Na Juma Mohamed
Timu ya taifa ya soka ya Ujerumani imewasili nchini humo kwa
kishindo wakiwa na kombe lao la ushindi walilolinyakua katika mashindano ya
kombe la dunia ambyo yalikamilika juzi nchini Brazil.
Maelfu ya mashabiki wa soka wamekuwa wakisubiri tangu asubuhi na mapema mjini
Berlin kuwakaribisha wachezaji hao.Watu wengi wamenunua jezi zenye nyota nne kuashiria ushindi wa nne wa nchi hiyo katika kombe la dunia.
Wachezaji wa timu hiyo ambao huchezea timu ya Bayern Munich pia watapata ukaribisho mkubwa baadaye mjni Munich.
Mwandishi wa BBC Steve Evans ambaye yuko mjini Berlin anasema kuwa watu nusu milioni wanatarajiwa kukutana na wachezaji hao mjini Berlin.
SOURCE: BBC
No comments:
Post a Comment