Idadi
ya wadau waliojitokeza kuchukua fomu za kuwania uongozi katika
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imeongezeka ambapo wengine
saba wamechukua leo (Januari 15 mwaka huu) na kufanya idadi yao kufikia
26.
Hata
hivyo, idadi hiyo ni kwa wale wanaochukua fomu hizo katika ofisi za
TFF, kwani vilevile zinapatikana kupitia tovuti ya TFF ya www.tff.or.tz ambapo mwisho wa kuchukua na kurejesha ni saa 10 kamili alasiri Januari 18 mwaka huu.
Waliochukua
leo ni Michael Wambura anayewania umakamu wa rais wakati kwa wajumbe wa
Kamati ya Utendaji ni Mbasha Matutu, Muhsin Balhabou, Salum Chama,
Titus Osoro na Zafarani Damoder.
Idadi
kamili ya waliochukua Michael Wambura, Ramadhan Nassib na Wallace Karia
(Makamu wa Rais). Kwa upande wa wajumbe na kanda zao kwenye mabano ni
Salum Chama (Kagera na Geita), Mugisha Galibona, Samuel Nyalla, Titus
Osoro na Vedastus Lufano (Mara na Mwanza).
Epaphra
Swai na Mbasha Matutu (Shinyanga na Simiyu), Charles Mugondo, Elly
Mbise na Twahili Njoki (Arusha na Manyara), Yusuph Kitumbo (Kigoma na
Tabora), Ayubu Nyaulingo, Nazarius Kilungeja na Selemani Kameya (Katavi
na Rukwa) na James Mhagama (Njombe na Ruvuma).
Athuman
Kambi (Lindi na Mtwara), Hussein Mwamba na Stewart Masima (Dodoma na
Singida), Farid Nahdi (Morogoro na Pwani), Khalid Mohamed (Kilimanjaro
na Tanga) na Muhsin Balhabou, Shaffih Dauda na Zafarani Damoder (Dar es
Salaam).
Naye Said Mohamed amechukua fomu ya kuwania umakamu mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu (TPL Board).
No comments:
Post a Comment