Na Juma
Mohamed.
Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani hapa, kimeutaka uongozi wa chama hicho
ngazi ya Taifa kufika haraka kwa ajili ya kutatua mgogoro uliopo baina ya
viongozi wa chama ngazi ya mkoa na wilaya.
Akizungumza
na Nipashe, Kaimu katibu wa chama hicho wilya ya Mtwara, Salum Sudi (Saibogi),
alisema hali ya chama kwa sasa ni mbaya kutokana na uwepo wa kundi la watu 14
ambalo ndani yake wamo waliokuwa viongozi wa chama hicho kabla ya kupinduliwa
kama inavyodaiwa, linalokivuruga chama.
Alisema,
watu hao wakiongozwa na aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa mkoa, Kasim Bingwe na
Katibu wa mkoa, Willy Mkapa ambao kwa upande mwingine bado wanatambulika kama
viongozi halali, linafanya mbinu chafu za kukivuruga chama na kupangua kila
kitu kinachofanywa na viongozi waliopo kwa madai kuwa wao ndio viongozi halali
wa chama hicho.
Alisema,
uongozi uliopo ambao yeye ndio anakaimu nafasi ya ukatibu uliingia madarakani
mwezi Septemba mwaka huu baada ya maamuzi ya mkutano wa dharula wa baraza la
mashauriano la mkoa, ambapo liliamua kuuondoa uongozi wa awali uliokuwa chini
ya mwenyekiti Kasim Bingwe na katibu Willy Mkapa kwa madai kuwa haukuridhishwa
na utendaji wao wa kazi.
“Sasa
kilichotokea ni kwamba baada ya kundi hili ambalo liliondolewa na balaza la
mashauriano la mkoa, likawaachisha hawa kina Bingwe na huyu Mkapa,
walichokifanya wakaja wakaungana na kutengeneza kundi lao la kubishana na
uongozi wa kikatiba wa Chadema wilaya na ule wa mkoa, wao wakaenda moja kwa
moja na kundi la Chama Cha Wananchi (CUF) bila kujali taratibu za UKAWA..swala
hili mimi naongea kwa masikitiko makubwa sana nikiwa kama Chadema damu..”
alisema.
Alisema,
jambo lingine linalopelekea kuwepo kwa mgogoro ndani ya chama hicho ni kutokana
na matumizi mabaya ya fedha za ‘chakula’ zilizotolewa na makao makuu kwa ajili
ya kuwalipa mawakala wa chama waliosimamia na kulinda kura kipindi cha
Uchaguzi, na kwamba alidai fedha hizo ambazo alikabidhiwa Diwani wa viti
maalumu, Lulu Abdallah, hazikutumika kama ilivyopangwa.
“Baadae
tulipata kufahamu matumizi ya fedha zile kwamba zipo ambazo alikabidhiwa diwani
wa Kata ya Ufukoni (CUF) zingine alikabidhiwa diwani wa Tandika na hii ya
Vigaeni ilikoenda haijulikani..kilichozaliwa tukafanya utafiti tukaamini ni
hivyo na tukasema huyu mtu hatufai, baada ya kumuhoji yeye anasema tuulize
makao makuu, kuna mtu alikuja sijui kutoka Ngome, tukasema hela si ulipewa wewe
si unatajwa na hawa madiwani, tunazihitaji tuwalipe mawakala..tukaanza sasa
kupambana na mawakala ambao ni kundi wanadai pesa yao ya Chakula, ikawa ni
shida kweli..” alisema.
Alisema,
baadae walikaa na mawakala na kuwaeleza ukweli juu ya fedha hizo ambapo
waliwaelewa na mpaka sasa bado mawakala hao hawajalipwa.
Aidha,
matatizo yote yaliyopo yanasababishwa na hilo kundi la watu 14 ambalo anaamini
kuwa linapata nguvu kutoka kwa Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema upande wa Zanzibar,
Salum Mwalimu, kutokana na namna alivyo karibu nao na kuwasiliana nao mara kwa
mara kwa masuala mbalimbali ya chama.
Jambo
lingine linalolalamikiwa kwa hilo kundi ni juu ya mchakato wa kumpata Naibu
Meya wa manispaa ya Mtwara Mikindani ambapo kulitokea mkanganyiko baada ya
kupendekezwa watu wawili ndani ya chama kimoja kuwania nafasi hiyo.
Upande mmoja
uliwasilisha barua manispaa wakimpendekeza Diwani wa Kata ya Shangani, Mbarale
Ahmad huku upande mwingine ukiwasilisha barua inayompendekeza Diwani wa Kata ya
Rahaleo, Erick Mkapa.
Hata hivyo,
Mkapa ambaye alipendekezwa na uongozi unaoongozwa na mwenyekiti Bingwe, barua
yake ilikatiliwa kwa madai kuwa imekosa vigezo ambapo Mbarale aliyependekezwa
na uongozi wa kina Saibog alikubaliwa na kupigiwa kura za ndio au hapana ambapo
hata hivyo kura za hapana zilikuwa nyingi na kumfanya ashindwe kupata nafasi ya
Naibu Meya. Uchaguzi huo utarudiwa.
“Na hawa wtu
14 ndio wanakivuruga chama Mtwara mjini, na kikubwa wanachojivunia
wanafahamiana na viongozi wakubwa wa Chadema wa Kitaifa ambao sisi tunadharaulika,
jambo ambalo lilibidi litembee kikatiba, na huyu wanayemtumia ni Salum Mwalimu,
wao wanasema sisi tunajizuuka kwenye wilaya wao wanacheza juu, na kweli
inatusumbua, huyu Salum Mwalim anatusumbua kwelikweli..haya mengine anayoyaleta
huku hatuelewi kama chama na anasoma katiba, na inafikia hatua sasa tunajiuliza
sisi tumekaa kwa hidhini ya katiba ya Chadema au kwa hidhini ya Salum
Mwalimu?..” alihoji.
Kwa upande
wake, diwani wa viti maalumu anayelalamikiwa, Lulu Abdallah, alisema Chadema
kama chama ambacho ni miongoni mwa vyama vinavyounda Umoja wa Kaiba ya Wananchi
(UKAWA) kinafanya shughuli zake kwa kushirikiana na vyama vingine vya umoja huo.
“Na mimi
kama mwanachadema wa mkoa wa Mtwara, kama ni diwani wa viti maalumu wa mkoa wa
Mtwara, nasema nilifanya kazi pamoja na CUF, CHADEMA, NCCR na NLD na tukampata
Mbunge ambaye ni Maftaha Nachuma na tukawapata Madiwani ambao ni CUF na
Chadema, na sasaivi tunaendelea na kazi zetu ndani ya manispaa yetu, kama kuna
mgogoro ndani ya Chama, naomba ushughulikiwe ndani ya chama na sio kupeleka
kwenye vyombo vya habari au serikali ambao hawahusiki kabisa na migogoro yetu
ndani ya chama..” alisema Lulu.
Kwaupande
wake, Willy Mkapa ambaye amelalamikiwa na kutajwa katika kundi la watu 14,
alisema swala la kupendekezwa kwa Erick Mkapa kugombea Unaibu Meya ilitokana na
taarifa zake kupelekwa katika uongozi wa Kitaifa kasha wao ndio walitoa maamuzi
ya kuamua Mkapa agombee nafasi hiyo kutokana na wasifu wake na hata hivyo mpaka
wanafikia maamuzi ya kupeleka taarifa hizo makao makuu, taarifa za Mbarale
zilikuwa bado hazijawafikia.
Kuhusu swala
la kukataliwa kwa Mkapa, alielekeza lawama kwa mkurugenzi wa manispaa kwa kudai
kuwa hakufuata taratibu, kwasababu alitakiwa kufuata maamuzi ya ngazi za juu na
si vinginevyo.
“Sawasawa na
Rais awe ameteuwa alafu waziri anakuja kuvunja, kitu kama hicho mimi sijawahi
kuona..kwahiyo mimi nasema tu kwamba huu mchakato mpaka kufikia pale
umeharibiwa kwanza na serikali, na kama mkurugenzi aliona kama kunatatizo
angewaita wagombea wote ofisini kwake akakaa nao na kuwaambia zimekuja barua
mbili, hebu rudini kwenye chama mkakubaliane mlete barua moja, lakini ukumbini
ndio ameanza kuzisoma zile barua..” alisema.
Aliongeza kuwa,
mawakala kuto kulipwa pesa zao taarifa hizo sio sahihi kwasababu kuna baadhi ya
maeneo walienda kama UKAWA hasa katika kusimamia kura za Rais, ambapo maeneo
mengine Chadema hawakuwa na mawakala kwahiyo walitumia mawakala wa CUF
kusimamia, kwahiyo tuliwaachia wao.
No comments:
Post a Comment