Sunday, November 6, 2016

Ndanda FC wamaliza mzunguko wa kwanza VPL kwa kishindo


Wachezaji wa Ndanda FC, Nahodha Kigi Makassy, Riphati Khamis na Ahmad Msumi wakishangilia bao la kwanza lililofungwa kwa Penalti na Riphati Khamisi katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Stand United katika uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara. Ndanda walishinda bao 2-1.



Kiungo wa Ndanda FC na nahodha Kigi Makassy akimiliki mpira mbele ya mlinzi wa Stand United Lulambo Aron, katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara katika uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara. Ndanda walishinda bao 2-1.


Kiungo wa Ndanda Ahmad Msumi akiambaa na mpira kuelekea langoni mwa Stand United, katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara katika uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara. Ndanda walishinda bao 2-1.

 
Juma Mohamed, Juma News

Ndanda FC ya mkoani hapa imefanikiwa kumaliza vizuri mzunguko wa kwanza wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya hii leo kusambaratisha Stand United ya Shinyanga kwa mabao 2-1 katika uwanja wa Nangwanda Sijaona.
Mabao ya Ndanda yamefungwa kipindi cha kwanza na Riphati Khamis kwa mkwaju wa penalty dakika ya 30 baada ya kufanyiwa madhambi katika eneo la hatari na golikipa wa Stand Muwonge Frank, huku Ahmad Msumi akifunga la pili kwa kichwa akiunganisha kona ya Kigi Makassy dakika 45.

Wachezaji wa Ndanda FC walivyofunga bao la pili langoni mwa Stand United, katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara katika uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara. Ndanda walishinda bao 2-1.



Stand walipata bao la kufutia machozi kipindi cha pili baada ya mlinzi wa Ndanda Bakari Mtama kuusindikiza wavuni mpira uliopigwa na Khamis Frank wa Stand.
Ndanda wanamaliza mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo wakiwa wamejikusanyia jumla ya alama 19 baada ya mchezo huo, huku Stand United wakiwa na alama 22.

Kikosi cha Ndanda FC kilichoanza katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Stand United katika uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara. Ndanda walishinda bao 2-1.


Kikosi cha Stand United kilichoanza katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Ndanda FC katika uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara. Ndanda walishinda bao 2-1.



No comments: