Monday, March 25, 2013

HOTUBA YA RAIS WA CHINA



Rais wa China Xi Jinping
Leo nafurahi sana kuona ukunjufu zaidi kwa kuweza kukutana na marafiki wote kwenye kituo cha kimataifa cha mikutano cha mwakalimu Nyerere cha Tanzania.
Katika miaka ya hivi karibuni, chini ya uongozi wa rais Kikwete, utulivu umedumu katika hali ya kisiasa nchini Tanzania, mambo ya ujenzi yanaendelea motomoto, yote hayo yamefanya kazi kubwa katika mambo ya Afrika na mambo ya kimataifa.
Wananchi wa China na Afrika wameunda hisia za kindugu za kusaidiana na kufanya ushirikiano wa dhati.
Mpaka mwaka jana, vitega uchumi vilivyowekezwa moja kwa moja na China barani Afrika vimezidi dola za kimarekani bilioni 15.
Baada ya China kukumbwa na tetemeko kubwa la ardhi huko Wenchuan, nchi za Afrika zilitoa msaada kwa watu walioathirika.
Urafiki na ushirikiano kati ya wananchi wa China na wananchi wa Afrika, umekuwa alama ya uhusiano kati ya China na Afrika, ambao umesifiwa sana na jumuiya ya kimataifa.
Historia hii imetuambia kuwa, China na Afrika siku zote ni jumuia ya mustakabali wa pamoja.
Kila upande wetu siku zote una msimamo wazi na kuunga mkono upande mwingine bila kusitasita katika masuala yanayohusu maslahi makuu ya upande mwingine.
Historia hii imetuambia, tunapaswa kwenda na wakati wa kufanya uvumbuzi ili kufanya uhusiano kati ya China na Afrika uwe na nguvu kubwa ya uhai.
Kusukuma mbele ushirikiano wa China na afrika ni matumaini ya pamoja ya wananchi wa pande zotu mbili, huu unafuata mkondo wa duniani, na kuambatana na nia ya wananchi.
Maendeleo ya China hayataweza kudhoofisha uhusiano wake na Afrika, bali yataimarisha tu uhusiano wake na Afrika.
Tunawatendea marafiki wa Afrika kwa udhati. Marafiki wa dhati ni wenye thamani zaidi.
Pande mbalimbali zinapaswa kuheshimu ustaarabu wa aina mbalimbali duniani na njia mbalimbali za kujiendeleza.
Afrika ni bara la waafrika, nchi yoyote inayoendeleza uhusiano kati yake na Afrika inapaswa kuheshimu heshima ya Afrika na juhudi zake za kujiamulia.
China ikitoa ahadi zake, hakika itatekeleza kihalisi ahadi zake hizo.
Katika miaka mitatu ijayo China itazisaidia kuwaandaa watu elfu 30 wenye ujuzi wa aina mbalimbali, itatoa udhamini wa masomo kwa wanafunzi wa Afrika wapatao elfu 18.
China itaendelea kutoa msaada wa kustahiki kwa maendeleo ya Afrika bila masharti yoyote ya kisiasa.
Msingi na mizizi ya uhusiano kati ya China na Afrika iko kwa wananchi wa pande mbili.
Na tamthiliya ya China ya "Doudou na mama wakwe zake" inayooneshwa nchini Tanzania imewafanya watazamaji wa Tanzania wajihisi ladha za aina mbalimbali za maisha ya familia za raia wa China.
Tunapaswa kutilia maani zaidi mawasiliano ya utamaduni kati ya China na Afrika na kuongeza maelewano na ufahamu wa wanachi wa pande mbili.
China imejiunga na itaendelea kujiunga na nchi za Afrika, kuchukua hatua halisi za kushguhulikia vizuri matatizo yaliyoko kwenye ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya China na Afrika.
Daima China itazichukua nchi za Afrika kuwa marafiki zake wa dhati katika wakati wowote.
Maendeleo ya China hayawezekani kutengana na dunia na Afrika, na ustawi na utulivu wa dunia na Afrika pia unaihitaji China.
Wananchi wa China na Afrika wanatakiwa kuimarisha mshikamano na ushirikiano, ili kujitahidi kutimiza ndoto ya kila upande.
Tutajiunga na jumuiya ya kimataifa katika kuhimiza juhudi za kutimiza amani ya kudumu na ustawi wa pamoja, ili kutoa mchango mkubwa zaidi kwa ajili ya amani na maendeleo ya binadamu.

No comments: