Na Juma Mohamed, Mtwara.
Chama cha
Waandishi wa Habari mkoani humo (MTPC), kimemuomba katibu mkuu wa wizara ya
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Gabriel, kuwashinikiza
waajiri kuwapatia mikataba waandishi wa mikoani ili kulinda masilahi yao na
kutatua baadhi ya changamoto za kimkataba wanazokabiliana nazo.
Akizungumza katika
ofisi ya chama hicho ambako katibu mkuu alitembelea kwa ajili ya kusikiliza
maoni na changamoto za wanahabari ikiwa ni sehemu ya ziara yake, mwenyekiti wa
chama hicho Hassan Simba, alisema changamoto nyingine walizomweleza ni pamoja
na waandishi kutokuwa na vitambulisho maalumu (Press Card) kutoka wizara ya
habari vitakavyowawezesha kufanya kazi zao mahala popote nchini.
“Kwanza ni
suala la mikataba kwa wafanyakazi wanaofanya kwenye vyombo mbalimbali, kwamba
hawa wawe na mikataba ambayo inaeleza wazi masialahi yao na mambo yao mengine
yanayotakiwa kufanywa pamoja na yale makato kwa ajili ya mifuko ya uzeeni..”
alisema na kuongeza;
“Lakini
jambo jingine tumeona hapa waandishi wetu wamekuwa wakifanya kazi bila kuwa na ‘Press
Card’ yani kile kitambulisho maalumu kinachotolewa na wizara ya habari kwa
ajili ya kufanya kazi popote Tanzania” aliongeza Simba.
Elisante Gabriel na Hassan Simba |
Hata hivyo,
Simba hakusita kutoa shukrani zake kwa niaba ya chama hicho kufuatia
kukabidhiwa iPad moja ambayo itasaidia katika mawasiliano baina ya chama na
wizara juu ya masuala mbalimbali ya kiutendaji.
Kwa upende wake, katibu huyo aliahidi
kuyafanyia kazi maombi yaliyowasilishwa kwake pamoja na suala la ufadhili kwa
wanahabari wanaohitaji kwenda masomoni kuongeza taaluma zao.
“Kilichonifurahisha
kuliko vyote ni kitendo cha nyie kusema sio tu kwa vile wewe umesomea habari na
ujue tu kuandika..lakini nafikiri bado mungeweza kuandika kwa Mhe. Nape (Waziri
wa Habari, sanaa, utamaduni na michezo), na mimi nitamfikishia na maelezo ya
ziada, na nyinyi baada ya kupanda basi kupeleka Dar es Salaam mfikishieni
zawadi kwa kumtumia andiko leo (jana) ili kesho (leo) na mimi nikifika ofisini
nivione alafu tuweze kuvifanyia kazi..” alisema.
Katibu mkuu wa wizara ya habari, sanaa, utamaduni na michezo, Prof. Elisante Gabriel, akimsikiliza mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Mtwara (MTPC), Hassan Simba. |
Aidha,
alikabidhi iPad moja kwa uongozi wa MTPC ambayo itasaidia katika mawasiliano
baina ya MTPC na wizara juu ya masuala mbalimbali ya kiutendaji pale inapobidi.
Ziara ya
katibu mkuu huyo mkoani Mtwara ilikuwa na lengo la kuitoa wizara jijini Dar es
Salaam na kuipeleka mikoani kwa ajili ya kupata maoni na changamoto kutoka kwa
wadau.
Unaweza kushea na wengine habari hii..
No comments:
Post a Comment