Kaimu mwalimu mkuu wa shule ya msingi Msangamkuu, Zaitun Mkamumba, akiwa mbele ya moja ya nyumba za walimu zilizopo katika shule yake. |
Moja ya nyumba ya walimu. |
Moja ya nyumba za walimu-shule ya msingi Msangamkuu |
Na Juma
Mohamed.
WALIMU wa
shule ya msingi Mkubiru, halmashauri ya Mtwara vijijini, wamelalamikia ugumu wa
maisha wanaoupata kutokana na kushindwa kumudu gharama za maisha ambazo haziendani
na kipato wanachokipata kwa mwezi, na kujikuta wanakabiliwa na madeni.
Wakizungumza
na Nipashe wiki iliyopita, walisema kuna mambo mengi ambayo yamekuwa ni
changamoto katika mazingira yao ya kazi, ikiwa ni pamoja na miundombinu mibovu
katika shule yao kiasi cha kuzidi kuyafanya maisha yao kuwa magumu.
Moja ya
changamoto ambazo walizieleza ni kukosekana kwa nyumba za walimu shuleni hapo
na kusababisha walimu wengi kuishi maeneo ya kijijini ambako wanalazimika
kupanga na kulipa kodi kila mwezi huku wakikabiliwa na changamoto nyingine ya
usafiri wa kutoka huko wanakoishi mpaka kufika shuleni kiasi cha kulazimika
kutumia pesa kwa ajili ya nauli ya pikipiki za kubeba abiria (Bodaboda).
“Hali ya
mshahara na maisha yalivyopanda haviendani, na hii ndio maana inasababisha
baadhi ya walimu kujihusisha na biashara labda zingewza kuwakwamua..mshahara
nalipwa sh. 350,000 na matumizi yangu kwa mwezi yanafika sh. 520,000, kwahiyo
mwisho wa mwezi najikuta nakabiliwa na madeni sana mpaka inafikia wakati
tunagombana na wenye nyumba maana kama majengo unavyoyaona hakuna nyumba za
waalimu sisi tuliokuwa wengi tunaishi mitaani kwa kupanga..” alisema mwalimu
mmoja ambaye jina lake limehifadhiwa.
Alisema,
kuna mahitaji ambayo analazimika kuyapata kila siku na yanahitaji pesa ikiwa ni
pamoja na kununua samaki wanaopatikana kwa sh. 5,000 ambao ndio mboga kubwa
kutokana na kijiji hicho kuwa katika mazingira karibu na bahari na mchele ambao
wananunua sh. 2,200.
“Mahitaji
mengine ambayo nalazimika kutumia pesa kila siku ni vocha kwa ajili ya
mawasiliano (Hakutaja anatumia kiasi gani) pamoja na viungo kama nyanya,
vitunguu na vingine, kwasababu samaki siwezi kupika bila viungo..” aliongeza.
Alisema,
kutokana na kubanwa katika majukumu yao ya kufundisha, wanajikuta wanakosa hata
muda wa kufanya shughuli nyingine ambazo labda zingeweza kuwapatia kipato
mbadala tofauti na mshahara wao, huku akisema kuwa mpaka sasa anakabiliwa na
deni la sh. 126,000.
Alisema,
toka ameanza kazi shuleni hapo mpaka sasa ni kama mwaka mmoja na miezi kadhaa
imepita na kwamba kitu ambacho anajivunia kuwa nacho ni kumiliki kiwanja
ambacho hata hivyo upatikanaji wake kwa kiasi kikubwa umechangiwa na ndugu zake
waliompatia pesa kiasi cha sh. Milioni 1.2 huku mwenyewe akitoa sh. 250,000.
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Mkubiru, halmashauri ya Mtwara vijijini, Hazam Nambunga, akielezea changamoto alizonazo shuleni kwake. |
Kwa upande
wake, mwalimu mkuu wa shule hiyo, Hazam Nambunga, alikiri kukumbwa na
changamoto hizo na kusema kuwa nyumba za walimu zilizopo ni mbili ambazo moja
anaishi mwalimu mkuu na nyingine anaishi mwalimu mwingine mmoja.
Aidha,
alisema, shule hiyo nakabiliwa pia ukosefu wa ofisi ya waalimu ambapo ambayo
ilikuwa ikitumika jingo lake lipo katika hali mbaya na halifai kutumika tena
kiasi cha kulazimika kutumia darasa moja kama ofisi ya waalimu na kwamba
wanafunzi wa darasa la awali ambao walikuwa wakisomea katika chumba hicho kusomea
chini ya miti.
“Tunamwomba
Mhe. Rais wa awamu ya tano, pamoja na mambo mengine, aangalie sana na kuboresha
masilahi ya walimu zaidi kuboresha miundombinu kwa kutujengea nyumba bora za
walimu” alisema.
No comments:
Post a Comment