ataweza kuvimudu. Viingilio vitakuwa kama ifuatavyo.
Viti vya bluu na
kijani itakuwa Sh. 5,000, Rangi ya Chungwa Sh, 10,000, VIP C 15,000, VIP B
20,000 na VIP A 30,000.
Tiketi zitauzwa
katika maeneo yafuatayo, Big Bon, Benjamin Mkapa, Stears Mjini, Mbagala Dar
Live, OilCom Buguruni, Tandika Mwembeyanga, Ubungo Oilcom, Mwenge Bus Stand, BP
Mwananyamala na Gapco Ukonga.
Tiketi zitaanza
kuuzwa siku ya Ijumaa asubuhi katika maeneo yaliyotajwa.
Klabu imepokea maombi
mengi kutoka kwa wanachama na wapenzi wake kutoka mikoani na ingeomba kwamba
wale wanaotaka kuja kutazama mechi hii kwa makundi kutoka mikoani, wawasiliane
mapema na uongozi ili wanunuliwe tiketi zao mapema.
Simba SC imechapa tiketi za
kutosha na ingeomba wapenzi na wanachama wake kujitokeza kwa wingi kwenye
pambano hilo.
Wana Simba wote
wanaombwa kuja uwanjani wakiwa wamevalia mavazi yao ya rangi Nyekundu na Nyeupe
ili uwanja mzima upendeze kwa rangi hizo.
Tunatoa wito kwa
vyombo vya habari kuisaidia Simba na Tanzania kwa kuelekeza nguvu zao katika
uandishi wa taarifa ambazo zitaisaidia timu yetu kusonga mbele na si kuondoa
morali au kusababisha watu wasiende uwanjani.
Shukrani.
Uongozi wa Simba SC
unatoa shukrani, kwa namna ya kipekee kabisa, kwa serikali kutokana na uamuzi
wake wa kuruhusu Wekundu wa Msimbazi kufanya mazoezi katika Uwanja wa Taifa
kujiandaa na mechi hii muhimu.
Ezekiel
Kamwaga
Msemaji
Simba SC
KWANINI KILA SIKU NI AZAM TU: MECHI YAO YA 3 REFA AWA CHANZO CHA MATATIZO MCHEZONI.
Kwa mara ya tatu
katika kipindi cha miezi miwili, juzi refa aliyechezesha mechi ya Azam FC katika
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, alikuwa chanzo cha matatizo mchezoni.
Mtibwa waligomea
mechi na kuondoka uwanjani wakiwa wamefungana 1-1 na Azam FC, Uwanja wa Azam,
Chamazi.
Msimu uliopita Mtibwa
Sugar walifungwa nyumbani na Azam mabao manne, hawakuleta tatizo, lakini juzi
wakiwa wapo 1-1 wakaamua kugoma.
Waligoma baada ya
kuchoshwa na maamuzi mabovu ya refa, ikiwemo kuwapa penalti ambayo si halali
wenyeji.
Hii ni mara ya tatu
ndani ya miezi miwili, marefa wanaochezesha mechi za Azam wanakuwa sababu ya
kuvurugika kwa mchezo.
Wiki mbili zilizopita
tu, refa aliyechezesha mechi kati ya Azam FC na wenyeji Polisi Dodoma, Uwanja wa
Jamhuri alipigwa na mashabiki baada ya mechi.
Azam ilishinda 1-0,
beo pekee la beki wake wa kati wa kimataifa wa Tanzania, Aggrey Morris Ambroce
dakika ya 83 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya wenyeji
Polisi Dodoma.
Katika mchezo huo,
Polisi Dodoma, ilipata pigo baada ya beki wake, Bakari Omari kutolewa nje kwa
kadi nyekundu, dakika ya 57 baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya
njano.
Refa wa mchezo huo
alipigwa na mashabiki kwa madai ya kuwapendelea Azam, baada ya mpambano
kukamilika, lakini askari walifanikiwa kumuokoa asipokee kipondo
zaidi.
Awali, mwezi
uliopita, refa aliyechezesha mechi kati ya Yanga na Azam, Israel Nkongo alipigwa
na Stefano Mwasyika na angeweza kupigwa pia na mashabiki wa Yanga.
Kwa nini apigwe? Kisa
kutuhumiwa kuipendelea Azam. Mechi zinazochezwa kwenye Uwanja wao, timu nyingi
zimekuwa zikilalamika Azam inabebwa.
Kwa muda mrefu
wapenzi wa soka Tanzania wamekuwa wakilalamikia desturi ya klabu kongwe nchini
Simba na Yanga kutamba nyumbani, kudaiwa kushinda kwa kununua
mechi.
Hii inasababisha timu
zetu zinakuwa dhaifu kwenye michuano mikubwa na ndiyo maana zinashindwa japo
kucheza hatua ya makundi tu ya michuano ya Afrika.
Watu wanataka timu
ishinde kwa uwezo, ili idhihirishe ubora ambao utakwenda kuifanya ishiriki vyema
michuano ya Afrika.
Kwa sababu hiyo, ujio
wa Azam FC timu inayomilikiwa na Milionea Said Salim Bakhresa ulipokewa kwa
furaha na wadau wa soka nchini, wakijua amepatikana mkombozi wa
kweli.
Azam imewekeza fedha
nyingi kuanzia kwenye usajili, ajira za makocha, Uwanja wake kule Chamazi- na
kwa ujumla ni timu ambayo ukiangalia inapoelekea unajenga
matumaini.
Azam haina wanachama
wa kuleta mizengwe ya kuvuruga timu, wanaweza kujivuruga wao kwa wao
tu.
Mchezaji wa Azam
hachezi kwa presha ya kutukanwa na mashabiki akikosea kama mchezaji wa Yanga au
Simba. Azam imesajili wachezaji nyota kuanzia ndani na nje ya nchi.
Azam inaongoza
kutumia fedha nyingi na kusajili wachezaji bora nchini. Hivyo timu hii
inastahili kuwa bingwa wa nchi kulingana na jinsi ilivyowekeza.
Lakini wasiwasi ni
kwamba, mechi zao zinatiliwa shaka sasa nao kama wanatumia mbinu chafu ikiwemo
kuhonga marefa ili kushinda.
Kama kweli watakuwa
wanafanya hivyo, ina maana watakuwa wanaiga Simba na Yanga, ambazo kimsingi
zinanyooshewa kidole kwa kudumaza maendeleo ya soka ya nchi hii.
Kama Azam wanaiga
Simba na Yanga kununua mechi, wanaweza wakafanikiwa kuwa mabingwa, lakini swali
la kujiuliza soka ya Tanzania itakuwa kweli imepata mkombozi?
Napata shaka sana juu
ya mustakabali wa soka ya nchi hii, ikiwa Azam nayo inakuja kwa staili hii-
dhahiri bado tuna kazi ngumu na safari ndefu kufikia japo karibu na
mafanikio.
Kwa sababu mchezaji
akishajua kwamba kuna unafuu katika mchezo kutokana na mabosi wao kuhonga,
hawezi kujituma tena kwa sababu anajua ushindi upo tu.
Mwaka 2007, baada ya
Yanga kutolewa katika Ligi ya Mabingwa Afrika na Esperance ya Tunisia, aliyekuwa
kipa wa timu hiyo, Ivo Mapunda aliwashauri viongozi wa klabu yake wakati huo,
wawe wanafanya mipango na marefa kurahisisisha mechi.
Tayari mchezaji
kujenga dhana hiyo- inamaanisha amefikia mwisho wa uwezo wake, wakati suluhisho
ni kufanyia kazi mapungufu ili wakati mwingine ufanye vizuri.
Mwaka juzi, Simba
ilifungwa 5-0 na Haras El Hodood nchini Misri katika mchezo wa Kombe la
Shirikisho, mwaka jana ilifungwa 3-0 na Wydad Cassablanca, mara zote ikitolewa
katika michuano ya Afrika.
Mwaka huu, imefungwa
3-1 ikitoka kushinda 2-0 nyumbani na ES Setif moja ya timu tishio tu Afrika na
kuingia hatua ya 16 Bora ya Kombe la Shirikisho.
Hii nini maana yake?
Simba imefanyia kazi mapungufu kutoka kufungwa 5-0, 3-0 na 3-1 sambamba na
kusonga mbele.
Lakini desturi ya
kutaka kurahisisisha kazi kwa kununua mechi- maana yake hatuwezi kufanyia kazi
mapungufu.
Kweli wapenzi wa soka
Tanzania wanaitegemea Azam iijengee heshima nchi hii katika michuano ya Afrika,
lakini kwa staili ambayo wanataka kwenda nayo. Hakuna hakika kama
watafanikiwa.
Yapo maneno tayari
yanasemwa semwa kuhusu Azam na harakati zao za ubingwa na mbinu wanazodaiwa
kutumia hadi watu wanaodaiwa kutumiwa kutoka kwenye mamlaka husika- japo kwa
sasa tunayachukuliwa kama maneno ya mtaani tu, lakini ipo haja ya kuiangalia
Azam kwa jicho la tatu.
Haina maana Yanga
kukosekana michuano ya Afrika mwakani, wakati ilipigana kwa uwezo wake na
kuzidiwa na timu ambayo ushindi wake ulitokana na mbeleko za
marefa.
Namna hii hata mtu
huwezi kustaajabu kwa nini John Bocco mabao yake anafunga Azam tu na timu ya
taifa anabaki yeye na kipa mara kibao anashindwa. Akizomewa eti anasusa.
Watu hawataki
kujadili ukweli wa kiini cha tatizo, kwa sababu tayari kuna kosa lilitendeka-
lakini hawajui kwamba hata kosa lina sababu.
Jasiri yoyote
hakubali kudhulumiwa haki yake bana- tusidanganyane na wala watu wasitake
kujiona wao miungu watu katika dunia hii- misingi ya haki ni ile
ile.
Kila jina zuri lina
jina mbadala la uasi- watu wakikupenda kwa ujasiri wako wa kutopenda kuonewa
kiasi cha kuwa tayari kupambana na yeyote kutetea haki, watakuita jasiri,
shujaa, shupavu.
Lakini kwa sababu
hizo hizo, wakiwa hawakupendi watakuita mkorofi- mgomvi, huelewani na watu- hiyo
ndio dunia yetu ya leo- dunia tofauti na ile waliyoishi akina Mtemi Mirambo,
Chifu Mkwawa na Adolph Hitler.
Mtibwa walikuwa
wastaarabu wakaondoka uwanjani- hawajui mbali na kupoteza pointi tatu, watatozwa
faini na sijui kanuni zinasemaje zaidi, ili kuna hatari ya kufungiwa pia kucheza
ligi.
Wachezaji wa Yanga
waliona bora kumtandika Nkongo- hawakujua mbele yake kuna kufungiwa kucheza na
kuigharimu zaidi klabu yao.
Lakini chanzo cha
yote haya ni nini? Azam hao. Wanafanya nini, sijui na sina ushahidi kama
wanahonga marefa na siwezi kusema wanahonga marefa, ila naweza kujiuliza kwa
nini wawe wao tu? Mara moja bahati mbaya- lakini sasa mara ya tatu jamani, timu
hiyo hiyo moja! Hapana bwana!
CHEKA AJIFUA KUMKABILI MAUGO JUMAMOSI HII
Kocha wa mchezo wa Masumbwi Abdalah Ilamba 'Komandoo' akimfanyisha mazoezi ya kukaza misuli ya tumbo bondia Francis Cheka Dar es salaam jana Chaka anajiandaa na mpambano wake na Mada Maugo utakaofanyika jumamosi hii katika ukumbi wa PTA Sabasaba ambapo mshindi atakuwa bingwa wa Mkanda wa I.B.F na atanyakua Zawadi ya gari.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Tuesday, April 24, 2012
SUAREZ DHIDI YA AKINA ROONEY - BRAZIL WAPANGWA KUNDI MOJA NA MISRI - OLYMPIC 2012
Brazil legend Ronaldo akitangaza makundi ya michezo ya
Olympic itakayofanyika nchini Uingereza .
GROUP A
GROUP A
Great Britain
Senegal
UAE
Uruguay
Senegal
UAE
Uruguay
Fixtures: July 26,
Manchester, UAE v Uruguay, Great Britain v Senegal; July 29, London, Senegal v Uruguay, Great
Britain v UAE; August 1, Cardiff, Great
Britain v Senegal; Coventry, Senegal v UAE
GROUP B
MexicoNorth Korea
Gabon
Switzerland
Fixtures: July
26, Newcastle, Mexico v N Korea, Gabon v Swiss; July 29, Coventry, Mexico v Gabon, N Korea,
Switss; August 1, Cardiff, Mexico v
Swiss; London, N Korea v Gabon
GROUP C
BrazilEgypt
Belarus
New Zealand
Fixtures: July
26, Coventry, Belarus v New Zealand; Cardiff, Brazil v Egypt; July 29, Manchester, Brazil v Belarus, Egypt v
New Zealand; August 1, Newcastle, Brazil
v New Zealand; Glasgow, Egypt v Belarus
GROUP D
SpainJapan
Honduras
Morocco
Fixtures: July 26,
Glasgow, Spain v Japan, Honduras v Morocco; July 29, Newcastle, Spain v Honduras, Japan v
Morocco; August 1, Coventry, Japan v
Honduras; Manchester, Spain v Morocco
FIRST DIVISION LEAGUE FINALS 2011 - 2012
NO | TEAMS | P | W | D | L | GF | GA | GD | PTS | YLW | RED | TOTAL | |
1 | Polisi Moro FC | 8 | 6 | 2 | 0 | 16 | 5 | 11 | 20 | 12 | 0 | 12 | |
2 | Mgambo Shooting | 8 | 4 | 3 | 1 | 12 | 6 | 6 | 15 | 15 | 1 | 16 | |
3 | Tanzania Prisons | 8 | 4 | 2 | 2 | 10 | 6 | 4 | 14 | 12 | 0 | 12 | |
4 | Polisi Dar FC | 8 | 3 | 4 | 1 | 11 | 4 | 7 | 13 | 11 | 1 | 12 | |
5 | Mbeya City FC | 8 | 3 | 2 | 3 | 10 | 8 | 2 | 11 | 8 | 1 | 9 | |
6 | Rhino Rangers FC | 8 | 2 | 2 | 4 | 4 | 8 | -4 | 8 | 9 | 1 | 10 | |
7 | Mlale JKT | 8 | 2 | 2 | 4 | 8 | 15 | -7 | 8 | 7 | 1 | 8 | |
8 | Polisi Tabora FC | 8 | 1 | 3 | 4 | 7 | 14 | -7 | 6 | 8 | 0 | 8 | |
9 | Transit Camp | 8 | 0 | 2 | 6 | 3 | 15 | -12 | 2 | 7 | 0 | 7 | |
TOTAL | 36 | 13 | 11 | 13 | 81 | 81 | 0 | 97 | 89 | 5 | 94 | ||
AS FOR: 23.04.2012 | |||||||||||||
Average of Goal per game | 2.3 | ||||||||||||
Average of Yellow Cards per game | 2.5 | ||||||||||||
Average of Red Cards per game | 0.1 | ||||||||||||
Average of Total Cards per game | 2.6 |
Subscribe to: Posts (Atom)
No comments:
Post a Comment