Mlinda mlango namba moja wa timu ya Ndanda Sc,Nahodha, Wilbert Mweta, akizungumza na waandishi wa habari juu ya walivyojipanga kuelekea katika mchezo wao na Mgambo Shooting. |
Msemaji wa mashabiki wa Ndanda Sc, George Wena, akizungumza na waandishi wa habari. |
Na Juma
Mohamed.
MASHABIKI
wapatao 50 wa Ndanda Sc wanatarajiwa kuwasili mkoani Mtwara kesho wakitokea
jijini Dar es Salaam na kuungana na wenzao wa mkoani humo kwa ajili ya
kuishangilia timu hiyo siku ya Jumamosi itakapoteremka dimbani kuvaana na
Mgambo Shooting ya Tanga, katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara.
Akizungumza na
East Africa Radio, msemaji wa mashabiki wa Ndanda mkoani humo, George Wena,
amesema wanatarajia kuwapokea wenzao katika kijiji cha Hiyari, ambapo wanakuja
kwa ajili ya kuongeza nguvu katika ushangiliaji ili kufanikisha ushindi kwa
timu hiyo.
“Tunawaomba
wadau na wakazi wote wa mkoa wa Mtwara, tunaomba waisapoti timu yetu kwasababi
ni timu ambayo tunaitegemea kutupatia burudani katika mkoa wetu..na tujitolee
kuhusu timu ili matatizo madogomadogo tuyamalize sisi wenyewe, na tusichanganye
na mambomengine ya kisiasa..” alisema.
Alisema,
wamejipanga vizuri kushangilia katika mchezo huo utakaopigwa katika uwanja wa
Nangwana Sijaona, na wanaimani kubwa na timu yao kuibuka na ushindi hapo kesho
kutokana na usajili uliofanywa chini ya kocha mkuu, Hamimu Mawazo.
Aidha, kocha
Hamimu Mawazo alisema, kitu kikubwa kinachompa matumaini ya kuibuka na ushindi
katika mchezo huo ni kuimarika katika idara zote, zaidi katika safu ya ulinzi na
ushambuliaji ambazo msimu uliopita ndio zilikua na tatizo kubwa kiasi cha
kuchangia kupata matokeo mabovu.
Alisema timu
ikiwa na safu imara ya ulinzi inasaidia kuto ruhusu idadi kubwa ya magoli na
kutoa nafasi kubwa kwa washambuliaji kupata morali ya kufumania nyavu za timu
pinzani.
“Mwaka huu
tunabahati kwamba maeneo yale yamepta marekebisho mazuri kwenye timu, ninaamini
tutakuwa na timu nzuri ambayo itakuwa na uwezo wa kufunga na ninaamini ninamabeki
wazuri wenye uwezo wa kuzuia kwenye upande wetu wa timu ya Ndanda..kwahiyo hayo
mawili yakifanikiwa tutapata ushindi, na mimi naamini kwasababu wachezaji ambao
wana uwezo wa kutuletea ushindi kwenye hiyo mechi ya Jumamosi..” alisema
Mawazo.
Kocha mkuu wa timu ya Ndanda Sc, Hamimu Mawazo, akizungumza na
waandishi wa habari, juu ya namna alivyokiandaa kikosi chake kwa ajili
ya kuikabili Mgambo Shooting ya Tanga.
|
Alisema,
kuhusu changamoto zingine za nje ya uwanja wanazokumbana nazo wachezaji, amekaa
nao na kuzungumza nao ambapo wameonyesha kukubali na wote kuwa na lengo moja la
ushindi kuelekea katika mchezo huo ambao ni miongoni mwa michezo saba ya ligi
kuu itakayochezwa siku ya Jumamosi.
Kwa upande
wake, Nahodha wa timu hiyo, Wilbert Mweta, aliwataka wachezaji wenzake kucheza
kwa ushirikiano na kujituma zaidi huku wakifuata maelekezo ya mwalimu wao ili
kufanikisha hadhma yao ya kuondoka na poiti tatu katika mchezo huo.
“Wachezaji
wenyewe tujitume na tushirikiane uwanjani, tufuate maelekezo ya walimu wetu na
ninaamini tutayafuata kwasababu tumejiandaa muda mrefu..jambo lingine la msingi
ni kwamba mashabiki wetu wajitokeze waje kutusapoti kwasababu tupo katika
uwanja wetu wa nyumbani ili tupate hamasa kubwa..” alisema.
No comments:
Post a Comment