Neema Namangaya, mkazi wa Mtwara vijijini ambaye anafuatilia cheti cha kuzaliwa cha mwanaye katika ofisi ya Wakala wa Usajili wa Vizazi na Vifo (RITA) mkoa wa Mtwara. |
Neema Namangaya |
Afisa Tawala wa wilaya ya Mtwara, Edith Shayo, akitolea ufafanuzi juu ya malalamiko ya wananchi kuhusu adha wanayoipata katika kufuatilia vyeti vya kuzaliwa vya watoto. |
Na Juma
Mohamed.
WANANCHI wa
halmashauri ya Mtwara vijijini wamepaza sauti zao kuulalamikia uongozi wa Wakala
wa Usajili wa Vizazi na Vifo (RITA) mkoa wa Mtwara, kutokana na usumbufu
wanaoupata katika ufuatiliaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wachanga.
Wananchi hao
ambao wanalazimika kusafiri kutoka vijijini kufuata huduma hiyo katika manispaa
ya Mtwara Mikindani, walisema wanajikuta wanatumia gharama kubwa ya fedha
katika nauli na kujikimu wanapokuwa mjini hapa kwa ajili ya kusubiri kwa
kufuata maagizo wanayopewa na wahusika.
Wakizungumza
juzi wakiwa nje ya ofisi hiyo, walisema mara kadhaa wamekuwa wakitekeleza bila
mafanikio, maagizo wanayopewa na wahusika kwa kuwapangia tarehe za kupatiwa
vyeti hivyo lakini inashindikana kutokana na ofisi kuwa inafungwa kila
wanapofika na kukosa mtu wa kuwahudumia.
Husna
Mohamed, mkazi wa kijiji cha Nanguruwe, alisema alianza kufuatilia cheti kwa
ajili ya mwanaye tangu miezi sita iliyopita lakini bado hajafanikiwa na kwamba
kila akifika ofisini hapo anapangiwa tarehe.
Liliane Vicent, mkazi wa Mtwara vijijini akizungumzia namna anavyokumbana na vikwazo katika kufuatilia cheti cha mtoto wake, katika ofisi ya Wakala wa Usajili wa Vizazi na Vifo (RITA) mkoa wa Mtwara. |
“Tunashindwa
kuwaelewa kwasababu sisi tunatumia nauli na maisha magumu, ndio maana sisi
hatuwaelewi hawa watu..na sisi tumefikia sehemu za watu mjini hapa, tutakula
nini anaposema tusubiri mpaka Jumatatu na lao Al-Hamis (juzi)..na sheria za
kazi Al Hamisi mtu anakuwa kazini sasa tunamshanga sijui Babu sijui kijana
aliko huko tunashangaa kila tukifika hapa hayupo..” alisema.
Alisema ofisi
hiyo ilifungwa na hakukuwa na mtu isipokuwa walijibiwa na mtu wa ofisi nyingine
(hakumtaja jina) kuwa mwenyewe hayupo na kuwataka warudi tena siku ya Jumatatu.
Alisema,
ofisi hiyo imeanza kufungwa tangu mwezi Agosti mwaka huu baada ya kuanza kwa
kampeni za Uchaguzi mkuu wa Madiwani, Wabunge na Rais uliofanyika mwezi Oktoba,
kutokana na muhusika kuamua kujiingiza katika siasa.
“Yani tangia
mwezi wa Nane kipindi cha kampeni kile, pale hapakuwa na mtu ukifika tu
unaambiwa pamefungwa hayupo, mwenyewe amesafiri..zamani hapo alikuwa anafanya
kazi ila baada ya kuanza kampeni mpaka hatua hii hafanyi kazi, pale pamefungwa
nendeni mkapige picha tu muone..” aliongeza Husna.
Naye Liliane
Vicent, alisema alianza kufuatilia toka mwezi June ambapo mpaka sasa bado
hajafanikiwa kupata cheti jambo ambalo linampa gharama kubwa ya nauli kutokana
na namna anavyopangiwa tarehe za kurudi kila baada ya mwezi huku kukiwa hakuna
mafanio yoyote.
Neema Namangaya |
“Toka mwezi
wa sita nikja hapa naamibwa uje mwezi wa Saba, nilipofika sikupata nikaambiwa
mpaka mwezi wa Nane, nilipofika mwezi wa Nane sikupata nikaambiwa njoo mwezi wa
Tisa, nilipofika sijamkuta..basi yakaanza masuala ya uchaguzi nikaona haina
jinsi nikaamua kubaki nyumabni..” alisema.
Kwa upande
wake, Afisa Tawala wa wilaya ya Mtwara, ambako ndiko kuna ofisi hiyo, Edith
Shayo, alikiri kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi hao na kusema kuwa mara
kadhaa anajitahidi kutoka na kuwaeleza changamoto walizo nazo zinazosaabisha
ofisi kufungwa na wao kukosa huduma.
Alisema,
ofisi hiyo ina mtumishi mmoja hadi sasa ambaye anafanya kazi zote na kwamba
akipatwa na dharula basi ofisi inafungwa kutokana na kukosa msaidizi huku
akisema kuwa mtumishi aliyekuwepo awali alijiingiza katika masuala ya kisiasa
kwa kugombea Udiwani katika kata moja ambaye hakuitaja.
Edith Shayo |
Alisema kutokana
na maamuzi yake hayo ambayo yalimuondoa moja kwa moja katika utumishi wa Wakala
hiyo ya Serikali, walilazimika kumtafuta mtu mwingine ambaye walimuelekeza
namna ya kutekeleza majuku ya ofisi hiyo, ambapo baada ya kujiridhisha kuwa
anaweza kufanya wakamkabidhi ofisi ambapo anaendelea na kazi hadi sasa lakini
toka wiki iliyopita alisafiri kwenda jijini Dar es Salaam kwa ajili ya masuala
ya kiofisi.
“Nafikiri ni
toka Al Hamisi iliyopita alisafiri kuna kikao huko Dar es Salaam kwa masuala hay
ohayo ya RITA, kuna stakabadhi amepeleka walimuita wenyewe, na ndio maana
umeona ofisi imefungwa..ni kweli watu huko nje unasikia wakilalamika na binafsi
hua natoka na kuwaeleza, unajua sisi ni binadamu unakuta mtu anakuja amesimama
mda mrefu ..hata juzi mimi nilikua hapa si unajua watu wanajazba..” alisema.
Kuhusu usumbufu
wa kurudishwa mara kwa mara kwa kupangiwa tarehe za kufuata vyeti kwa wananchi,
alisema alikuwa hafahamu chochote juu ya changamoto hiyo na kudai kuwa ndio
ameisikia kwa mara ya kwanza, na kutaka kumafahamu mwananchi aliyetamka hayo ili
aweze kuongea mbele yake.
Aliwataka wananchi
kufika katika ofisi yake kueleza iwapo wanakumbwa na changamoto kama hizo na
sio kuishia kulalamika wakiwa wenyewe bila kupata ufafanuzi kwa wahusika.
No comments:
Post a Comment