Friday, September 11, 2015

Habari njema kwa 'Fans' wa Man Utd..De Gea ajitia kitanzi hadi 2019

David De Gea

Juma Mohamed

HABARI njema kwa mashabiki wa Manchester United ni kwamba, mlinda mlango namba moja wa klabu hiyo raia wa Hispania, David De Gea, amesaini mkataba wa miaka minne wa kuendelea kukipiga Old Tafford mpaka mwaka 2019 ambao una kipengele cha kuongeza mwaka mmoja.
Taarifa zilizotolewa leo na mtandao wa klabu hiyo zinasema kuwa, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24, alijiunga na United mwaka 2011 ambapo amecheza kwa mafanikio michezo 174 na kunyakua ubingwa wa Uingereza mwaka 2013 kabla ya kutwaa tuzo mbili za mchezaji bora wa mwaka wa klabu hiyo (Sir Matt Busby­).
“Ninafuraha kuanza ukurasa mpya wa kuendelea kuitumkia United..nina ‘enjoy’ kucheza pamoja na wachezaji wenye viwango vikubwa tukiwa mbele ya mashabiki wetu. Man Utd ndio klabu pekee na Old Trafford ndio maali pekee kwangu kuendeleza kazi yangu..” alisema De Gea.
Na kuongeza “ninaamini utakuwa ni msimu mgumu lakini nitapambana kwa ajili ya kuisaidia timu kwa kusaidiana na wenzangu kufikia mafanikio..” aliongeza.
Kwa upande wake, kocha wa mashetani wekundu hao, Muholanzi, Luis Van Gaal, alisema “ninafuraha kusema David amesaini mkataba mpya. Huyu ni mmoja wa magolikipa bora duniani..nisema tu kwamba atakuwa sehemu ya timu yetu ka miaka mingine mingi tu” alisema.

Na kuongeza “David alikuwa na mchango mkubwa katika timu yetu msimu uliopita, na alikuwa mchezaji bora wa klabu kwa miaka miwili mfululizo..ni mchezaji maarufu ambaye anahitaji kujifunza zaidi na kutokana na kuwa na umri mdogo, ana nafasi kubwa ya kucheza michezo mingi zaidi..” aliongeza LVG.
SOURCE: MAN UTD.COM

No comments: