Monday, June 18, 2012

DITTO, LINEX NA MWASITI WAPAWISHA EBSS WAKAWAKA PARTY

 

Linex Sunday Mjeda akifanya vitu vyake kwenye ukumbi wa Royal Village katika EBBS Wakawaka Party

Ikafika zamu ya soldier Mwasiti kusababisha kwenye jukwaa la Epiq BSS Wakawaka Party, alifunika hatari.

Ditto aliwakilisha vizuri nae kwa kupiga show kali iliyoleta hisia kubwa miongoni mwa waudhuruiaji wa Wakawaka Party.

WAZIRI AKITOA BURUDANI KWENYE WAKAWAKA PARTY

WILLIAM PINGO WA ZANTEL, DITTO, MHE. JANUARY MAKAMBA, AWAICHI MAWALLA WA ZANTEL NA IBRAHIM ATTAS WA ZANTEL WAKIPATA GROUP PICTURE NA MHE. JANUARY MAKAMBA

MWASITI, DITTO AND LINEX AT CLUB 84


KAZI NA DAWA: VIDEO MPYA YA MSANII AY YATOKA.

VIDEO YA WIMBO PARTY ZONE WA MSANII AY AKIMSHIRIKISHA MARCO CHALI.

ITALY VS IRELAND: KUMTEGEMEA SANA ANDREA PIRLO NI HATARI KWA ITALIA

Kuna suala la kubishana kidogo kwamba Andrea Pirlo alikuwa ndio kiungo bora wa ulaya msimu uliopita. Alisajiliwa na Juventus na kuisadia kushinda taji la kwanza la serie A tangu ilipotokea skendo ya Calciopoli ya mwaka 2006; chini ya Pirlo Juventus walimaliza msimu bila kufungwa kwenye ligi, na Andrea Pirlo aliifanya bibi kizee wa Turin kutisha tena.

Utulivu na uvumilivu wa Pirlo akiwa na mpira ulikuwa hauna mfano mwingine kwenye bara la ulaya, na akiwa anaelekea kwenye Euro 2012, alikuwa kwenye kiwango cha maisha yake.



MIDFIELD MAESTRO
PIRLO'S STATS VS SPAIN
PASSES MADE
LONG PASSES
SHORT PASSES
PASSING ACCURACY
GOALS
ASSISTS

39
9
30
82.1%
0
1
PIRLO'S STATS VS CROATIA
PASSES MADE
LONG PASSES
SHORT PASSES
PASSING ACCURACY
GOALS
ASSISTS

67
11
56
82.1%
1
0


Akiwa na miaka 33, kiungo mchezeshaji huyo hakutegemewa kucheza kwa kiwango kizuri kwenye msimu wa 201-12. Aliachwa na AC Milan kwa kuwa na umri mkubwa, lakini chini ya uongozi wa Antonio Conte, akaweza kuwa mhimili mkuu wa timu hasa kwenye eno la kiiungo.

Kiwango chake kikubwa kiliwafanya Italia waende kwenye michuano ya Euro nchini Poland na Ukraine wakiwa kwenye hali ya matumaini. Kama ilivyo Juve, kocha Cesare Prandelli amemfanya Pirlo ndio nguzo ya timu yake; huku akicheza pembeni ya Claudio Marchisio na Thiago Motta kwenye kiungo, ilionekana kwamba Azzuri wangepita kwenye hatua ya makundi bila wasiwasi wowote.

Baada ya mechi ya kwanza dhidi ya Spain, ambayo Italy walionekana kucheza vizuri. Walipata suluhu ya kuipigani sana ya 1-1 dhidi ya mabingwa watetezi. Azzuiri walionekana kuwa vizuri kwenye ulinzi, mawinga na ushambuliaji wa mtu kama Di Natale mwenye uwezo wa kufunga mabao muhimu, lakini kubwa kuliko ilikuwa na kiwango cha Pirlo aliyecheza dhidi ya midfield maestros Xavi na Iniesta.

"Mchezaji aliyeleta tofauti kubwa ni Pirlo," Fabio Capello aliiambia UEFA.com. "Kila mara alipoanzisha shambulizi, lilikuwa ni shambulizi la hatari kwa wapinzani Spain."

Corriere dello Sport lilisema kwenye gazeti la asubuhi ya siku iliyofuatia "Beautiful Italy". Lakini gazeti hilo halikuendeleza sifa hizo siku nne baadae, likaandika, "Sare & Shida" kama kichwa cha habari baada ya vijana wa Prandelli kutoka suluhu na Croatia katika mechi ya pili ya kundi C.

Italy walihangaika na kucheza hovyo, hasa kwenye kipindi cha pili, wakipewa presha kubwa na kikosi cha Bilic, na hatimaye wakaruhusu goli la kusawazisha kwa Croatia likifungwa na Mandzukic. Pirlo alitulizwa hasa kwenye dakika 45 za kipindi cha pili, na matokeo yake timu ya Italia ikaonekana imevunjika vipande vipande.

Imekuwa hali kma inayoitokea Portugal kumtgemea sana Ronaldo, Pirlo asipokuwa kwenye kiwango kizuri basi na Italia inapotea kabisa.

Akiwa ndio tishio pekee kwenye creative department, Pirlo alikuwa ndio target kwa vijana wa Slaven Bilic. Alikabwa vilivyo na viungo wa Croatia chini Ognjen Vukojevic, na hivyo kupelekea kushindwa kucheza vizuri.

Suluhisho pekee kwa Prandelli, ni kuongeza kiungo mwingine mbunifu kwenye safu ya kiungo, Thiago Motta, akiwa mzuri jinsi alivyo lakini sio mchezeshaji mzuri sana kwa mchezo wa kushambulia, hivyo kwenye mechi dhidi ya Ireland, haihatajiki sana. Kwa maana hiyo itabidi Antonio Nocerino aanze kwenye kikosi cha kwanza badala ya Motta. Nocerino ni ni kiungo wa aina ya Box to Box, kiungo ambaye Italy wanahitaji dhidi ya wachezaji aiana ya Keith Andrews na Paul Green, kwa hakika atakuwa mbadla sahihi.

Ikiwa Italy wataendelea mbele kwenye michuano hii itabidi wachezaji wengine waongeze kasi kwenye viwango vyao na kujituma zaidi, na sio kumuachia kiungo mwenye umri wa miaka 33, Pirlo, kubeba mzigo wa taifa kwenye mabega yake.

HIVI NDIVYO MAMBO YALIVYOKUWA MSUMBIJI WALIPOITOA TAIFA STARS

Umati wa mashabiki wa Msumbiji wakiwa uwanjani kuisapoti timu yao

Haruna Moshi Boban , Mrisho Ngassa, Nurdin Bakary na wachezaji wengine wa Tanzania wakiwa kwenye benchi.


Shoamri Kapombe akipambana dimbani kumtoka beki wa Msumbiji

Frank Domayo na Shomari Kapombe wakipata maelekezo kutoka kwa kocha Kim Poulsen


Baadhi ya mashabiki wa kitanzania wakiisapoti timu kwenye mchezo wa jana

Mrisho Khalfan Ngassa akiwapeleka puta mabeki wa Msumbiji

Mbwana Samatta akijaribu kumtoka beki wa Msumbiji



MAXIMO ALONGA KUHUSU YANGA



* Akiri pia kupata ofa nono Ethiopia na Rwanda
* Yanga wasisitiza atawasili badaye mwezi huu



ALIYEKUWA Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Mbrazil Marcio Maximo akiri kuwa ni kweli yupo katika mazungumzo na klabu ya Yanga ila bado hawajakubaliana siku ya kuja na si rahisi kama wanavyodhani.

Maximo kwa sasa anafundisha kwa mafanikio makubwa klabu ya Democrata F.C ya Mjini Rio de Jeneiro Brazil.

Maximo aliondoka nchini baada ya mkataba wake kumalizika Agosti mwaka 2009 ambapo Shirikisho la soka nchini TFF lilishindwa kumuongezea mkataba kwa kutoridhishwa na utendaji wake na nafasi yake kuchukuliwa na Mdenmark Jan Poulsen ambae pia alishindwa kuitoa Tanzania kimasomaso.

Akizungumza na Dimba kwa njia ya mtandao Maximo alisema bado yupo katika mkataba na klabu yake hivyo si rahisi yeye kukurupuka na kuondoka ni lazima afuate mkataba unavyosema.

“Ni kweli nipo katika mawasiliano na Yanga lakini tupo katika mazungumzo kwani nina mkataba na klabu ya Democrata si rahisi mimi kuja huko kwa sasa bila kufuata taratibu, hata hivyo hadi sasa hatujapanga na Yanga tarehe ya kuja huko, nashangaa kusikia kuwa watu wanasubiria kuwasili kwangu.

“Mimi naheshimu sana mkataba na kama kuja ni lazima nifuate taratibu kwanza na si kukurupuka, si rahisi labda wasiwe wanajua nini maana ya mkataba, sijapangiwa na wala tiketi sina kwa kuwa hatujafikia huko,” alisema Maximo.

Maximo alieleza kuwa amefurahishwa na nia ya Yanga kumtaka na kama wataafikiana basi hana budi kuja kujiunga nao kwa ajili ya kuifundisha timu.

Alisema anaifatilia kwa makini ishu ya Yanga kwasababu anaona wakurugenzi wa Yanga wana nia thabiti ya kuendeleza klabu hiyo hivyo hataki kuwaangusha.

Kocha huyo ambae alileta hamasa kwa timu ya Taifa na kuifanya ipendwe na iwe gumzo katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, amepata mawasiliano mengine toka kwa timu ya St. George ya Ethiopia na timu za Taifa za Zimbabwe na Rwanda ambayo ipo chini ya kocha Milutin Sredojevic ‘Micho’

Hata hvyo klabu ya Yanga jana ilijulisha umma kuwa Maximo alietarajiwa kufika jana sasa atawasili nchini mwishoni mwa wiki hii kitu ambacho Maximo hakijui.

Katika taarifa ya Yanga jana, ilieleza kuwa Maximo tayari amekwishatumiwa tiketi ya safari ya kuja hapa nchini na ameshindwa kuwasili jana kutokana na Klabu yake anayofundisha ya Democrata kukabiliwa na mchezo mgumu siku ya Jumamosi wiki hii kitu ambacho hakina ukweli.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa Marcio mara baada ya kuwasili nchini atafanya mazungumzo na Uongozi wa Klabu ya Yanga ikiwemo kusaini Mkataba na Klabu ya Yanga kabla ya kuanza kazi ya kukinoa kikosi hicho.

Kocha huyo kabla ya kuondoka nchini Brazil amewaahidi Wanachama na Wapenzi wa Klabu ya Yanga kuwa atafanya jitihada za kukiimarisha kikosi cha Mabingwa wa Soka wa Afrika Mashariki na Kati katika kuinua vipaji mbalimbali kupitia soka la Vijana wenye umri mdogo kwa ajili ya kupata wachezaji Bora.
Ilieleza ambo mengine aliyoyapanga Kocha huyo ni pamoja na kuimarisha nidhamu kwa Wachezaji atakaokuwa akiwafundisha na mara baada ya kuanza kibarua chake cha kukinoa kikosi hicho atakuwa na mtihani wa kwanza kwa kukabiliwa na michuano ya Kombe la Kagame inayotarajiwa kuanza Julai 23 hadi Agosti 7 Mwaka huu.

Stori hii imeandaliwa na Mwani Nyangasa.

SD TV: PENALTI ZILIZOITOA TANZANIA DHIDI YA MSUMBIJI


SD TV: MABAO TAIFA STARS VS MSUMBIJI.


Sunday, June 17, 2012

USAHILI WA EPIQ BONGO STAR SEARCH WAMALIZIKA MKOANI DODOMA.


Kundi la akina dada wakitabasamu na kupiga pozi kabla ya kuingia kwa majaji


Awaichi Mawalla wa Zantel akichangia damu akiwa na mtu wa damu salama
Kundi la washiriki wa EBSS wakipiga pozi kabla ya kwenda kuonana na majaji
Mshiriki wa EBSS akiimba na kupiga guitar kwa nguvu zake zote ili majaji wamkubali na apate fursa ya kuwakilisha Dodoma
Mshiriki wa EBSS akiimba kwa nguvu ake zote ili majaji wamkubali

KIFUKWE NA MANJI SI WADHAMINI HALALI WA YANGA!

Mwananchama wa Yanga bwana Abeid.A. Abeid ameibuka na kuwekea pingamizi uchaguzi wa klabu ya Yanga kwa kile anachodai katiba iliyotumiwa na wagombea si halali.
Bwana Abeid amabye aliwahi kuwa mweka hazina wa Yanga siku za nyuma pia amedai ndugu Yusuf Manji na ndugu Francis Kifukwe si wadhamini halali wa Yanga.

RONALDO AWANYAMAZISHA WABAYA WAKE: APIGA MBILI URENO IKIENDELEZA UBABE KWA WAHOLANZI NA KUWATOA EURO


Portugal 2-1 Holland (Euro 2012 - Group B) All... by fasthighlights-2012

UJERUMANI KUWAVAA UGIRIKI WASIOTABIRIKA KWENYE ROBO FAINALI YA EURO


Denmark 1-2 Germany (Euro 2012 - Group B) by fasthighlights-2012

No comments: