Na Juma
Mohamed, Mtwara.
WANANCHI wa
manispaa ya Mtwara Mikindani wamehamasika kwa kiasi kikubwa na kujitokeza
katika program maalumu ya kuwaendeleza kielimu iliyoanzishwa na mbunge wa jimbo
la Mtwara mjini (CUF) Maftaha Nachuma, kwa lengo la kuinua kiwango cha elimu
kwa wananchi hao ambao wanalalamikia ukosefu wa ajira.
Wakizungumza wakati wa kujiandikisha kwa ajili
ya kuanza masomo programu hiyo inayofahamika kama Maftaha English Leaning
Program, baadhi yao walisema wameshawishika kujiunga kwasababu wanaamini
ukosefu wa ajira wanaokabiliana nao kwa sasa ni kutokana na kutokuwa na elimu
ya kutosha ikiwa ni pamoja na kutojua lugha ya kiingereza.
Walisema,
miongoni mwa changamoto wanazokabiliana nazo kutokana na kukosa elimu ni kuaibika
wanapotembea katika sehemu mbalimbali hapa nchini kwa kuambiwa wakazi wa Mtwara
hawana elimu, huku wengine wakidai kuwa hali hiyo inachangia umasikini kwa
baadhi yao.
“Kwakweli
hamasa ambayo imenifanya mimi kuja mahali hapa kwanza nikiangalia sikuizi ni
tofauti na zamani, sasahivi utandawazi ni mwingi, yani nikiangalia huu ni mwaka
2016 sasa mpaka kufikia 2020 kwa sisi ambao hatujui hii lugha ya kiingereza yani
tutakuwa tupo chini na ukiangalia huu mkoa wetu sasahivi ajira zipo nyingi,
tukishazembea kusoma itaonekana hata wabaki kutoka huko nchi za nje watakuja
kupata ajira..” alisema Zuhura Abeid.
Naye,
Ahmadani Nahembe, ambaye anashughulika na sanaa za maigizo, alisema suala la
kutojua lugha ya kiingereza limekuwa ni changamoto kubwa kwake kutokana na
kukosa kazi anapotakiwa kufanyiwa usaili kwa lugha hiyo ambayo ndio itakayoanza
kufundishwa katika program hiyo kwa muda wa miezi sita kabla ya kuanza masomo
ya elimu ya sekondari.
Kwa upande
wake, mbunge huyo alisema alibaini kuwepo kwa changamoto hiyo kutokana na
kuzunguka katika ofisi na kampuni mbalimbali za serikali na watu binafsi ambapo
aligundua kuwa kuna uhaba wa wananchi wa Kusini walioajiriwa katika ofisi hizo
huku alipouliza sababu za uhaba wao alijibiwa kuwa wananchi wengi hawana elimu.
“Kwahiyi
nikaona kwamba kuna haja ya kuwatangazia Wanamtwara, niazishe hii program
maalumu, kwanza waweze kujua kiingereza na ndio maana tumesema wasome kwa miezi
mitatu kwanza ‘then’ wafanye mtihani wasome tena miezi mitatu mingine wafanye
mtihani kwa maana kwamba ni miezi sita, ‘then’ tuaanze masomo ya sekondari kwasababu
masomo ya sekondari yanafundishwa kwa lugha ya kiingereza kwahiyo tukaona ni
vema wanafunzi wakajua kiingereza kwanza ili watakapojisomea vitabu vya
kiingereza waweze kufahamu kile kilichoandikwa..” alisema Maftaha.
Alisema,
amefurahishwa na muitikio wa watu ambao ni zaidi ya 500 walijitokeza
kujiandikisha huku akiwataka wananchi hao wazidi kujituma ili waweze kufikia
malengo kwasababu kusoma hakuna umri, ambapo alisema mpango huo anaugharamia
mwenyewe kupitia mshahara wake na tayari walimu wameshapatikana kwa ajili ya
kuanza kufundisha.
No comments:
Post a Comment