Tuesday, November 24, 2015

TCRA yawapa fursa wananchi kuwasilisha maoni juu ya mienendo ya vipindi, Redio/Tv.

Mwenyekiti wa kamati ya maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mhandisi-Margaret Munyagi (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya wajibu wa watangazaji wa redio na Tv katika kufuata maadili ya kazi zao. Wakwanza kulia ni aliyekuwa mtangazaji wa TBC Taifa zamani ikijulikana kama Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD), Abdul Ngarawa.


Mwandishi wa habari wa Mtukwao Media-Gregory Milanzi, akitekeleza majukumu yake.


Waandishi wa habari waliohudhuria mkutano wa kamati ya maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania-TCRA, juu ya wajibu wa watangazaji wa redio na Tv katika kufuata maadili ya kazi zao, uliofanyika leo katika ukumbi wa Naf Beach, Mtwara



Na Juama Mohamed.

WANANCHI wametakiwa kuwa makini katika ufuatiliaji wa vipindi mbalimbali vya Redio na Televisheni na kuwasilisha maoni yao katika Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) iwapo wanabaini ukiukwaji wa maadili kutoka kwa watangazaji.
Akizungumza jana mkoani hapa, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhandisi Margaret Munyagi, alisema wasikilizaji wana haki ya kulalamika katika kamati hiyo iwapo wanabaini kuwepo kwa dosari za kimaadili kwa watangazaji kiasi cha kusababisha uchochezi au uvunjifu wa amani.

Waandishi wa habari


“Watumiaji wa huduma hii wana haki ndani ya mujibu na kanuni ambazo zinatawala utangazaji, kwahiyo mtumie haki mliyonayo kama wasikilizaji..mna kofia mbili mnatoa huduma lakini pia taarifa iwafikie watumiaji waliopo ili watumie fursa hiyo kuweza kuleta malalamiki..unaposikia kipindi na maudhui na hujaridhika nayo unaona kabisa ni kinyume na utamaduni wan chi hii na ukiona kwamba kuna uchochezi, una haki kabisa kama msikilizaji kuileta kwenye kamati kwa ajili ya kuweza kuishughulikia..” alisema.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui-TCRA, Margaret Munyagi.


Alisema, mamlaka kupitia kamati hiyo inaimiza matumizi ya Lugha sanifu na kwamba kwakua Kiswahili ndio Lugha ya Taifa hapa nchini, vyombo vya habari kupitia vipindi vyao vina wajibu wa kuhakikisha kwamba lugha hiyo inakuzwa na kutambulika zaidi Kimataifa.
Alisema, chombo cha habari cha Taifa kama ilivyo kwa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kina wajibu mkubwa wa kukuza lugha kutokana na dhamana iliyonayo na kukemea watangazaji wanaotumia lugha za mkato na ambazo hazipaswi kusikika katika vyombo vya habari.

Mjumbe wa kamati ya maudhui ya TCRA-Abdul Ngarawa


“Tunajua kabisa kama Uingereza kupitia chombo chao cha Taifa kile BBC ndio kiini cha kuhakikisha kwamba lugha yao inakua na kutumika vizuri, kwahiyo tunategemea na sisi kupitia vyombo hivi vitatumika kabisa kukuza lugha yetu ya Kiswahili sanifu kabisa..lakini pia tunatambua kuwa Kiingereza kinatumika katika nchi hii, basi Kiingereza kinachotumika kiwe sanifu mjitahidi sana..” aliongeza.
Aidha, alitaja majuku ya kamati hiyo kuwa ni pamoja na kumshauri waziri wa habari juu ya sera inayohusu mambo ya utangazaji hapa nchini, kusimamia utekelezaji wa kanuni za utangazaji, maudhui/vitu vinavyotangazwa kupitia Redio na Televisheni pamoja na kuchambua malalamiko ya wasikilizaji.

Afisa sheria mwandamizi wa TCRA-Hassan Mwanga, akifafanua jambo



Naye, afisa sheria mwandamizi wa mamlaka hiyi, Hassan Mwanga, alitoa rai kwa waandishi na watangazaji wa Redio na Tv kufuata maadili ili kuhepuka kuchukuliwa hatua za kimaadili na mamlaka, kwani wapo ambao wameonesha kukiuka na mara kadhaa wameitwa katika kamati.

No comments: