YANGA YAUA 4-0 DAR, KAVUMBANGU AFUNGUA AKAUNTI YA MABAO JANGWANI
Yanga SC |
YANGA ya Dar
es Salaam imeifunga mabao 4-0 Moro United iliyoshuka Daraja msimu uliopita
kutoka Ligi Kuu, katika mchezo wa kirafiki kujiandaa na Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara, inayoanza Septemba 15, mwaka huu, uliofanyika kwenye Uwanja wa
Shule ya Msingi Kijitonyama, Dar es Salaam.
Kavumbangu,
amefungua akaunti ya mabao Yanga leo |
Kocha wa
Yanga, Tom Saintfiet raia wa Ubelgiji alitaka mechi moja dhidi ya timu
inayocheza kama wapinzani wao wa kwanza katika Ligi Kuu, Prisons na pia katika
Uwanja mbaya kama ambao atachezea mechi ya kwanza ya ligi hiyo, Sokoine mjini
Mbeya na ndiyo maana timu hiyo imecheza mechi hiyo leo kwenye Uwanja
huo.
Saintfiet
ameridhika na kiwango cha timu na sasa anasema timu iko tayari kwa Ligi Kuu,
akianza na Prisons iliyorejea Ligi Kuu msimu huu kwenye Uwanja wa Sokoine,
Septemba 15.
Hiyo inakuwa
mechi ya 11, Saintfiet anashinda Yanga katika mechi 12 tangu ajiunge nayo miezi
miwili iliyopita.
REKODI YA
SAINTFIET YANGA
1.
Yanga Vs JKT
Ruvu 2-0
2.
Yanga Vs
Atletico (Burundi) 0-2
3.
Yanga Vs Waw
Salam (Sudan Kusini) 7-1
4.
Yanga Vs APR
(Rwanda) 2-0
5.
Yanga Vs
Mafunzo (Z’bar) 1-1 (5-3penalti)
6.
Yanga Vs APR
(Rwanda) 1-0
7.
Yanga Vs Azam
2-0
8.
Yanga Vs
African Lyon 4-0
9.
Yanga Vs Rayon
(Rwanda) 2-0
10.
Yanga Vs
Polisi (Rwanda) 2-1
11.
Yanga Vs
Coastal Union 2-1
12.
Yanga Vs Moro United 4-0
SOURCE:BIN ZUBEIRY
No comments:
Post a Comment