Mtia nia ya kugombea Udiwani katika kata ya Shangani, Mtwara mjini, Mbarale Ahmad Mbarale alipokuwa akizungumza na wanahabari jana juu ya azma yake ya kuitaka kata hiyo. (PICHA NA JUMA MOHAMED) |
Na Juma
Mohamed, Mtwara.
Mtia nia ya udiwani katika kata ya Shangani, Mtwara mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA) Mbarale Ahmad Mbarale amesema kata hiyo inakabiliwa na changamoto nyingi ambazo ni pamoja na tatizo sugu
la ukosefu wa ajira kwa vijana, uchafu wa mazingira na hali duni ya kiuchumi
kwa akina mam.
Akizungumza
na NEWS ROOM jana, Mbarale ambaye tayari ameshachukua fomu ya kuwania nafasi hiyo
kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), alisema kuwa yapo matatizo
mengi ambayo wananchi wa kata hiyo ambayo ilikuwa chini ya Meya wa manispaa ya Mtwara Mikindani Selemani Mtalika (Shilingi) wanakumbana nayo na kwa kutumia elimu yake
na uwezo wa kiuongozi alionao, atahakikisha anafanyia kazi na kuyamaliza.
“Simaanishi
kwamba hakuna kilichofanyika, yapo ambayo yamefanyika lakini naamini
hayajafanyika katika ubora ambao watu watajua kuwa vimefanyika..lakini mimi kwa
mtazamo wangu naona bado kuna haja ya kuboresha zaidi..”alisema.
Alisema uamuzi
wake wa kuitaka kata hiyo umekuja baada ya kuangalia changamoto zote zilizopo
na kujipima uwezo wake na kuona kuwa anatosha kuwaondolea kero zao wananchi wa
kata hiyo kupitia uzoefu na elimu yake aliyonayo ya kiutawala na biashara.
Aidha,
Mbarale ambaye ana shahada ya kwanza aliyoipata chuo kikuu cha Dar es Salaam
alisema amefanya kazi na mashirika na kampuni mbalimbali kwa kipindi
kisichopungua miaka nane, ikiwa ni pamoja na shirika la Basic Needs mkoani hapa
kwa kipindi cha miaka miwili na kampuni moja ya mtandao wa mawasiliano ambako
alifanya kwa mika mitano.
“Kwa kutumia
uzoefu huo nilionao wa kutumikia mashirika na kampuni mbalimbali kwa kipindi
hicho, na kwa kuishi Mtwara kwa muda mrefu huku nikishuhudia mabadiliko mengi
ya uongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) yaliyofanywa na kushindwa kutimiza
matakwa na mahitaji ya wananchi..mimi binafsi nikapata hiyo nia pamoja na
kushauriwa na baadhi ya watu wenye nia njema kwamba nichukue fomu ili niweze
kugombea.” Aliongeza.
No comments:
Post a Comment