
Rais wa makampuni ya Dangote Aliko Dangote
Na Philipo Lulale, Mtwara.
Wananchi
wa Tanzania wamepongezwa kwa kubadilisha uongozi wa nchi kwa amani na utulivu
kupitia utaratibu wa kidemokrasia,hali ambayo inaelezwa ni kigezo muhimu kwa
nchi kueendelea kuvutia wawekezaji wengi wa nje kuwekeza hapa nchini.
Rais na
mtendaji mkuu wa makampuni ya Dangote ya Nigeria alhaji Aliko Dangote alitoa
pongezi hizo katika kijiji cha Msijute wilaya na mkoa wa Mtwara, alipokuwa
anazunguumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua kiwanda chake cha
saruji kinachotarajiwa kuanza uzalishaji wakati wowote wiki ijayo.
Alisema
ana imani kuwa raisi mpya wa Tanzania ataendeleza mahali alipoachia mtangulizi
wake na kuipeleka nchi kutoka ilipo,kwenda hatua nyingine ya maendeleo.
Alisisitiza
kuwa licha ya kuendelea kuombea nchi hii na uongozi mpya,pia wawekezaji kama
yeye wanatakiwa kuunga mkono jitihada za serikali kuhakikisha uwekezaji
endelevu utakaosaidia kuivusha nchi kutoka mahali ilipo sasa hadi hatua
nyingine.
Kwa
mujibu wa bw. Dangote watanzania wategemee fursa za ajira za kutokana kupitia
uwepo wa kiwanda hicho kikubwa kuliko vyote katika ukanda wa Afrika mashariki
na kati,kitakapoanza uzalishaji kwani kusafirisha mzigo wa tani milioni 3
unahitaji angalau malori makubwa ya mizigo kati ya 600 hadi 700 ambapo 30%
yatakuwa ni kwa ajili ya Tanzania.
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa makampuni ya Dangote bw. Sada Ladambeki alieleza kuridhishwa na hotuba ya raisi Dr John Magufuli aliyoitoa wakati wa uzinduzi wa bunge na kwamba kile kinachoonekana katika nchi ya Tanzania inatia moyo sana kuwekeza katika nchi hii kutokana na uwepo wa hali ya amani na utulivu.
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa makampuni ya Dangote bw. Sada Ladambeki alieleza kuridhishwa na hotuba ya raisi Dr John Magufuli aliyoitoa wakati wa uzinduzi wa bunge na kwamba kile kinachoonekana katika nchi ya Tanzania inatia moyo sana kuwekeza katika nchi hii kutokana na uwepo wa hali ya amani na utulivu.
Alisema
kile alichosisitiza riais ni utawala bora katika maeneo yote ambapo watu lazima
wafanye vitu kwa njia sahhi ili wawekezaji kama wao waweze kujiamni
wanapowekeza hapa nchini.
“Kama
kichwa kikiwa kizuri mwili wote utakuwa mzuri,kama kichwa kimeoza basi mwili
wote umeoza hiyo ni kanuni ya samaki” alisisitiza alhaji Sada.
“ukiwa
na kiongozi mzuri anayefanya mambo kwa usahihi kila kitu kitakwenda
vizuri,tunamwamini na tutafanya kila tunaloweza kufanya kuweza kumsaidia”
alikazia.


Ester Baruti-mkurugenzi mkazi wa Dangote
company.
Kwa
upande wake mwakilishi mkazi wa kampuni ya Dangote nchini Tanzania Ester Baruti
amewataka watanzania,wawekezaji na watendaji serikalini kwa ujumla
kushirikiana ili kumsaidia raisi wa Tanzania kutimiza azma ya kuwatumikia
watanzania na kukuza uchumi
Alisema kwa mujibu wa hotuba ya mheshimiwa Magufuli wakati wa uzinduzi wa bunge la 11,inaonyesha nia yake ya kuhakikisha Tanzania inafikia mabadiliko makubwa ya kiuchumi katika kipindi cha miaka mitano ijayo.
Alisema kwa mujibu wa hotuba ya mheshimiwa Magufuli wakati wa uzinduzi wa bunge la 11,inaonyesha nia yake ya kuhakikisha Tanzania inafikia mabadiliko makubwa ya kiuchumi katika kipindi cha miaka mitano ijayo.
“Ninaomba
sana tupendane watanzania,tuheshimiane,kuacha kudharauliana na kuthamini
michango ya kila mtu katika nchi” alisisitiza.
Kwa
mujibu wa Baruti nchi yetu ina wageni wengi wanaokuja kwa shughuli
mbalimbali,miongoni mwao wakiwemo wanaoitakia mema nchi yetu na wengine
wasioitakia mema nchi yetu.
![]() |
Alhaj Dangote akiongea na waandishi wa habari katika eneo kilipo kiwanda chake katika kijiji cha Msijute mara baada ya kukagua |
Alhaji
Aliko Dangote amewekeza zaidi ya dola za kimarekani milioni 600 kujenga kiwanda
kikubwa cha saruji mkoani Mtwara kinachosadikiwa kuwa kikubwa katika ukanda wa
Afrika mashariki na kati na kina uwezo wa kuzalisha tani milioni 3 kwa mwaka na
kwa sasa kiko katika hatua za mwisho kuanza uzalishaji.
Kutokana
na hali ya amani na utulivu mwekezaji huyo anatarajia kuwekeza katika maeneo
mengine ya uwekezaji hapa nchini ikiwemo kilimo.

No comments:
Post a Comment