Na Juma
Mohamed.
IDARA ya
Uhamiaji mkoani hapa inamshikilia meneja wa kiwanda cha Saruji cha Dangote,
Vidya Sagar Dxit kutokana na kubainika kwa uwepo wa raia wengi wa kigeni wanaofanya
kazi kiwandani hapo bila kuwa na vibali vya kuwaruhusu kufanya kazi hapa
nchini.
Akizungumza
na waandishi wa habari ofisini kwake, Afisa Uhamiaji mkoa wa Mtwara, Naibu
kamishna, Zakayo Mchele, alisema hata hivyo meneja huyo hakutoa ushirikiano kwa
maofisa wa uhamiaji walikwenda kiwandani hapo kwa ajili ya kutekeleza majukumu
yao ya kazi kiasi cha kuwazuia kuingia ndani ya kiwanda hicho.
Alisema
lengo la maafisa hao kutaka kuingia kiwandani humo ni kutaka kufanya ukaguzi
kwa raia hao kutoka nchini China ambao jumla yao ni 360 kutokana na baadhi yao
kudai kuwa waliwasilisha maombi yao ya vibali katika makao makuu ya Idara hiyo
jambo ambalo alisema halina uhakika na juhudi zinafanyika ili kuweza kubaini
ukweli.
“Wengine
walibainisha kwamba maombi yalikuwa ‘submitted’ wengine hawana ‘details’ zozote
kwasababu tulikosa ushirikiano kwa uongozi maana tulitaka kuhakiki mmoja baada
ya mmoja na tulipeleka maafisa wengi kukagua mtu paspoti zake lakini hatukupata
ushirikiano kwa ‘general manager’ na ikabidi tumkamate tulimleta hapa kusaidia
Idara ya Uhamiaji na tutamfikisha mahakani kwa makosa ambaye ameyafanya.”
Alisema.
Alisema
zoezi la kufanya msako kwa wahamiaji haramu au raia wanaoishi nchini kinyume na
taratibu ni utekelezaji wa agizo la Naibu waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mhe.
Hamad Yussuf Masauni, na kwamba raia hao wengi wao wapo kiwandani hapo kwa muda
wa miaezi mitatu hadi minne.
Alisema
zoezi ni endelevu ambapo lilianza katika baadhi ya maeneo mkoani hapa ikiwa ni
pamoja na mpakani mwa Tanzania na Msumbiji katika kijiji cha Kirambo na
wilayani Tandahimba ambako huko waliweza kuwakamata raia 48 ambao walidai kuwa
walisafirishwa kwa malori kutokea nchini Kenya.
“Na
tulikamata raia wawili wa Msumbiji ambao walikuwa na hati za kupigia kura na
hao tuliwandoa maeneo ya Mtambaswala..tunaendelea na uchunguzi wa makampuni
mbalimbali ‘in facts’ ni zoezi endelevu na tulianzia Mikindani, tulienda kwenye
kampuni ya Trade Aid ambao tuligundua kwamba wote wanaishi kihalali kuna raia
wawili wa Uingereza ambao tuligundua wana vibali halali..” alisema na kuongeza:
“Hii misako
pia tunashiriksha wananchi, kwasababu wanaishi katika maeneo yale na wana ‘very
interagency information’ ambazo zinasaidia katika idara ya utendaji wa kazi..hapa
mkoani tuna maafisa 45 ambao ni maafisa wachache ambao hawawezi kufika maeneo
yote, lakini tunategemea wananchi na vyombo vya ulinzi na usalama, jeshi la
wananchi na watu wa usalama.” Aliongeza.
No comments:
Post a Comment