
![]() |
Rais wa klabu ya Simba Evans Aveva (katikati) akikata utepe kuzindua duka la kuuza vifaa vya Simba lililopo Dar Free Market Mall Ground Floo |
Klabu ya Simba SC leo imeamua kufanya kweli baada ya kuzungumza mambo mengi ambayo mwisho wa siku yalikuwa yamebaki kwenye makaratasi. Simba leo wamezundua rasmi duka ambalo litakuwa linauza vitu mbalimabali vyenye nembo ya klabu hiyo kwa lengo la kutengeneza mkwanja.

Imekuwa muda mrefu sasa tangu vilabu hivyo viwili vya Simba na Yanga vilipoanza kupiga kelele za kuhakikisha bidhaa zenye nembo za klabu zao zinavinufaisha vilabu lakini bado wajanja waliendelea kufaidika kutokana na vilabu hivyo kushindwa kudhibiti watu ambao wamekuwa wakipiga pesa kwa kuuza bidhaa zenye nembo za vilabu hivyo.

Rais wa Simba Bw. Evans Aveva leo amezindua rasmi duka la Simba ambalo litakuwa likiuza vifaa vya michezo, jezi, kofia, T-shirts pamoja na vitu vingine vingi vyenye chapa ya Simba kwa ajili ya kujiingizia kipato kutokana na chapa ya timu yao.

Hiyo ni changamoto kwa vilabu vingine vya ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara ambavyo bado vimelala huku wajanja wa mjini wakiendelea kuponda pesa kutokana na kuuza bidhaa zenye nembo zao huku wao wakiwa hawapati hata shilingi 100.
SOURCE: shaffihdauda.co.tz
No comments:
Post a Comment