Baadhi ya wakazi wa kata ya Ziwani, wakisubiri kupatiwa fedha za kujikimu zinazotolewa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kupitia mpango wa kunusuru kaya masikini. |
Mnufaika wa TASAF akitoka kupatiwa fedha kutoka kwa wawezeshaji. |
Mmoja wa wazee wa kijiji cha Nambeleketela, kata ya Ziwani halmashauri ya wilaya ya Mtwara, akipokea fedha za kujikimu kutoka kwa wawezeshaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) |
Na Juma Mohamed, Mtwara.
Wananchi wa
kijiji cha Nambeleketela tarafa ya Ziwani, halmashauri ya wilaya ya Mtwara,
wamefanikiwa kuanzisha miradi ya ufugaji na kuwatimizia mahitaji ya shule
watoto wao kutokana na kupatiwa fedha za msaada kupitia mpango wa TASAF wa
kunusuru kaya masikini.
Wakizungumza
kijijini hapo wakati wa kupokea fedha hizo, walisema mpango huo umesaidia kwa
kiasi kikubwa kuokoa hali ngumu ya maisha ambayo walikuwa wakikabiliana nayo
huku wengine wakiiomba serikali kuzidi kuuboresha na kuongeza muda zaidi.
“Kwavile
msaada huu ninaoupata unanisaidia, unanisaidia kwasababu kwamba sioni alafu mahala
kama nilikuwa na nyumba yangu mbaya mbaya mungu amenijaalia upande mmoja
nimepata mtu wa kunijengea lakini upande mwingine sijamaliza..naiomba wazidishe
msaada..” alisema Hassan Makini, mkazi wa Nambeleketele.
Baadhi ya wakazi wa kata ya Ziwani, wanaotoka katika kaya masikini wakipatiwa fedha kutoka katika Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) |
Naye, Hashim
Meshetwe ambaye alimwakilisha mama yake alisema, tayari mzazi wake huyo
ameanzisha mradi wa kufuga kuku lakini kabla ya kupata mgao huo alikuwa katika
hali mbaya ya kifedha kwahiyo aliwashukuru wawezeshaji kwakua fedha hizo
zimesaidia kutatua baadhi ya mahitaji muhimu katika kipindi hiki cha mfungo wa
Radhamn.
Mwenyekiti
wa kijiji hicho Mahamudu Ally, aliishukuru serikali kupitia mpango huo ambao
unaelekea kufikia mwisho kwa kuweza kuwakomboa wananchi wake, huku mwezeshaji
wa mpango huo Agatha Tembo, amewataka wanufaika na mpango huo kutumia fedha
wanazozipata katika kuwekeza katika mitaji itakayowasaidia baadae pale mpango
huo utakapofikia mwisho.
Jumla ya
kaya 121 zimepata mgao wa fedha hizo katika kijiji hicho kupitia mpango huo
ambao unatekelezwa kwa miaka mitano kwa kila awamu.
No comments:
Post a Comment