Wednesday, March 28, 2012

TORRES APIGA BAO LA USHINDI DAKIKA YA MWISHO


Mchezaji wa Panama, Anibal Godoy (20) akimkaba Erick Torres (15) wa Mexico mfungaji wa bao pekee kwenye mechi hiyo ya CONCACAF kuwania kucheza Olimpiki. Mexico ilishinda 1-0.
BAO la Erick Torres dakika moja kabla ya filimbi ya mwisho, liliiwezesha Mexico kuifunga Panama 1-0 jana na kuongoza kundi lake katika mechi za kuwania kufuzu kucheza michuano ya Olimpiki Jijini London, mwaka huu.
Timu zote za fainali, zitaiwakilisha Amerika Kaskazini, Kati na Caribbean katika michezo hiyo ya London.
Kufuatia ushindi mfululizo kwenye kundi lake, kocha Luis Fernando Tena aliwapumzisha mastaa wake Marco Fabian na Alan Pulido.

No comments: