Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara, Alfred Luanda, akifungua Kikao cha Uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka 2016, katika ukumbi wa Montesori-Mtwara |
Na Juma
Mohamed
SERIKALI
mkoani hapa imesema itawakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wazazi
na walezi watakaobainika kutowaandikisha watoto wao kujiunga na elimu ya
sekondari, kwani hawana kisingizio kutokana na elimu kutolewa bure kwanzia
darasa la kwanza hadi kidato cha nne.
Akizungumza
katika kikao cha uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga na kidato cha kwanza mwaka
2016, katibu tawala wa mkoa wa Mtwara, Alfred Luanda, aliwaagiza viongozi wa
idara mbalimbali za elimu katika halmashauri ikiwa ni pamoja na maafisa elimu
na wakurugenzi, kuhakikisha kila mototo aliyechaguliwa kujiunga na kidato cha
kwanza naripoti shuleni katika tarehe husika.
Pia alionya baadhi
ya wazazi kuwaachisha masomo watoto wao hasa wakike kwa ajili ya kuwapeleka
Jando na Unyago kisha kuwaozesha, ambapo amewataka viongozi wa ngazi husika
kulidhibiti suala hilo na kuwachukulia hatua watakaobainika.
“Lakini kuna
tabia ya watu kuwachukua watoto wao kwa ajili ya kuwacheza ngoma na kuwaoza
wakiwa bado wadogo hasa watoto wakike, kuwaachisha shule mapema, tunaomba tutoe
onyo kama serikali, hiyo tabia kwakweli haikubaliki..tunaomba viongozi mkienda
mkafuatilie, mototo amechaguliwa kidato cha kwanza na hajaripoti hatua
zichukuliwe, mzazi achukuliwe hatua aseme Yule mototo amempeleka wapi..”
alisema.
Alisema,
wapo baadhi ya wazazi ambao wanakatisha masomo kwa watoto wao kwa makusudi kwa
lengo la kutaka wawasaidie katika shughuli zao za kilimo na wengine
kuwashinikiza waingie katika shughuli za ujaasiliamali, jambo ambalo ameliita
ni hujuma kwa watoto hao na ni vitendo ambavyo havikubaliki.
Awali
akiwasilisha taarifa ya uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga na kidato cha
kwanza mwaka 2016, afisa elimu wa mkoa, Fatuma Kilimia, alisema katika mwaka
2015 jumla ya wanafunzi 22,902 wakiwemo wavula 10,304 na wasichana 12,598
walifanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi, ambapo kati yao waliofaulu ni
15,670 wakiwemo wavulana 7,215 na wasichana 8,455.
“Ufaulu huo
ni sawa na asilimia 68.42, ufaulu wa mwaka huu ukilinganisha na ule wa mwaka
2014 umepanda, kwani mwaka 2014 ufaulu ulikua sawa na asilimia 62.0, hivyo mkoa
umepanda kwa asilimia 6.42..” alisema.
Licha ya
ufaulu kimkoa kuonekana kupanda kwa asilimia 6.42, mkoa wa Mtwara Kitaifa
umekuwa katika nafasi ya 12 na kuonekana kurudi nyuma kwa nafasi mbili kutoka
katika nafasi ya 10 mwaka 2014, huku halmashauri ya Mtwara vijijini ikifanya
vizuri na kuwa yakwanza kimkoa kwa kufaulisha kwa asilimia 86.84 na Kitaifa
kushika nafasi ya 16.
Kutokana na
takwimu hizo, halmasahuri hiyo imepanda ukilinganisha na takwimu za matokeo ya
mwaka 2014 ambapo ilifaulisha kwa asilimia 71 na kuwa yapili kimkoa na kitaifa
kuwa katika nafasi ya 31.
Halmashauri
ambazo zimeonekana kufanya vibaya katika mtihani huo ni za Masasi na Nanyumbu,
ambapo Masasi vijijini imefaulisha kwa asilimia 53.2 nakuwa katika nafasi ya
sita kimkoa na kitaifa kuwa nafasi ya 141, na kwamba ukilinganisha na ufaulu wa
mwaka 2014, imepanda kwa asilimia 0.2 kwasababu mwaka 2014 ilifaulisha kwa
asilimia 53.
Masasi miji
yenyewe imekuwa katika nafasi ya saba kimkoa na nafasi ya 142 kitaifa kutokana
na kufaulisha kwa asilimia 53.09, hivyo kurudi nyuma kwa nafasi mbili kutokana
na kuwa katika nafasi ya tano mwaka 2014.
Nanyumbu
ambayo imeshika nafasi ya tano kimkoa na nafasi ya 132 kwa kufaulisha kwa
asilimia 55.07, yenyewe imeshuka ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2014 ambapo
kimkoa ilikuwa nafasi ya 4 huku kitaifa ikiwa nafasi ya 77.
”Ufaulu
katika halmashauri zote umepanda, tatizo bado lipo Masasi (V) ambayo imebaki
palepale, Nanyumbu imerudi nyuma hatua 2.5 na Masasi mji imerudi hatua 2.9.
Tunazipongeza halmashauri zote kwa juhudi walizoziweka hadi kufanikiwa kuinua
taaluma..pongezi kubwa ni kwa halmashauri ya Mtwara kwa kuchukua nafasi ya 16
kitaifa na Mtwara Manispaa kwa kupanda kwa hatua 22.8 ikilinganishwa na mwaka
2014.” Aliongeza Kilimia.
Kufuatia
kufanya vibaya kwa halmasahuri hizo, katibu tawala alitoa onyo kwa maafisa
elimu na kuwataka kuhakikisha wanainua hali ya ufaulu katika mitihani ijayo, na
kama hali itaendelea kuwa hifyo hatua kali zitachukiliwa dhidi yao.
Aidha,
akitolea maelezo sababu za kufanya vibaya katika halmashauri yake, mkurugenzi
mtendaji wa halmashauri ya Nanyumbu, Idris Mtande, alisema sababu kubwa ni
wazazi kukosa muitikio mzuri kielimu na ukosefu wa vitendea kazi ikiwa ni
pamoja magari katika idara ya elimu.
No comments:
Post a Comment